Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Shirika la Elimu Kibaha watakiwa Kujiimarisha Kiuchumi

Imewekwa tar.: May 28th, 2020

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Selemani Jafo ameiagiza Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Elimu Kibaha kutumia rasilimali za shirika kujiimarisha kiuchumi.

Jafo alitoa agizo hilo jana jijini hapa wakati wa kuzindua bodi mpya ya Shirika hilo inayoongozwa na Profesa Raphael Chibunda.

Alisema Shirika limekuwa na rasilimali nyingi ikiwamo ukubwa wa ardhi ambao kama bodi itafanya ubunifu itaweza kuitumia kufanya uwekezaji wenye tija utakaosaidia shirika kujiimarisha kiuchumi na kujitegemea.

Hata hivyo katika kutekeleza hilo, Jafo alionya uongozi wa shirika na bodi ya shirika hilo kuwa makini na uwekezaji ambao wataamua kuufanya na kusisitiza kuwa ni lazima kuwe na uwekezaji wenye tija ambao utakuwa na manufaa.

“Shirika la Elimu Kibaha lina ardhi kubwa sana, ambayo kama mtakuwa wabunifu mtakuja na uwekezaji ambao utasaidia sana kuimarisha uchumi wa shirika, mnaweza kuja na maduka ya kisasa pale.

“ Lakini nitoe angalizo, ni lazima uwekezaji mtakaoamua kuufanya muwe makini kwa kuwa na uwekezaji wenye tija, maana kunawatu wajanja wanaweza kuja na maandiko yao feki na kufanya uwekezaji ambao hauna tija.”

Aidha, Jafo alisema ni vyema Bodi hiyo ikaandeleza na kuchagiza maono ya Baba wa Taifa, Julius Nyerere ambaye aliamua kuanzisha Shirika hilo ili kupambana na maadui watatu ambao ni ujinga, maradhi na umasikini.

Jafo pia aliitaka Bodi kuhakikisha inaimarisha taasisi za shirika hizo kama hospitali ya Tumbi, chuo na shule zilizo chini ya Shirika ili ziendelee kufanya vizuri na kuwanufaisha wananchi wanaozunguka shirika na watanzania kwa ujumla.

Jafo pia alilipongeza Shirika hilo kwa Hospitali ya Tumbo kuja na ubunifu wa kutengeneza maji tiba(drip) ambao umesaidia kuipunguzia serikali gharama za kuagiza maji hayo sambamba na shule ya sekondari kibaha na Chuo cha Ufundi (TDF) kufanya vizuri.

MKuu wa wilaya ya Kibaha, Assumpter Mshama ambaye pia ni makamu mwenyekiti wa Bodi alisema changamoto inayofanya Shirika hilo kutosonga mbele ni ufinyu wa bajeti.

Mshana ambaye pia alikuwa ni mjumbe wa bodi iliyopita aliomba serikali kuhakikisha inatoa majibu ya kuruhusu au kukataa maandiko mradi ambayo Shirika inaomba kutekeleza kwa haraka ili kuweza kusonga mbele.

“Tumekuwa tunakwama sana kutokana na kuchelewa kwa serikali kutoa kauli ya ndio au hapana katika maandiko mradi ambayo Shirika tumekuwa tukiomba kutekeleza.

“ Unapeleka andiko, mwaka mmoja, miwili hupati jibu lakini tukipata majibu mapema ya kama ndio tuendelee au hapana inakasoro badilisheni hili na lile, au mradi huu haufai kabisa ili kuja na mawazo mengine, hivyo tunawaomba wataalamu wa TAMISEMI kufanyia kazi maandiko tunayowaletea.”

Naye Mwenyekiti wa Bodi, Profesa Chibunda alisema Bodi yake inakwenda kutekeleza maagizo aliyoyatoa na kulifanya shirika liimarike zaidi.

Pia alioamba ushiriki wa karibu wa Shirika katika hospitali ya Tumbi na Shule zake ambavyo kwa sasa viko chini ya Serikali.

“Tunaona kuna haja ya kubadilishwa kwa mfumo wa uendeshaji, tunataka  ya shirika kwenye shule, hopitali ya Tumbi ili Shirika liweze kuwekeza.”

Shirika la Elimu Kibaha ni Shirika la umma linalotoa huduma mbalimbali, lililopo Mkoa wa Pwani, lilianzishwa mwaka 1963 kama mradi wa pamoja chini ya wafadhili watano- Serikali ya Tanganyika kwa kipindi hicho kwa upande mmoja pamoja na nchi nne za Kinordic (Dernmark, Norway, Finland na Sweden) kwa upande mwengine.

Kwa kipindi hicho mradi huu ulijulikana kama “Tanganyika Nordic Project” mpaka mwaka 1970 ambapo mradi huu ulikabidhiwa rasmi kwa Serikali ya Tanzania na kuitwa Shirika la Elimu Kibaha. Na kusajiwa chini ya sheria ya Mashirika ya Umma Na.17 ya mwaka 1969, marejeo ya mwaka 2002.


 

Na. Nteghenjwa Hosseah, OR-TAMISEMI

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert May 12, 2025
  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert May 12, 2025
  • Fursa kwa Wahitimu wa Kidato cha Nne 2024 kubadili Tahasusi na Kozi April 02, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI AJIRA ZA AFYA - TAMISEMI 2025 March 15, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • NENDENI MKAITANGAZE SERIKALI.

    May 24, 2025
  • SOKO LA KISASA LA NYAMA CHOMA LAZINDULIWA VINGUNGUTI

    May 24, 2025
  • DKT. Biteko asisitiza wazazi kuthamini nafasi ya familia katika malezi na makuzi ya mtoto.

    May 24, 2025
  • Mhe. Rais Samia amtaka Prof. Nagu kuboresha  huduma ya afya ya msingi.

    May 24, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.