• Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Machapisho
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
    • Green and Smart Cities
    • Miongozo ya Kilimo
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Michoro ya Ujenzi
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)

TAMISEMI, PS3 na TSC Kuboresha OPRAS ya Walimu kwa Matokeo

Imewekwa tar.: October 9th, 2018

Mkurugenzi wa Serikali za Mitaa Ofisi ya Rais TAMISEMI Dkt. Charles Mhina, amefungua mafunzo ya kuongeza ufanisi wa utekelezaji wa OPRAS kwa ajili ya walimu wanaofundisha darasani kwa wawezeshaji wa Kitaifa Jijini Dodoma na kuwataka washiriki kuleta matokeo chanya katika sekta ya Umma nchini.

Akifungua mafunzo hayo katika ukumbi wa African Dreams Hotel Jijini Dodoma, Dkt. Mhina amewataka washiriki kutumia nafasi hiyo adimu ya mafunzo ili kuleta mabadiliko ya mfumo mzima wa upimaji wa utendaji katika sekta ya umma ujulikanao kama OPRAS. Dkt Mhina alibainisha kuwa katika sekta ya Umma, sekta ya Elimu ndiyo inachukua asilimia kubwa ya watumishi wa Serikali hapa nchini na hii imepelekea kuanza maboresho katika sekta ya elimu.

“tumiemi nafasi hii mkalete mabadiliko katika upimaji wa utendaji kwani hakuna kundi la Utumishi wa Umma lisilotekeleza mfumo wa OPRAS, watumishi wote lazima wajaze, hivyo kundi hili la wawezeshaji wa kitaifa ndilo linalotegemewa katika kufundisha wengine katika sekta ya Elimu”.

Dkt. Mhina amesema watumishi wote wa Umma wanapaswa kufanya kazi kwa bidii ili kuleta matokeo, na hii ndiyo sababu ya kumpima mfanyakazi. “Kila mtumishi anapaswa afanye kazi kwa bidii na kuleta matokeo, sisi kama wataalam tunapaswa kutambua na kujua eneo hili muhimu la OPRAS na ndio maana kuna maboresho katika eneo hili”

Dkt Mhina alibainisha kuwa Mfumo huu umeanza kutekelezwa Mwaka 2004 na alitaja changamoto za utekelezaji wa mfumo wa OPRAS ambazo zinaweza kutatuliwa kwa watekelezaji kupata uelewa juu ya mfumo. Dkt Mhina ameshukuru Shirika la Misaada la Marekani (USAID) kupitia Mradi wa Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta ya Umma ‘PS3’ kwa kugharamia mafunzo ya timu ya wawezeshaji wa kitaifa wa sekta ya elimu.

Kwa upande mwingine, Dkt. Josephine Kimaro ambaye ni Msimamizi wa Kitengo cha Mifumo ya Rasilimali Watu (HR Team Lead) kutoka PS3 amesema lengo la mafunzo hayo ni kuboresha utekelezaji wa mfumo wa OPRAS kwa Walimu wanaofundisha darasani. Dkt Kimaro alibainisha kwamba mnamo Februari 2017, OR-TAMISEMI, OR-Utumishi, Tume ya Utumishi wa Umma na Mradi wa PS3 walishirikiana katika utafiti wa kubaini changamoto za utekelezaji wa mfumo wa OPRAS katika Mamlaka za Serikali za Mitaa. Utafiti huu uligundua changamoto ya ujazaji wa malengo ya OPRAS na kupelekea makubaliano ya kuanza kutatua changamoto hii kwa kurahisisha ujazaji wa malengo ya OPRAS kwa Walimu wa darasani.

Aidha, Dkt. Kimaro ameishukuru Serikali kwa kuwa mshirika mkubwa katika uimarishaji wa mifumo mbalimbali, ikiwemo ya Rasilimali Watu katika Utumishi wa Umma. PS3 imefanya kazi na Mamlaka za Serikali Mitaa katika kuboresha upangaji wa Rasilimali Watu kwa kuzingatia uzito wa kazi na vipaumbele vya halmashauri, pia katika kutengeneza mipango ya motisha kwa watumishi ambapo kuna Halmashauri zinatenga bajeti kwa ajili ya motisha, na nyingine zimeanza utekelezaji wa mipango hiyo. Aidha, Mradi umetekeleza uboreshaji wa masjala za Halmashauri 30 hapa nchini kwa kushirikiana na wadau mbalimbali katika sekta ya umma.

Naye Bi. Neema Lemunge ambaye ni Mwakilishi wa Katibu Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC) amewashukuru Programu ya PS3 kwa kuendelea kufadhili baadhi ya miradi na mifumo ambayo inaleta manufaa nchini hususani katika Mamlaka za Serikali za Mitaa.  

Mafunzo hayo ya siku nne yanafadhiliwa na Mradi wa Uimarishaji Mifumo ya Sekta ya Umma ‘PS3’ kwa ushirikiano wa pamoja na Ofisi ya Rais-TAMISEMI na Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC).



                    Anaandika Fred Kibano

Matangazo

  • Orodha ya waliopata vibali vya Uhamisho Septemba - Disemba 2022 (OR - TAMISEMI) January 21, 2023
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kidato cha Kwanza Waliorudia Mtihani January 15, 2023
  • Matumizi ya Lugha ya Kiswahili na Kingereza January 14, 2023
  • Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Kwanza 2023 December 14, 2022
  • Orodha ya Waliopangwa kwenye Vituo vya Kazi Kada za Afya (Awamu ya Pili) Agosti 2022 August 30, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA KWA KADA ZA AFYA (Marudio) July 20, 2022
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • LAAC YAPOKEA TAARIFA KUHUSU UTAWALA NA UENDESHAJI WA MAMLAKA ZA SERIKALI ZA MITAA

    March 14, 2023
  • SERIKALI YAWEKA MIKAKATI KATIKA USIMAMIZI WA MIRADI YA MENDELEO, UKUSANYAJI NA UDHIBITI WA MAPATO KATIKA HALMASHAURI

    March 13, 2023
  • WAUGUZI NA WAKUNGA WATAKIWA KUSIMAMIA MAADILI YA KAZI

    March 13, 2023
  • ACHENI KUTUMIANA NYARAKA ZA SERIKALI KWENYE MITANDAO YA KIJAMII NA BARUA PEPE BINAFSI - DKT. MPANGO

    March 13, 2023
  • Angalia zote

Video

Taarifa ya Ukusanyaji wa Mapato ya Halmashauri, kipindi cha robo ya pili ya mwaka wa fedha 2021/22
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.