Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Serikali yaagiza Kituo cha Afya Majengo kuhudumia wananchi

Imewekwa tar.: June 9th, 2018

Serikali imeagiza kuanza kutolewa kwa huduma za afya katika kituo cha afya majengo wilayani Nanyamba mkoani Mtwara ndani ya miezi mitatu kwa kuwa ujenzi wa majengo yake yote yapo katika hatua za mwisho.

Akitoa maagizo ya Serikali, Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI, Dkt. Zainab Chaula amesema hakuna haja ya kuchelewesha kutoa huduma za afya katika kituo cha afya majengo kwa kuwa wananchi wanahangaika kuitafuta huduma hiyo mbali wakati miundombinu ya kituo hicho ipo katika hatua za mwisho.

“kwa sababu watu wanahitaji huduma, wanafanya mawasiliano sehemu nyingine ili kupata huduma ambayo hapa haipo, lakini ndani ya miezi mitatu lazima huduma zianze kutolewa, Mganga Mkuu wa Wilaya Nanyamba andaa andiko ili mchakato wa kuanzisha kituo uanze mara moja”

Dkt. Chaula ametoa agizo hilo mbele ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya Nanyamba, Mganga Mkuu wa Mkoa Mtwara, wataalam wengine kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na Ofisi ya Rais TAMISEMI wakati akiongea na wananchi katika mkutano ulioandaliwa baada ya kukagua miundombinu ya kituo cha afya majengo.

Aidha, Chaula amesema wakati Serikali inawapangia vituo watumishi wapya 6,180 imewaweka katika mpango wa kuwapangia vituo watumishi wapya katika vituo vipya vinavyokamilika kwa wakati, lakini pia ametoa angalizo kwa wananchi, watumishi na viongozi wote wilayani Nanyamba kuweka mazingira rafiki ili watumishi wapya wasipatwe na hali ya kuyakataa mazingira ya kazi bali watoe motisha kutatua changamoto hiyo.

Hassan Mnengu ni mwananchi wa kijiji cha majengo anasema huenda usumbufu waliokuwa wakiupata utakwisha kwa kufuata huduma za afya mbali na kijiji chao kwa hivi sasa.

“haya majengo yatatutatulia changamoto zilizopo, moja ya usumbufu ni wa kufuata huduma za afya kutoka Nanyamba kwenda wilaya ya Tandahimba au kituo cha afya kilichopo Nanguruwe”

Katika hatua nyingine, Dkt. Zainab Chaula amewaasa wananchi kupanda miti ya matunda zaidi badala ya miti ya kivuli ikiwa ni pamoja na maeneo ya vituo vya afya kwani ni sehemu ya lishe ya jamii.

Kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa, wilaya ya Nanyamba ina zaidi ya wakazi 114,000 na hivyo vituo vitatu vya afya wanavyovijenga wilayani humo, vitakidhi mahitaji ya jamii kwani Sera ya afya inataka watu 50,000 wahudumiwe katika kituo kimoja cha afya.  


Imeandikwa na Fred Kibano

Matangazo

  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert (extension) 1 May 28, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert (extension) May 28, 2025
  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • RC CHALAMILA ATAKA MACHINGA KARIAKOO KUFUNGUA NJIA

    May 30, 2025
  • Wamiliki wa vituo vya kulelea watoto wadogo mchana watakiwa kuzingatia miongozo na kanuni zilizopo.

    May 29, 2025
  • Mhe. Katimba awapokea Wabunge wa Zambia waliokuja kujifunza kuhusu Usimamizi na Uendeshaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa Tanzania Bara

    May 28, 2025
  • Mtwale Atoa Mwongozo kwa Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.