Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Shule 8 za Serikali zaingia kumi bora matokeo ya Kidato cha Sita

Imewekwa tar.: August 21st, 2020

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe.  Selemani Jafo amesema uwekezaji mkubwa uliofanywa katika sekta ya elimu na serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dk John Magufuli ndio siri iliyopelekea shule nane za serikali kuingia kwenye kumi bora katika matokeo ya kidato cha sita 2020.

Ameyasema hayo leo ofisini kwake Jijini Dodoma wakati akiongea na waandishi wa habari kuhusu ufaulu wa Shule za sekondari zinazomilikiwa na Serikali katika matokeo ya kidato ya sita.

Amesema katika kipindi cha miaka mitano Serikali imeendelea kufanya vizuri katika Sekta ya Elimu ambapo kwenye matokeo yaliyotangazwa leo tarehe 21/08/2020  ufaulu umeongezeka kwa wanafunzi wa kidato cha sita kutoka  asilimia 98 kwa mwaka 2019 hadi kufikia asilimia 99.51 kwa mwaka.

Amesema kuwa katika matokeo hayo shule za Serikali nane zimeweza kuingia katika  shule kumi bora kwa mara ya kwanza zikiwemo shule za kata 3 ambazo ni Kasimiri, Mwandeti na Dareda.

Amezitaja shule za Serikali zilizoshika nafasi kumi bora kuwa ni Mzumbe, Shule ya wasichana Tabora, shule ya wavulana Tabora, Iiliboru na  Kibaha

“Zamani ufaulu wa shule za Serikali ulikuwa mdogo  kiasi kwamba wazazi walikuwa hawapendi kuwapeleka watoto wao kusoma katika shule hizo wanapochaguliwa kujiunga na shule hizo, lakini sasa shule hizo zimekuwa na ufaulu mkubwa na kuwa tegemeo  kwa wazazi kuwapeleka watoto wao” amesema Waziri Jafo

Waziri Jafo anafafanua kuwa  uwekezaji uliofanywa na Serikali ya awamu ya Tano chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli umeleta mabadiliko makubwa katika eneo la taaluma nchini

Aidha. Jafo amewashukuru waalimu, maafisa elimu Mikoa na Wilaya kwa usimamizi uliotukuka wa kuhakikisha  vijana wa kidato cha sita wanafaulu  vizuri na kuliongezea taifa sifa katika suala zima la sekta ya Elimu.

Amewapongeza Wanafunzi wote wa kidato cha Sita kwa kusoma kwa bidi na kupata ufaulu mzuri japokuwa kulikuwa na  changamoto ya ugonjwa wa CORONA nchi ya Tanzania bado waliweka juhudu katika masomo na kufaulu mitihani yao vizuri.

Waziri Jafo anaendelea kusema kuwa Serikali imetumia kiasi cha shilingi trilioni 1.09 katika suala zima la utoaji wa elimu bila malipo ambayo imehamasisha  sekta ya Elimu nchini,pia kiasi cha shilingi milioni 588 kwa ajili ya  ujenzi wa miundombinu  jambo hili limesaidia kuongeza idadi ya ufaulu wa wanafunzi.

Sambamba na hilo amesema kuwa Serikali imeweza kuongeza idadi ya waalimu  kwa lengo la kuongeza rasilimali ambao  watasaidia kupeleka elimu juu zaidi hali ambayo inapelekea kuongeza ufaulu zaidi nchini.

"Matokeo hayo yameonyesha pia wanafunzi waliopata daraja la kwanza hadi la tatu ni asilimia 97.74, haya ni mafanikio makubwa,malengo yetu yalikuwa kuingiza shule sita za serikali kwenye kumi bora lakini tumeingiza shule nane,huu ni ufaulu uliozidi viwango" amesema Waziri Jafo.

Na. Angela Msimbira OR-TAMISEMI

Matangazo

  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert (extension) 1 May 28, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert (extension) May 28, 2025
  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • MHE MCHENGERWA AWATAKA MA RC, DC KUONGOZA JOGGING KWENYE MAENEO YAO

    June 14, 2025
  • MANYARA NA MWANZA MABINGWA RIADHA MITA 800 

    June 14, 2025
  • HAKIKISHENI MNAKUWA WABUNIFU  KATIKA KUANDAA MIRADI YA MAENDELEO- ADOLF NDUNGURU 

    June 13, 2025
  • WAVU KWAENDELEA KUNOGA UMITASHUMTA

    June 13, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.