Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Vituo vya Afya 234 Kuboresha Huduma ya Afya ya Kinywa na Meno

Imewekwa tar.: November 23rd, 2022

Na Fred Kibano, Mwanza    

Serikali imewataka Watendaji wa Halmashauri nchini kufanya tathmini ya rasilimali zilizopo kwenye vituo vya afya 234 vinavyojengwa kwa fedha za Tozo ili kuboresha huduma za afya ya kinywa na meno.

Kauli hiyo ya Serikali imetolewa na Dkt. Grace Magembe Naibu Katibu Mkuu (AFYA) Ofisi ya Rais TAMISEMI wakati akifunga Mkutano wa Madaktari wa Afya ya Kinywa na Meno wa Mikoa Tanzania Bara jana Novemba 22, 2022, uliofanyika katika Ukumbi wa TMDA, Jijini Mwanza. Dkt. Magembe ameongea kwa njia ya Mtandao (Zoom).

“vituo vya afya 234 vya Tozo vinavyojengwa kuna vyumba mahsusi kwa ajili ya kutoa huduma za afya ya Kinywa na Meno, natoa maelekezo kwa Halmashauri zote kutathmini rasilimali walizonazo na kuwekeza katika vituo hivi hususan vile ambavyo kuna mahudhurio makubwa ya wateja” amesema Dkt. Magembe.

Dkt. Magembe amesema Ofisi ya Rais TAMISEMI itaendelea kuboresha huduma za afya ya kinywa na meno, kuratibu huduma za afya ya msingi kulingana na Sera na Miongozo iliyopo pamoja na hatua nzuri iliyofikiwa mpaka sasa ambapo huduma hizo zinatolewa kwenye hospitali za Halmashauri 159 sawa na asilimia 86 ikilinganishwa na asilimia 56 mwaka 2019.

Aidha amesema jumla ya vituo vya afya 173 vikiwemo vituo 164 vya serikali na vituo 9 vya mashirika ya dini vinatoa huduma kwa sasa sawa na ongezeko la vituo 46.

Kwa upande wa watumishi wanaotoa huduma katika vituo tajwa hapo juu wapo watumishi 614 kati ya mahitaji ya 1894 sawa na uwepo wa watumishi kwa asilimia 32 ikilinganishwa na asilimia 24 mwaka 2019.

Aidha, amesema Serikali imeajiri watumishi 145 wa afya ya kinywa na meno kwa ajili ya huduma za afya ya msingi wakiwemo matabibu wa meno 142 na madaktari wa kinywa na meno watatu waliajiriwa sambamba na utoaji wa shilingi Bilioni 7.1 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya afya ya kinywa na meno na huduma za macho kwa hospitali 71 za Halmashauri ambapo mpaka sasa shilingi Bilioni 1.7 zimeshatumwa katika Halmashauri.

Dkt Omary Chande Mwenyekiti wa Madaktari wa Afya ya Kinywa na Meno wa Mikoa Tanzania Bara maagizo yote watayatekeleza kama ilivyoagizwa na Serikali lakini pia ameshukuru kutengwa bajeti ya vifaa tiba shilingi Bilioni 7.1 pamoja na ujenzi wa vituo vya afya vya kimkakati.

Naye Katibu wa Waganga Wakuu wa Wilaya (DMOs) Dkt. Lusubilu Adam amesema mkutano huo umekuwa na manufaa kwake kwani amejifunza vitu vingi ambavyo vitaleta matokeo kwenye maeneo yao ya kazi ikiwa ni pamoja na kufanya kazi kwa pamoja na Wataalam wa Afya ya Kinywa na Meno na uandaaji wa mipango na bajeti ya sehemu ya kinywa na meno.  

Mkutano huo wa siku mbili ulifunguliwa mapema jana na kauli mbiu yake inasema “Mchango wa Takwimu bora za afya ya Kinywa na Meno katika kufikia maamuzi na utekelezaji” inayosisitiza matumizi ya takwimu bora na kufanya maamuzi sahihi yenye tija katika utoaji wa huduma za afya ya Kinywa na Meno nchini.





Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert May 12, 2025
  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert May 12, 2025
  • Fursa kwa Wahitimu wa Kidato cha Nne 2024 kubadili Tahasusi na Kozi April 02, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI AJIRA ZA AFYA - TAMISEMI 2025 March 15, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI

    May 23, 2025
  • PJT-MMMAM Yawezesha Uanzishwaji wa Vituo 206 vya Malezi ya Watoto Wadogo

    May 21, 2025
  • SERIKALI KUJENGA DARAJA LINALOUNGANISHA KIJIJI CHA NEGERO – KILINDI

    May 21, 2025
  • MHE. MCHENGERWA ABORESHA TAARIFA ZAKE KWENYE  DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

    May 20, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.