Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Serikali yataka Halmashauri ya Njombe kuongeza kasi ujenzi wa hospitali

Imewekwa tar.: May 3rd, 2019

Na Mathew Kwembe, Njombe

Serikali imeutaka uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe kuongeza kasi katika ujenzi wa majengo yake saba ya Hospitali mpya ya Halmashauri hiyo ambapo, majengo sita kati ya saba yapo katika hatua ya msingi.

Akizungumza na Uongozi wa Timu ya Uendeshaji Huduma za Afya ya Halmashauri ya Wilaya hiyo na Mkoa wa Njombe ambao, kwa pamoja walitembelea eneo la Matembwe lililopo umbali wa kilometa 65 kutoka Mji wa Njombe, Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa anayeshughulikia Afya Dkt. Dorothy Gwajima amesema kuwa, ukiacha jengo la kutoa huduma za vipimo vya mionzi, majengo mengine yote sita bado yapo katika hatua ya msingi na ya umwagaji wa zege na hatua hii ni kinyume na kasi ya matarajio ya Serikali kuwa, majengo yote yawe yamekamilika ifikapo tarehe 30 Juni, 2019.

Kufuatia hali hiyo, Dkt Gwajima amemtaka Meneja wa TARURA anayesimamia ujenzi huo Mhandisi Samson Kalesi kuhakikisha kuwa anamsimamia mkandarasi anayejenga majengo hayo ili aongeze idadi ya mafundi ukilinganisha na waliopo sasa kwa ajili ya kuongeza kasi ya ujenzi wa majengo hayo na kuhakikisha yanakamilika mapema kama ilivyokusudiwa.

Dkt. Gwajima ameiagiza Halmashauri kuhakikisha kila wiki iwe inampatia taarifa za ujenzi wa hospitali hiyo ikiwemo picha zinazoonesha hatua iliyofikiwa kwa kila jengo. Aidha, ameagiza kuwe na daftari la taarifa fupi ya ujenzi uliofanyika kila jengo kila siku na taarifa hiyo itumwe pamoja na picha za majengo hayo. Aidha, ameagiza sambamba na kitabu cha Wageni na Viongozi wanaotembelea mradi huo pia, kuwe na daftari linalorekodi maelekezo na ushauri uliotolewa ili, kuweka kumbukumbu nzuri za ushiriki wao katika kufuatilia utekelezaji wa mradi huo.

Vilevile, Dkt Gwajima ameagiza Halmashauri kuhakikisha Kamati zote za Usimamizi wa Ujenzi huo zinafanya Vikao na kutunza muhtasari zote ili, kila inapohitajika kumbukumbu hizo zipatikane. Aidha, amesisitiza kuwa, katika Vikao hivyo uwakilishi wa wataalamu wa afya uzingatiwe ili, waweze kutoa ushauri wao kwa ajili ya kuwezesha kuepuka kasoro za kujenga bila kuzingatia ubora wa maeneo ya kitaalamu kwa kuwa katika huduma za hospitali kila eneo lina kanuni zake mahususi. Dkt. Gwajima amezitaja Kamati hizo kuwa ni Kamati ya Ujenzi, Manunuzi ya vifaa na Mapokezi ya Vifaa.

Pia, Naibu katibu Mkuu amesisitiza umuhimu wa majengo hayo kujengwa katika ubora unaotakiwa kwa kuzingatia ramani “DMO (Mganga wa Wilaya) hakikisha majengo yote saba yanajengwa katika ubora unaotakiwa, na kuepuka kuanza kufanya marekebisho kutokana na kukosekana kwa ufuatiliaji wa kitaalamu wakati wa ujenzi“ amesema Dkt Gwajima.

Kwa upande wake Mhandisi Kalesi amemhakikishia Naibu Katibu Mkuu kuwa, pamoja na uwepo wa changamoto kadhaa walizopitia wakati wa utekelezaji wa mradi huu, atahakikisha wanazingatia maelekezo yote aliyowapa na kuongeza kasi ya ujenzi. Aidha, Dkt. Gwajima ameupongeza Uongozi wa TARURA kwa kushirikiana katika utekelezaji wa mradi huu na kuziba pengo la upungufu wa Wahandisi licha ya majukumu makubwa waliyonayo. Aidha, Dkt. Gwajima ametambua ushirikiano huu na kusisitiza uendelee katika halmashauri zote wanazotekeleza miradi kama hii.

