Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Wakurugenzi acheni kubana fedha za Lishe - Prof. Shemdoe

Imewekwa tar.: April 28th, 2021

Na Atley Kuni, DODOMA.

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Prof. Riziki Shemdoe amewataka wakurugenzi wa Halmashauri nchini kuhakikisha fedha zinazotengwa katika bajeti kwa ajili ya shughuli za afua za lishe zinatolewa ili kutokwamisha kazi hizo.

Akifungua kikao cha siku tatu leo tarehe 28 Aprili, 2021, mjini Dodoma, Prof. Shemdoe amesema kila mwaka serikali imekuwa ikitenga fedha kwa ajili ya kushughulikia masuala ya afua za Lishe, lakini tatizo hutokea wakati wa upangaji wa vipaumbele.

Amesema licha ya ongezeko la bajeti katika mamlaka za serikali za mitaa kutoka Sh. bilioni 11.6 mwaka 2017/18 hadi Sh.bilioni 16.87 2019/20 lakini kumekuwa na utoaji wa fedha za afua za lishe usio wa kuridhisha.

“Kuanzia sasa pamoja na vipimo vingine vya ufanisi vinavyotumika kuwapima Wakurugenzi, suala la afua za lishe kitakuwa ni kigezo muhimu katika kuwapima watendaji hao, hivyo lazima wahakikishe masula yote ya suala la Lishe yanapewa kipaumbele” amesema Prof. Shemdoe.

Pia, Katibu Mkuu amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri nchini kuzingatia miongozo inayotaka kutengwa Sh.1000 kwa kila mtoto aliye chini ya miaka mitano kwa ajili ya lishe.

Katika hatua nyingine Katibu Mkuu Shemdoe hakusita kuwanyooshea vidole wadau wanaoshirikiana na Serikali kwa kuwataka kushirikiana na mamlaka za serikali za mitaa wanapotekeleza miradi yao na kutoa taarifa kila robo mwaka ikiwepo taarifa za fedha wanazopokea kutoka kwa wafadhili kuingizwa kwenye mipango ya Bajeti za Halmashauri.

“Tukifanya hivyo tutaepuka kupeleka fedha eneo moja na kufanya shughuli zile zile, bado kuna wadau wanafanya shughuli za lishe bila kuzingatia mkataba waliowekeana na uongozi, Mashirika yasiyo ya serikali yanayofanya shughuli za lishe wahakikishe wanashirikiana na TAMISEMI na mamlaka zingine zilizo chini ya Ofisi hiyo wakati wa utekelezaji,”alisema.

Akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha katibu Mkuu kufungua Mkutano huo, Mratibu wa Lishe, TAMISEMI, Mwita Waibe, alisema tangu kuanzisha idara katika mamlaka za serikali za mitaa pamoja na mambo mengine wameanzisha mfumo wa (Information Management Monotoring and Evaluation System -IMES), ambao unafuatilia na kupata takwimu sahihi za afua za lishe.

Mwita alisema sekta ya lishe ina changamoto ya watumishi kwani katika mikoa 26 ni mikoa 20 tu yenye wataalamu wa lishe na kati ya halmashauri 184 ni halmashauri 66 pekee zenye wataalamu hao.

Akizungumza kwa niaba ya washiriki 80 wa mkutano huo, Mwenyekiti wa Maofisa Lishe nchini, Bibi, Bertha Donald ameiomba serikali kuhimiza utoaji wa fedha zinazotengwa kwa ajili ya lishe katika halmashauri.

“Mtakumbuka Waziri wa Nchi Mhe. Ummy Mwalimu alinukuliwa akisema “Wakurugenzi wa halmashauri ambao halmashauri zao hazijafikia asilimia 50 ya ukusanyaji mapato hawatoshi,” Hivyo tungefurahi kusikia pia Wakurugenzi watakaoshindwa kutenga na kutoa kipaumbele kwenye fedha za Lishe hawatoshi”

Kikao hicho cha siku tatu, kitatumika Kujadili, uratibu na utekelezaji wa afua za lishe katika ngazi ya Mikoa na Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2020/21 sambamba na kuona mafanikio yaliyopatikana kisha kuweka mikakati endelevu kwenye sekta hiyo muhimu nchini.

Mwita Waibe Mratibu wa masula ya Lishe TAMISEMI alipokuwa akimkaribisha Katibu Mkuu

Katibu Mkuu Prof. Riziki Shemdoe akifungua mkutano huo.

Bibi Bertha Donald, akitoa salama za umoja wa Maafisa Lisha hao.

Baadhi ya Maafisa Lishe wa Wizara, Mikoa na Halmashauri, wakiwa wanasikiliza Hotuba ya Ufunguzi

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert May 12, 2025
  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert May 12, 2025
  • Fursa kwa Wahitimu wa Kidato cha Nne 2024 kubadili Tahasusi na Kozi April 02, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI AJIRA ZA AFYA - TAMISEMI 2025 March 15, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI

    May 23, 2025
  • PJT-MMMAM Yawezesha Uanzishwaji wa Vituo 206 vya Malezi ya Watoto Wadogo

    May 21, 2025
  • SERIKALI KUJENGA DARAJA LINALOUNGANISHA KIJIJI CHA NEGERO – KILINDI

    May 21, 2025
  • MHE. MCHENGERWA ABORESHA TAARIFA ZAKE KWENYE  DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

    May 20, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.