Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

TAMISEMI QUEENS YAPANIA KUFANYA MAKUBWA LIGI DARAJA LA KWANZA NETIBOLI TANZANIA BARA

Imewekwa tar.: September 3rd, 2019

Na Mathew Kwembe, Dodoma

Timu ya netiboli ya Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa ‘TAMISEMI QUEENS’ imejigamba kufanya vizuri katika michuano inayoendelea ya netiboli ligi daraja la kwanza inayoendelea katika uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma.

Tayari timu hiyo imeshinda michezo minne kati ya sita iliyokwishacheza na  hivi sasa inashika nafasi ya pili mbele ya vinara timu ya Mbweni JKT kutoka jijini Dar es salaam.

TAMISEMI QUEENS imekwishazifunga timu za Cocacola,Jiji la Dodoma, Jiji la Tanga na SMART na imepoteza michezo miwili hadi sasa ambayo ni ya Mbweni JKT na Jiji la Arusha.

Akizungumzia michuano hiyo kocha wa timu hiyo Maimuna Kitete amesema kuwa timu yake ina nafasi nzuri ya kushiriki ligi ya muungano kutokana na maandalizi mazuri ambayo timu yake imeyafanya.

Amesema kufikia sasa timu yake imeonyesha upinzani mzuri dhidi ya timu tishio kama Mbweni JKT na ameahidi kuzichapa timu zote tatu zilizosalia katika michuano hiyo.

Kwa upande wake Meneja wa timu hiyo Doto Bintaraba amesema kuwa timu ya ‘TAMISEMI QUEENS’ ina uhakika wa kushika nafasi tatu za juu kutokana na kuwaandaa vijana wake kufanya makubwa katika michuano ya ligi daraja la kwanza inayoendelea jijini Dodoma.

Amesema ari kubwa waliyo nayo wachezaji wake imempa imani ya kuendelea kufanya vizuri katika mechi tatu zilizosalia.

Naye mchezaji Lilian Jovin ambaye ndiye mfungaji tegemeo wa ‘TAMISEMI QUEENS’ amesema kuwa timu yake inaendelea kuimarika siku hadi siku na akaahidi kufanya vizuri katika michuano iliyobaki ya ligi daraja la kwanza.

Amesema kuwa kufikia sasa timu yake haiwaogopi timu yoyote na akawatahadharisha timu pinzani watakazokutana nazo wajipange kupata kipigo kitakatifu.

Kauli ya Lilian iliungwa mkono na mchezaji mkongwe wa timu hiyo Flora Odilo ambaye aliahidi ushindi mnono kwenye michezo mitatu iliyosalia katika michuano ya ligi hiyo.

‘TAMISEMI QUEENS’ imebakiza mechi dhidi ya Eagle, JKT Makutupora na JKT Mbweni.

Hadi sasa wanaoongoza ligi hiyo ni timu ya JKT Mbweni yenye pointi 10, ikifuatiwa na ‘TAMISEMI QUEENS’ikiwa na pointi 8, huku nafasi ya tatu ikichukuliwa na timu ya JKT Makutupora iliyo na pointi 8 pia huku nafasi ya nne na ya tano zikichukuliwa na timu za Jeshi Stars na Jiji la Arusha.

Mbali na michuano hiyo kutoa bingwa wa mchezo wa netiboli Tanzania Bara, timu sita za juu zitafanikiwa moja kwa moja kushiriki ligi ya netiboli ya muungano iliyopangwa kufanyika mjini Zanzibar baadaye mwaka huu.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert May 12, 2025
  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert May 12, 2025
  • Fursa kwa Wahitimu wa Kidato cha Nne 2024 kubadili Tahasusi na Kozi April 02, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI AJIRA ZA AFYA - TAMISEMI 2025 March 15, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI

    May 23, 2025
  • PJT-MMMAM Yawezesha Uanzishwaji wa Vituo 206 vya Malezi ya Watoto Wadogo

    May 21, 2025
  • SERIKALI KUJENGA DARAJA LINALOUNGANISHA KIJIJI CHA NEGERO – KILINDI

    May 21, 2025
  • MHE. MCHENGERWA ABORESHA TAARIFA ZAKE KWENYE  DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

    May 20, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.