Mapema akisoma taarifa ya ujenzi wa Hospitali hiyo, Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe Dkt Deusdedit Kalaso amemweleza Naibu Katibu Mkuu kuwa halmashauri hiyo imepokea fedha kiasi cha shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya ujenzi ambapo majengo yaliyopendekezwa kujengwa kwa fedha hizo ni pamoja na jengo la utawala, wagonjwa wa nje, stoo ya dawa, maabara, vipimo vya mionzi, jengo la kufulia nguo na jengo la huduma ya uzazi. Dkt Kalaso ameongeza kuwa, kufikia sasa halmashauri imetumia shilingi milioni 418.4 ambayo ni sawa na asilimia 28 ya matumizi ya fedha yote ya mradi na kwamba, hivi sasa taratibu za manunuzi ya vifaa vya ujenzi zinaendelea kwa kutumia fedha iliyobaki.

Wakati huo huo Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ys Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa anayeshughulikia afya Dkt Dorothy Gwajima jana alipata fursa ya kutembelea Kituo cha Afya Lupembe kilichopo katika Wilaya ya Njombe na kujionea hali ya utoaji huduma. Akiwa katika kituo hicho, Dkt. Gwajima amesikitishwa na hali isiyoridhisha ya mazingira ya kituo ikiwemo hali ya usafi na uwajibikaji kwa ujumla ambapo, amezitaka timu za usimamizi na uendeshaji wa huduma za afya mkoa na halmashauri (RHMT na CHMT) kutekeleza jukumu lao la kufuatilia na kusimamia mwenendo wa utoaji huduma huduma katika vituo vya afya na kuleta mabadiliko ya uwajibikaji vinginevyo, wazembe atawaondoa katika majukumu ya uongozi maana inaonekana hawatumii muda wao kufuatilia hali ya huduma katika vituo.

Kufuatia hali hiyo, Naibu Katibu Mkuu ameitaka RHMT na CHMT husika kujitathmini juu ya utendaji wao kwani kituo hicho kipo karibu zaidi na ofisi zao na kungekuwa na fursa kubwa zaidi ya kuwezesha ufuatiliaji lakini sivyo ambavyo imekuwa.

Aidha Dkt Gwajima alipata fursa ya kuongea na baadhi ya wateja waliokuwa kituoni ambao, nao walitoa maoni na kero zao ikiwemo hali duni ya usafi, majibu yasiyo rafiki ya watoa huduma na ukosefu wa baadhi ya dawa. Vilevile, Dkt. Gwajima alifanya mapitio ya takwimu mbalimbali za huduma ambapo baadhi ya aliyobaini kwa ufupi ni pamoja na uzembe katika ufuatiliaji wa wagonjwa hususan siku za mwisho wa wiki na mapumziko ya kazi, ukosefu wa baadhi ya vipimo na ukosefu wa kumbukumbu stahiki za dawa.

Dkt. Gwajima ameagiza maboresho katika kituo hicho yafanyike mara moja na kwamba, mapungufu anayokutana nayo katika vituo ni madogo na ambayo alishayatolea maelekezo na yalitakiwa kubainiwa na timu husika za usimamizi na uendeshaji huduma za afya katika mkoa na halmashauri husika.

Dkt. Gwajima amesema, kwa ujumla timu za usimamizi na uendeshaji huduma za afya mikoa na halmashauri (RHMT na CHMT) zikumbuke kuwa, ubora wa huduma za afya katika vituo ndiyo kioo pekee cha uwajibikaji wao hivyo, wajipange kuhakikisha wanatumia nguvu zaidi na muda zaidi kwa ajili ya ufuatiliaji wa huduma.

Aidha, Dkt. Gwajima amesema, timu itakayobainiwa kushindwa kufuatilia mwenendo wa utoaji huduma katika vituo na kuchukua hatua itambue kuwa, timu hiyo itakuwa imepoteza sifa za kuendelea na majukumu ya uongozi.

Matangazo

  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert (extension) 1 May 28, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert (extension) May 28, 2025
  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • RC CHALAMILA ATAKA MACHINGA KARIAKOO KUFUNGUA NJIA

    May 30, 2025
  • Wamiliki wa vituo vya kulelea watoto wadogo mchana watakiwa kuzingatia miongozo na kanuni zilizopo.

    May 29, 2025
  • Mhe. Katimba awapokea Wabunge wa Zambia waliokuja kujifunza kuhusu Usimamizi na Uendeshaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa Tanzania Bara

    May 28, 2025
  • Mtwale Atoa Mwongozo kwa Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.