Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

USHIRIKISWAJI WA WADAU: NGUZO MUHIMU KUFIKIA MALENGO YA MRADI

Imewekwa tar.: June 25th, 2024

USAID Kizazi Hodari Kanda ya Kusini ni mradi unaofadhiliwa na watu wa Marekani kupitia shirika ya misaada la USAID. Mradi huu unatekelezwa na shirika la Deloitte Consulting kwa kushirikiana na taasisi za kiraia (CSOs) na wadau wengine muhimu katika mikoa kumi na moja nchini Tanzania. Ushirikiano huuunalenga kuimarisha uhusiano kati ya vituo vya afya na jamii, kujenga uwezo, na kutoa huduma bora kwa walengwa.

Mradi unalenga kuboresha upatikanaji wa huduma za afya, ustawi, na ulinzi kwa Watoto Yatima na Vijana wanaoishi katika mazingira hatarishi (OVC) katika jamii zenye idadi kubwa ya maambukizi ya VVU ndani ya Kanda ya Kusini ya Tanzania. Mradi unalenga kuchangia Malengo ya 95-95-95: kuhakikisha kwamba ifikapo mwaka 2030, asilimia 95% ya Watu Wanaoishi na VVU (PLHIV) wanajua hali yao, asilimia 95% ya PLHIV wanaojua hali yao wanapata matibabu, na asilimia 95% ya PLHIV wanaopata matibabu wanapata kufubaza VVU.

Ili kuhakikisha uendelevu na kuendana na vipaumbele vya kitaifa, Mradi wa USAID Kizazi Hodari Kanda ya Kusini unafanya kazi kwa karibu na wizara tatu: Wizara ya Afya, TAMISEMI, na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, pamoja na Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS). Ushirikiano huu ni muhimu katika kuongeza uwezo wa kusimamia, kuboresha, na kuendeleza upatikanaji wa huduma na mifumo ya kusaidia OVC, na kuendeleza mchango wa mradi katika kudhibiti janga la UKIMWI.

Mnamo Tarehe 21 Juni 2024, wafanyakazi wa mradi wa USAID Kizazi Hodari Kanda ya Kusini walikutana na wadau muhimu wa Serikali mjini Morogoro kujadili mapendekezo ya utekelezaji wa mradi kwa mwaka wa fedha (FY25) utakaoanza Oktoba mosi 2024 na kukamilika Septenmba 2025. Kikao hiki cha siku mbili kilijumuisha mawasilisho ya mpango kazi uliopendekezwa, ambapo wawakilishi wa serikali walitoa michango na mapendekezo muhimu ili kuhakikisha mipango ya mradi inaendana na vipaumbele vya Serikali na upatikanaji wa huduma bora kwa walengwa.

Baada ya mawasilisho, mjadala mkubwa ulijikita katika maeneno tofauti, ikiwa ni pamoja na uendelevu wa mradi, kujengeaa uwezo wa wahudumu wa afya ngazi ya jamii, kushirikisha wadau mbalimbali katika ngazi tofauti, kuboresha mfumo wa rufaa kati ya vituo vya kutolea huduma za afya na watoa huduma ngazi ya jamii na kuimarisha mifumo ya serikali. Wawakilishi wa serikali walitoa ushauri muhimu juu ya kuboresha ushirikiano na kuhakikisha uendelevu baada ya mradi kuisha.

Washiriki wa kikao hicho walitembelea maeneo mbalimbali ya mradi, ikiwemo vituo vya afya, kaya, na vikundi vya kuimarisha uchumi. Madhumuni ya ziara hizi ilikuwa ni kuongeza ufahamu zaidi juu ya malengo mahususi ya mradi na namna unavyoboresha maisha ya walengwa.

Tunatoa shukrani zetu za dhati kwa wizara kwa ushirikiano wao endelevu. Ushirikiano huu ni muhimu katika nia ya kufikia malengo ya mradi ya kulinda na kuboresha maisha ya Watoto Yatima na Vijana wanaoishi katika mazingira hatarishi katika Kanda ya Kusini ya Tanzania.


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert May 12, 2025
  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert May 12, 2025
  • Fursa kwa Wahitimu wa Kidato cha Nne 2024 kubadili Tahasusi na Kozi April 02, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI AJIRA ZA AFYA - TAMISEMI 2025 March 15, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • NENDENI MKAITANGAZE SERIKALI.

    May 24, 2025
  • SOKO LA KISASA LA NYAMA CHOMA LAZINDULIWA VINGUNGUTI

    May 24, 2025
  • DKT. Biteko asisitiza wazazi kuthamini nafasi ya familia katika malezi na makuzi ya mtoto.

    May 24, 2025
  • Mhe. Rais Samia amtaka Prof. Nagu kuboresha  huduma ya afya ya msingi.

    May 24, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.