Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

SHUGHULIKIENI MIGOGORO YA ARDHI’ MCHENGERWA

Imewekwa tar.: March 17th, 2024

Na. Fred Kibano, Dodoma

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Mohamed Mchengerwa amewataka Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa Mikoa nchini kusimamia na kutatua migogoro ya ardhi katika maeneo yao. 

Mhe. Mchengerwa ameyasema hayo katika ukumbi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Njedengwa Jijini Dodoma tarehe 16 Machi, 2024 wakati akihitimisha kikao kazi cha kujadili Sura ya Mipango na Bajeti ya Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Tume ya Utumishi wa Walimu, Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa Mwaka wa fedha 2024/25.

 Suala la migogoro ya ardhi limekuwa kero kubwa kwa wananchi na njia pekee ni Viongozi hao wa mikoa kuisimamia na kutatua wakishirikiana na wataalam wao.

“kuendelea kuwepo kwa migogoro ya ardhi katika maeneo yenu inadidimiza shughuli za maendeleo kutokana na muda na rasilimali nyingi kutumika kushughulikia migogoro hiyo, tumieni busara na wataalamu mlionao katika Ofisi zenu katika kusuluhisha migogoro iliyopo kwa kuzingatia Sheria za Nchi, Kanuni na Taratibu” alisema Mhe. Mchengerwa.

Aidha, amewataka Wakuu wa Mikoa kuwafuatilia baadhi ya viongozi wa Mkoa na Wilaya ambao hawafuati sheria katika kuzuia utekelezaji wa tuzo za mabaraza ya ardhi na nyumba ya Kata na Wilaya katika kutolewa kwa tuzo ya ushindi, suala ambalo limekuwa likilalamikiwa na wananchi na mahakama yenyewe ambapo amewashauri kuwatumia vyema wanasheria wao ili kuepusha malalamiko na migongano na mhimili wa mahakama. 

Katika hatua nyingine Mheshimiwa Mchengerwa amemwagiza Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI Adolf Ndunguru kuwasiliana na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora ili kuhakikisha Wakuu wa Mikoa wanapewa mamlaka ya kushughulikia kero za ardhi kwenye mikoa yao kwani pia ni msingi wa Madaraka Mikoani (Decentralization by Devolution) badala ya Maafisa Ardhi kuwa chini ya Wizara ya Ardhi jambo linalosababisha viongozi hao kushindwa kutatua migogoro mingi ya ardhi.

Kwa upande wake Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Adolf Ndunguru akitoa maelezo ya awali amewashukuru Waheshimiwa Wakuu wa Mikoa kwa kazi nzuri wanazozifanya katika mikoa yao lakini pia amesema lengo la kikao kazi hicho ni kujadili utekelezaji wa mipango na bajeti kwa mwaka uliopita 2022/2023 na pia kupata mwelekeo wa utekelezaji wa mwaka ujao 2024/2025, lengo pia likiwa ni kujenga uelewa wa pamoja kwa maana ya ufahamu wa vipaumbele vya Taifa na mikoa katika mwaka 2024/2025.  

Awali akiwasilisha makisio ya bajeti ya Ofisi ya Rais TAMISEMI kwa niaba ya Waziri wa Nchi Mhe. Mchengerwa, Bw. John Cheyo Mkurugenzi wa Sera na Mipango Ofisi ya Rais TAMISEMI amesema jumla ya Shilingi Bilioni 247 ni makisio ya Bajeti yote ambapo Bilioni 220 ni kwa ajili ya Mikoa yote ya Tanzania Bara.

Itakumbukwa kuwa mapema wiki hii, Mheshiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alitoa hotuba kwa viongozi wateule kuhusu masuala mbalimbali likiwemo rushwa, ubadhirifu wa fedha na ukusanyaji wa mapato na Mhe. Mchengerwa amewataka Wakuu wa Mikoa kwenda kuitekeleza hotuba hiyo na kusema ndio msingi wa nini wakatekeleze kwa nafasi yao.

Kikao kazi hicho kimehudhuriwa na Wakuu wa Mikoa, Makatibu Tawala wa Mikoa, Wakuu wa Taasisi zilizopo chini ya Ofisi ya Rais TAMISEMI, Wakurugenzi wa Ofisi ya Rais TAMISEMI, baadhi ya Wizara za kisekta na baadhi ya Maafisa wa Ofisi ya Rais TAMISEMI.


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert May 12, 2025
  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert May 12, 2025
  • Fursa kwa Wahitimu wa Kidato cha Nne 2024 kubadili Tahasusi na Kozi April 02, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI AJIRA ZA AFYA - TAMISEMI 2025 March 15, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI

    May 23, 2025
  • PJT-MMMAM Yawezesha Uanzishwaji wa Vituo 206 vya Malezi ya Watoto Wadogo

    May 21, 2025
  • SERIKALI KUJENGA DARAJA LINALOUNGANISHA KIJIJI CHA NEGERO – KILINDI

    May 21, 2025
  • MHE. MCHENGERWA ABORESHA TAARIFA ZAKE KWENYE  DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

    May 20, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.