Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

TAMISEMI HAIVUNJI SHERIA KUANDAA KANUNI ZA UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA

Imewekwa tar.: June 18th, 2024



WADAU wa uchaguzi wamesisitiza kuwa hatua ya Ofisi ya Rais-TAMISEMI kuandaa kanuni za uchaguzi wa serikali za mitaa haivunji sheria yoyote.


Akichangia utoaji maoni wa kanuni za uchaguzi wa serikali za mitaa, Mkurugenzi Mtendaji wa shirika lisilo la kiserikali la Women in Social Entrepreneurship (WISE), Astronaut Bagile amesema wananchi wanapaswa kuelewa kuwa hakuna sheria yoyote imevunjwa katika mchakato wa uchaguzi wa serikali za mitaa.


“Niwatoe hofu watanzania kuwa huu uchaguzi si kwamba unavunja sheria iliyopitishwa na bunge, leo tunazungumzia uchaguzi wa serikali za mitaa na hakuna mahali ilipokesewa na sana sana unaakisi adhima ya Serikali ya kuhakikisha kwamba demokrasia inarudi kwa wananchi kwasababu Serikali za mitaa ndipo wananchi wanapoishi na wanategemea huduma mbalimbali ziletwe kwao kupitia serikali yao.”


Dk.Bagile alisema ukatili wa kijinsi umekuwa kikwazo kwa wanawake kushiriki kwenye chaguzi za serikali za mitaa na kusisitiza kuwa kanuni hizo zinaenda kuwakaba wale wote wanajiingiza katika kutoa kejeli matusi na vitisho kwa wanawake ambao wanajitokeza kuwania nafasi za uongozi.


Akifungua kikoa hicho cha kupokea maoni ya rasimu ya kanuni za uchaguzi wa serikali za mitaa leo jijini Dodoma, Naibu Waziri wa Tamisemi, Dk Festo Dugange amesema sheria ya Serikali za Mitaa inampa dhamana Waziri mwenye mamlaka za Serikali za mitaa kuandaa kanuni za uchaguzi wa Serikali za Mitaa na kusimamia uchaguzi huo.

 

“Na kanuni hizo zitawasilishwa kwenu kwa ajili ya kupata maoni. Nimeona nianze kwa kutoa ufafanuzi huu ambao mara nyingi maeneo mbalimbali tumekuwa tukipata hoja za wadau kuwa ni namna gani mamlaka hii inahusika na uchaguzi wa Serikali za Mitaa.”


Dk. Dugange amesema maelekezo ya Rais Samia Suluhu Hassan ametaka uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa Mwaka 2024, kuwa huru na haki na kwamba rasimu hiyo imezingatia maoni ya wadau.


Naye Shehe Mkuu wa Jumuiya ya Shiha (TIC) Tanzania, Hemed Jalala alipongeza hatua ya Serikali ya kuwashirikisha viongozi wa dini na watu tofauti tofauti katika kutoa maoni na kusema hatua hiyo inawapa nguvu viongozi wa dini.


“Nipongeze serikali kwa kutukusanya kutoa maoni viongozi wadini ambao ni wadau muhimu katika kuhubiri amani, upendo na wa kutawaka watanzania wavumiliane na wakae vizuri,”


Alisema hatua ya Ofisi ya Rais-TAMISEMI kuwakutanisha viongozi wa dini na kutoka maeneo tofauti tofauti ni ishara ya nia njema ya Rais Samia na wizara ya kutenda haki na kuimarisha demokrasia ndani ya Tanzania.


Alisema kitendo hicho pia kinaonesha ujasiri wa Rais Samia na kuwapa nguvu viongozi wa dini wanapokutana na waamini wao siku za jumapili na ijumaa kuendelea kuhubiri umuhimu wa kukaa kwa amani, mshikamano, kuvumiliana.


Naye Askofu Mkuu wa Kanisa la Elim Pentekoste Tanzania, Peter Konki aliishauri serikali kuongeza wigo wa kupokea maoni kuhusu maboresho ya rasimu ya kanuni hizo.


“Unapowapa watu uhuru wa kuweka mawazo yao katika kuweka Serikali madarakani kunajenga imani kwa wananchi na kuwa karibu na serikali na haki ya kuitetea serikali na kuwa sehemu ya serikali.”


Kwa upande wa Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Tanzania Padri Charles Kitima alishauri kuwepo uwazi wakati wa wagombea wanaporejesha fomu ili kuondoa manunguniko pale mtu anapoenguliwa kushiriki uchaguzi.


Naye. Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Kivulini la jijini Mwanza, Yassin Ally alishauri kanuni hizo kutoa uwiano sawa kwa wanawake kuongombea nafasi za uongozi katika mamalaka za serikali za mitaa.


Akitoa maoni, Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki Tanzania (TEC), Padri Charles Kitima alitaka kuwepo kwa uwazi wakati wa uteuzi wa wagombea kwenye uchaguzi huo. 


“

Matangazo

  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert (extension) 1 May 28, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert (extension) May 28, 2025
  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • RC CHALAMILA ATAKA MACHINGA KARIAKOO KUFUNGUA NJIA

    May 30, 2025
  • Wamiliki wa vituo vya kulelea watoto wadogo mchana watakiwa kuzingatia miongozo na kanuni zilizopo.

    May 29, 2025
  • Mhe. Katimba awapokea Wabunge wa Zambia waliokuja kujifunza kuhusu Usimamizi na Uendeshaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa Tanzania Bara

    May 28, 2025
  • Mtwale Atoa Mwongozo kwa Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.