• Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Machapisho
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
    • Green and Smart Cities
    • Miongozo ya Kilimo
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Michoro ya Ujenzi
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)

Shilingi Bilioni Tano Kuboresha Miji 45, wamachinga kunufaika – Mhe. Majaliwa

Imewekwa tar.: November 30th, 2021

Na Fred Kibano, Mbeya

Serikali imesema shilingi Bilioni tano zilizozotengwa zitasidia kupanga mipango ya miji na majiji 45 ikiwemo maeneo ya biashara ambayo yanatumiwa na wamachinga hapa nchini.  

Kauli hiyo imetolewa na Waziri Mkuu wa Tanzania Mheshimiwa Kassim Majaliwa alipokuwa akiongea na wafanyabiashara wadogo (wamachinga) Jijini Mbeya kuwa changamoto zinazowakabili zinatambuliwa na Serikali na hatua stahiki zinachukuliwa.

Mheshimiwa Majaliwa amesema Serikali imeendelea kuweka mazingira rafiki kwa makundi yote wanapofanya kazi zao bila bugudha yoyote kama ahadi ya Serikali ya Awamu ya Sita ilivyoagiza.

Aidha, ameuagiza Wakala wa Barabara za Mijini na Vijini (TARURA) kuhakikisha wanatengeneza barabara zote zinazozunguka eneo la Uwanja wa ndege wa zamani na soko la Salanga ambalo linatumiwa na wamachinga Jijini Mbeya.

Waziri Mkuu Majaliwa ameagiza wamachinga wote ambao walitelekeleza maeneo waliyopangiwa na Mamlaka ya Jiji la Mbeya hapo awali na kurejea tena baada ya kuanza kwa maboresho, wapatiwe nafasi za vibanda ili wafanyebiashara kwa kuwa Serikali inawajali wamachinga wote.

Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI, Dkt. Festo Dugange amesema Serikali kupitia Ofisi ya Rais TAMISEMI ilipokea maagizo ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kufanya upangaji wa wamachinga nchi nzima ili kuondoa kero zao ikiwemo maboresho ya maeneo ya kufanyia biashara.

“naomba niwahakikishie kuwa Serikali ina mpango kwa miji 45 kupatiwa fedha kutoka Benki ya Dunia, Jiji la Mbeya likiwa ni mojawapo kupatiwa fedha za kujenga barabara, stendi za kisasa na eneo hili la wafanyabiashara wadogo wadogo (Wamachinga) lipo kwenye mpango wa kupatiwa fedha za Benki ya Dunia itakayoanza mwakani kwa ajili ya kuboresha eneo hili” alisema Dkt. Dugange.  

Aidha, amesema  Mkurugenzi wa Jiji la Mbeya na Mstahiki Meya wameitwa Ofisi ya Rais TAMISEMI Dar es Salaam kwa ajili ya kwenda kufanya tathmini ya mradi huu mapema iwezekanavyo ambayo itatatua kero ya wafanyabiashara wadogo wadogo.

Akitoa maelezo ya awali kabla ya hotuba ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mheshimiwa Juma Homera amesema  eneo la Uwanja wa ndege wa zamani na Soko la Salanga lilikuwa na changamoto nyingi na hivyo kupelekea wafanyabiashara ndogondogo kulikimbia lakini baada ya kuanza kuboreshwa wafanyabiashara hao wanaohitaji vibanda vya biashara eneo hilo wamerudi tena.

Mheshimiwa Homera amesema Mradi mpya wa kiwanda cha kusindika mboga mboga unaogharimu shilingi Bilioni moja na milioni mia sita unajengwa karibu na eneo hilo lakini utahitaji wafanyabiashara ndogo ngogo wapatao 200 na hivyo kutoa ajira kwao na wananchi wengine.

Mbunge  wa Mbeya Mjini Dkt. Tulia Ackson ametoa ombi la kujengwa kwa barabara zenye kiwango cha lami kuzunguka eneo hilo na kuliinua juu kwa kuweka kifusi kwa kuwa mazingira ya eneo hilo ni chepe chepe kwani yanajaa maji kipindi cha masika.

Masanja Matondo Mwenyekiti wa Wafanyabiashara wadogo (Machinga) mkoa wa Mbeya amesema wanaiomba Serikali kuwafanyia mpango wa kupata mikopo nafuu kutoka kwenye mabenki kwa ajili ya kujenga vibanda vyao vya biashara, kupata mikopo ya asilimia 10 kutoka Mamlaka za Serikali za Mitaa, mikopo maalum kwa ajili ya kuwakopesha wamachinga, pamoja na Serikali kuuagiza Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA) kujenga barabara zenye kiwango cha lami kuzunguka eneo hilo la Uwanja wa ndege wa zamani na soko la Salanga.



Matangazo

  • Orodha ya waliopata vibali vya Uhamisho Septemba - Disemba 2022 (OR - TAMISEMI) January 21, 2023
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kidato cha Kwanza Waliorudia Mtihani January 15, 2023
  • Matumizi ya Lugha ya Kiswahili na Kingereza January 14, 2023
  • Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Kwanza 2023 December 14, 2022
  • Orodha ya Waliopangwa kwenye Vituo vya Kazi Kada za Afya (Awamu ya Pili) Agosti 2022 August 30, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA KWA KADA ZA AFYA (Marudio) July 20, 2022
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • BODI YA MIKOPO YA SERIKALI ZA MITAA KUSUKWA UPYA

    January 23, 2023
  • MAKAMU WA RAIS AWAPONGEZA DODOMA JIJI KWA UWEKEZAJI

    January 20, 2023
  • SERIKALA YASISITIZA KILA MMOJA KUTUNZA MAZINGIRA

    January 20, 2023
  • TANZANIA ITAENDELEA KUSHIRIKANA NA WADAU KATIKA MAPAMBANO DHIDI YA UKIMWI

    January 20, 2023
  • Angalia zote

Video

Taarifa ya Ukusanyaji wa Mapato ya Halmashauri, kipindi cha robo ya pili ya mwaka wa fedha 2021/22
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.