Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Ujenzi wa Shule ya Mfano Dodoma hauendani na Viwango vya Mfano

Imewekwa tar.: June 22nd, 2019

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.Selemani Jafo(Mb) amesema ujenzi unaoendelea wa shule ya mfano inayojengwa Mkoani Dodoma haiendani na viwango vya mfano ambavyo mtu yeyote akija atatambua kuwa hiyo ndio shule ya mfano.

Akikagua maendeleo ya ujenzi wa shule hiyo ya Msingi inayojengwa katika Kata ya Ipagala Jijini Dodoma wakati wa ziara yake Waziri Jafo ameyasema alitegemea kukuta kitu kitofauti na alichokikuta eneo la ujenzi kwa sababu Dodoma ndio Makao Makuu ya Nchi.

“Ujue mpaka shule inapewa hadhi ya kuwa ya mfano inatakiwa iwe ya utofauti mkubwa sana na shule za kawaida kuanzia kwenye ramani ya majengo, ukubwa wa eneo, muonekano wa majengo yanayojengwa, mandhari, viwanja vya michezo na kila kitu kitakachowekwa katika shule hiyo” Amesema Jafo

Aliongeza kuwa Sasa kwa hapa Ipagala kwanza ukiingia tu unaanza kuona eneo la shule limezingirwa na makazi ya watu kwa karibu sana halafu majengo yanayojengwa yote ni ya chini kama mabehewa ya Treni hamuoni kwa eneo lililopo hapa hamtapata nafasi ya kutosha kwa ajili ya kufanya vitu vingine vya Msingi.

Aidha Mhe. Jafo alifafanua kuwa “eneo mlilonalo la Ekari saba sio dogo kwa ujenzi wa shule ya kawaida lakini sio lakini kubwa kwa ujenzi wa shule ya mfano yaan hapa mlitakiwe mpate ekari hata thelathini kuwe na nafasi ya kutosha kisha mjenge majengo ya gorofa, vipatikane viwanja vya michezo vizuri, maeneo ya kupumzikia watoto na nyumba za walimu ziwe pembeni kidogo sio vitu vyote visongamane katika eneo moja;

Hii ni shule ya mfano inatakiwa kuwa na muonekano ambao kila mtu akija hapa atakubali kuwa kweli hapa ni eneo la mfano na wengine watakuja kujifunza kwaiyo sitafurahia kuona vitu vya kawaida kawaida tu lazima mjue kujiongeza”.

Aliongeza kuwa sitegemei kuona shule hii inafanana na shule ya Msingi Chaduru au Nzuguni B lazima iwe tofauti katika kila kitu, mkifanya mchezo nyie Dodoma ndio mtakuwa tofauti na wenzenu wote wanaojenga shule hizi za Mfano na watawazidi endeleni kufikiria kawaida tu.

Akizungumza katika ziara hiyo Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Belnith Mahenge alikiri kuwa wataalamu wa Dodoma hawakupanua mawazo yao katika kuangalia namna bora ya kutekeleza ujenzi wa shule ya mfano katika Mkoa wa Dodoma.

“Nikiri tu kuwa tumekosea na baada ya ziara hii ya Mhe. Waziri tukaa pamoja na wataalamu wetu kuangalia namna gani tunaweza kurekebisha kasoro hizi zilizojitokeza katika ujenzi huu wa Shule ya Mfano ili iwe na ubora unatakiwa katika shule hizi” Alisema Mahenge.

Naye Mkurgenzi wa Elimu Ofisi ya Rais TAMISEMI Julius Nestory ametaja vigezo vya shule za Mfano kuwa ni Uwepo wa Vyumba vya madarasa kuanzia 17 tofauti na shule za kawaida ambazo zina vyumba sita mpaka tisa na shule hiyo itajengwa eneo lenye idadi kubwa ya watu ambapo pia kutakua na idadi kubwa ya wanafunzi.

Nestory aliendelea kutaja vigezo vya shule ya mfano kuwa ni uwepo wa miundombinu muhimu kama Nyumba za Walimu, Maktaba, Ukumbi wa Mikutano, Jengo la Utawala, vyoo vya kutosha pamoja na viwanja vya michezo.

Alimaliza kutaja maeneo ambayo shule hizo zitajengwa Nchini kuwa ni Dodoma eneo la Ipagala, Kigome kule Buhigwe, Geita, Mtwara katika Halmashauri ya Wilaya ya Masasi na Mara kwenye shule aliyosoma Baba wa Taifa Mwl. Julius Nyerere ambayo ni Shule ya Msingi Mwisenge.

Naye Afisa Elimu Msingi Jiji la Dodoma Joseph Mabeyo amesema walipokea Tsh Mil 706 mnamo mwezi April 2019 na ujenzi unaondelea utahusisha vyumba vya madarasa 17, Maktaba, Bwalo la chakula, nyumba za walimu, matundu ya vyoo pamoja na Jjengo la Utawala na ujenzi huo unategemea kukamilika Mwezi Agosti, 2019.


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert May 12, 2025
  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert May 12, 2025
  • Fursa kwa Wahitimu wa Kidato cha Nne 2024 kubadili Tahasusi na Kozi April 02, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI AJIRA ZA AFYA - TAMISEMI 2025 March 15, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI

    May 23, 2025
  • PJT-MMMAM Yawezesha Uanzishwaji wa Vituo 206 vya Malezi ya Watoto Wadogo

    May 21, 2025
  • SERIKALI KUJENGA DARAJA LINALOUNGANISHA KIJIJI CHA NEGERO – KILINDI

    May 21, 2025
  • MHE. MCHENGERWA ABORESHA TAARIFA ZAKE KWENYE  DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

    May 20, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.