Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Serikali Yaagiza Halmashauri 30 Kuhamia na Kujenga Miundombinu

Imewekwa tar.: February 11th, 2020

Serikali imeagiza Halmashauri 30 zilizotakiwa kuhamia katika makao yao ya kiutawala kujenga ofisi za utawala na kuzikamilisha kwa wakati ili kutoa huduma bora kwa wananchi.

Akitoa agizo hilo Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhandisi Joseph Nyamhanga wakati wa ziara yake wilayani Geita ambapo aliongea na watumishi na kukagua baadhi ya miradi ya maendeleo ameziagiza halmashauri 30 kuwa pamoja na kuitikia wito wa Mheshimiwa Rais Magufuli kuhamisha makao yao ya Halmashauri tangu Novemba 7, 2019 bado kuna changamoto ya mvutano wa kimaamuzi ni wapi makao makuu ya halmashauri yajengwe na hili linachelewesha huduma kwa wananchi.

“hakikisheni taratibu za eneo lililopendekezwa ujenzi wake unaanza mara moja ili muhamie kwa wakati hii ni pamoja na halmashauri nyingine 29 ambazo Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli aliagiza tangu tarehe 7 Novemba, 2019”

Mhandisi Nyamhanga amesema pamoja na halmashauri hizo 30 kutii agizo la Mhe Rais Magufuli, halmashauri nyingi bado zimepanga kwenye majengo binafsi na wengine wapo katika ofisi za kata, shule, vituo vya afya, hospitali na majengo mengine kama magala ya chakula na kwamba hii haikubaliki kwani kuna baadhi ya halmashauri ambazo bado zina malumbano ya wapi majengo hayo ya utawala yajengwa.

Amesema agizo hilo ni la mara moja kwa halmashauri kuanza ujenzi na kukamilisha kwa wakati ili wananchi wafaidi matunda ya kupata huduma bora, karibu na kwa wakati lakini pia kutambua mipaka mipya ya kiutawala kwenye vitongoji, vijiji na wilaya ili kuandika hati za halmashauri.

Mhandisi Nyamhanga amezitaja baadhi ya halmashauri ambazo zimemaliza mchakato wa kutambua maeneo yao ya utawala na kuanza mchakato wa hati za halmashauri ambazo ni muhimu pia kwa ajili ya uchguzi mkuu wa 2020 kuwa ni pamoja na halmashauri za wilaya ya Mbulu (Manyara), Kibaha (Pwani), Handeni (Tanga), Uyui (Tabora) na Tanganyika (Katavi).

Wakati wa ziara hiyo Nyamhanga amekagua kituo cha afya Nzela ambacho kimepatiwa shilingi milioni 500 kwa ajili ya vifaa tiba na ukamilishaji wa majengo mengine ili kukipandisha hadhi kuwa hospitali ya wilaya ya Geita.

Mbunge wa Geita Joseph Musukuma ameomba kurejeshwa kwa shilingi milioni 293 ambazo zilirudishwa hazina kwenye mfuko mkuu wa Serikali baada ya kuvuka mwaka ili kumalizia baadhi ya kazi zilizobaki katika hospitali hiyo teule ya wilaya.

Kwa upande wake Katibu Tawala Mkoa Geita Dennis Bandisa amesema halmashauri ya wilaya ya Geita ina watu wapatao laki 9 lakini kimapato inazidiwa na halmashauri ya Mji Geita lakini pia kuna changamoto ya kiutawala katika Mji mdogo wa Geita ambapo Mtendaji wa kijiji ndiye anayefanya kazi kama Mkurugenzi wa Mji mdogo.

Naye Mkurugenzi Mtendaji  wa Halmashuri ya Wilaya ya Geita Bw. Ally Kidwaha amesema tayari wamepata eneo la ekari 400 kwa kushirikiana na Wadau wengine kujenga ofisi za halmashauri ya wilaya na kupima viwanja ili kuboresha makao ya halmashauri hiyo.

                      Anaandika Fred Kibano


Matangazo

  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert (extension) 1 May 28, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert (extension) May 28, 2025
  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Mhe. Katimba awapokea Wabunge wa Zambia waliokuja kujifunza kuhusu Usimamizi na Uendeshaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa Tanzania Bara

    May 28, 2025
  • Mtwale Atoa Mwongozo kwa Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa

    May 27, 2025
  • Nipo tayari kufanya kazi pamoja nanyi kufikia malengo ya Mhe. Rais – Prof. Tumaini Nagu

    May 26, 2025
  • TARURA IMEKUWA NA MCHANGO MKUBWA KWA SERIKALI YA AWAMU YA SITA

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.