Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

“Timu za Afya Mikoani Mjipange Vizuri” Dkt. Gwajima

Imewekwa tar.: February 8th, 2019

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa, anayeshughulikia afya, Dkt. Dorothy Gwajima, ameziagiza timu za Afya za Mikoa (Regional Health Management Team- RHMT) yote nchini, kujitathmini hali yao ya utendajikazi na kuona kama wanatija inayokubalika kwa taifa.

Gwajima ameitoa kauli hiyo, alipokuwa akizungumza na timu ya Afya ya Mkoa wa Dodoma inayo ongozwa na James Kiologwe, Mganga Mkuu wa Mkoa huo wakati alipofanya ziara yake ya kwanza toka ateuliwe kushika wadhifa huo Januari 08,2019 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli.

Akiwa katika ziara hiyo, Gwajima alisema kila mmoja katika timu hiyo inayo simamia afya wajifanyie tathmini dhidi ya utendaji wao huku akisema, ametumia jukwaa hilo la timu ya Dodoma lakini na waliopo katika Mikoa Mingine yote nchini nao wajitathmini huko huko walipo wasingojee ziara yake ndio waanze kubadilika.

“Tatizo kubwa tulilonalo ni uratibu wa kazi, jukumu moja unakuta linakuwa na uratibu usiofahamika jambo ambayo wakati mwingine hata mtekelezaji anashindwa afanye lipi na aache lipi alisema Gwajima, na kuongeza kuwa, hili ndilo nililo ligundua ndani ya siku zangu 30 za kuwepo katika ofisini yangu mpya”.

Timu za Afya za Mkoa zimetakiwa kutambua kwamba, majukumu yao ndio maduka yao wanaotakiwa kuyafanyia kazi usiku na mchana huku wakionesha matokeo chanya ya kile wanancho kifanya kwa kutoa taarifa kwenye ngazi husika.

Gwajima amesisitiza kwamba katika dira aliyonayo kwenye kutekeleza majukumu yake mapya ni pamoja na kuzingatia, uratibu (Cordination), matokeo chanya (Result/Productivity), huduma bora (Good Services) kwa mteja pamoja na kuwajali wateja (Customer care), hivyo akawataka wajumbe wa timu zote za afya za mikoa Tanzania Bara, kulijua hilo na kulizingatia.

“Inatia hofu sana, unakuta mtu ni mratibu wa kitengo fulani katika ngazi ya Mkoa, lakini hata siku moja hajafanya ziara wilayani kwenda kujionea changamoto zilizopo na kushauri nini chakufanya, mimi niwaambie wakati nikiwa Mganga Mkuu wa Wilaya kuna mambo tulikuwa tunaibua katika ngazi ya wilaya na badae yanakuwa na maamuzi kwenye ngazi ya taifa” alisema Gwajima.

Gwajima akawataka wajumbe wote wa timu za mikoa kufanya kazi kiteknolojia ili kuongeza tija ya utendaji kazi wao lakini pia matumizi ya teknolojia iwe ni chachu ya wao kufanya kazi na kuonesha matokeo (Productivity).

“Serikali imeajiri watumishi Elfu sita (6,000) wa afya, je mmesha jiuliza katika kufanikisha utendaji wenye tija mmewatumiaje hususan katika matumizi ya teknolojia?” alihoji Gwajima, na kusema, lazima tuhakikishe wanajua namna yakuwafikia wananchi hata kwa njia ya mtandao na kutoa ushauri ili kupunguza misongamano katika vituo vyetu vya kutolea huduma, kwani sio kila mgonjwa aende hospitali wengine wanahitaji ushauri tu.” Alisisitiza Gwajima.  

Awali akiwa katika  kikao na Wajumbe wa Sekretarieti ya Mkoa, Katibu Tawala wa Mkoa huo Maduka Kessy, alimuelezea Naibu Katibu Mkuu kwamba, ushirikishwaji wa maamuzi yaliyo mengi yamekuwa yakifanywa na Wizara moja kwa moja na kukosa uratibu wa Mkoa hali ilizua mkanganyiko wa maamuzi, sambamba na  kuwakilisha kilio chake cha uhaba wa Magari ya viongozi katika mkoa huo wakiwapo waheshimiwa Wakuu wa Wilaya.

Dkt. Dorothy Gwajima aliteuliwa kushika wadhfa huo wa Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia Afya OR-TAMISEMI, akichukua nafasi iliyo achwa wazi na Dkt. Zainab Chaula aliyeteuliwa kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Afya nah ii ni ziara yake ya kwanza kufanya katika Sekretarieti ya Mkoa.

Anaandika: Atley Kuni


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert May 12, 2025
  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert May 12, 2025
  • Fursa kwa Wahitimu wa Kidato cha Nne 2024 kubadili Tahasusi na Kozi April 02, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI AJIRA ZA AFYA - TAMISEMI 2025 March 15, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • NENDENI MKAITANGAZE SERIKALI.

    May 24, 2025
  • SOKO LA KISASA LA NYAMA CHOMA LAZINDULIWA VINGUNGUTI

    May 24, 2025
  • DKT. Biteko asisitiza wazazi kuthamini nafasi ya familia katika malezi na makuzi ya mtoto.

    May 24, 2025
  • Mhe. Rais Samia amtaka Prof. Nagu kuboresha  huduma ya afya ya msingi.

    May 24, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.