Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Waganga Vituo vya afya, Wakuu wa shule jifunzeni elimu ya uhasibu

Imewekwa tar.: June 13th, 2018

Na Mathew Kwembe, Kagera

Waganga Wafawidhi wa Vituo vya Afya, Zahanati na Walimu Wakuu wa Shule za Msingi na Sekondari wanaopelekewa fedha na serikali moja kwa moja kwenye vituo vyao wametakiwa kujifunza elimu ya uhasibu ili waweze kutekeleza majukumu yao uafisa masuuli ya usimamizi wa fedha za serikali.

Ushauri huo umetolewa jana na Meneja wa Mradi wa Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma wa Mkoa wa Kigoma bwana Simon Mabagala wakati wa mahojiano maalum kuelezea alichojifunza kuhusu watendaji hao wa ngazi za chini wa Mamlaka za Serikali za Mitaa wanavyotekeleza majukumu yao kupokea fedha na kupitisha maamuzi ya matumizi ya fedha hizo kwa kupitia mfumo huo wa kielekitroniki.

Alisema kuwa baadhi ya walimu wakuu na waganga wafawidhi wamekuwa wakisita kutekeleza jukumu hilo uhasibu kwa kuwa taaluma zao ni tofauti lakini kutokana na uamuzi huo wa serikali wa kupeleka fedha moja kwa moja katika vituo vyao watalazimika kujifunza elimu ya uhasibu  ili waendane na majukumu yao ya uafisa masuuli katika  vituo vyao.

Bwana Mabagala aliongeza kuwa watendaji hao hawawezi kukwepa kujifunza elimu ya uhasibu kwani kwa jukumu lao la uafisa masuuli wasipoweza kuwa na elimu ya uhasibu kidogo wanaweza kushindwa kutekeleza majukumu yao.

“Kwa kuwa msimamizi wa kituo moja kwa moja wewe ni afisa masuuli, unalazimika kufahamu mambo ya msingi ya uhasibu kwani kushindwa kufahamu majukumu maana yake hela wasikuletee, kwani serikali haiwezi kukuletea hela, wakati wewe ndiyo msimamizi wa kituo, ni lazima uweze kuzisimamia na kuzitolea taarifa,” alisema.

Kwa upande wake Mhasibu wa Halmashauri ya Wilaya ya Kahama bwana Edwin Lupili alieleza kuwa katika halmashauri yake vituo vyote vya afya vimeletewa wahasibu, hivyo suala la kupeleka fedha moja kwa moja katika vituo hivyo linafanyika bila tatizo kwa kuwatumia wahasibu.

Aliongeza kuwa katika shule za msingi na sekondari kumekuwa na changamoto za kupata wahasibu watakaotosheleza vituo hivyo hasa kwa kuzingatia kuwa idadi ya shule za msingi nchini ni zaidi ya 16,000 na shule za sekondari ni zaidi ya shule 3600.

Sababu nyingine ya kutolazimika kuweka mhasibu kwa kila shule ni kutokana na kiwango cha fedha kinachopelekwa katika shule hizo kutokuwa kikubwa kiasi cha kuhitaji kuajiri mhasibu kwa kila shule.

Bwana Lupili aliongeza kuwa pamoja na serikali kutokuajiri wahasibu wanaoweza kukidhi mahitaji ya kila shule nchini, bado walimu wakuu na waganga wa vituo vya afya wana fursa ya kupata msaada wa kitaalamu kupitia miongozo ya serikali ambayo imeainisha mchanganuo wa matumizi wa fedha zinazopelekwa kwenye vituo.

Pia alisema kuwa zipo kamati za shule na afya ambazo zimekuwa zikipigwa msasa kuhusu mambo ya uhasibu na hivyo kusaidia jukumu la usimamizi na udhibiti wa matumizi ya fedha za serikali zisitumike kinyume na miongozo kwenye vituo hivyo.




Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert May 12, 2025
  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert May 12, 2025
  • Fursa kwa Wahitimu wa Kidato cha Nne 2024 kubadili Tahasusi na Kozi April 02, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI AJIRA ZA AFYA - TAMISEMI 2025 March 15, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI

    May 23, 2025
  • PJT-MMMAM Yawezesha Uanzishwaji wa Vituo 206 vya Malezi ya Watoto Wadogo

    May 21, 2025
  • SERIKALI KUJENGA DARAJA LINALOUNGANISHA KIJIJI CHA NEGERO – KILINDI

    May 21, 2025
  • MHE. MCHENGERWA ABORESHA TAARIFA ZAKE KWENYE  DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

    May 20, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.