Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Serikali kutumilia Bilioni 208.9 kuwezesha kaya duni laki mbili na elfu 60 kwa miaka sita

Imewekwa tar.: May 15th, 2025

OR – TAMISEMI

Serikali inakusudia kutumia Dola milioni 77.4 sawa na shilingi Bilioni 208.9 kuzijengea uwezo kaya duni laki mbili na elfu 60 za wakulima na wavuvi kwa kuziwezesha kitaalam na kuziunganisha na taasisi za kifedha hususani TADB kwa muda wa miaka sita mfululizo ili ziweze kujiimarisha kiuchumi kupitia uzalishaji wa mazao ya uvuvi na kilimo.

Kaya hizo ambazo ni sawa na watanzania milioni moja na laki tatu waliopo kwenye Mikoa 11 ya Tanzania Bara zinajengewa uwezo kupitia Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) katika mradi unaolenga kuimarisha Mifumo jumuishi ya usalama wa chakula na lishe kwenye Halmashauri 41 zinazounda mMikoa hiyo.

Ili kuwezesha utekelezaji chanya wa programu ya AFDP, Ofisi ya Waziri Mkuu – Sera, Bunge na Uratibu ambayo inaratibu programu hiyo kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais – TAMISEMI ambao ni watekelezaji imewakutanisha Makatibu Tawala wa Mikoa yote 11, pamoja na maafisa viungo kwenye halmashauri husika ili kujenga uelewa wa pamoja katika utekelezaji wa programu hiyo.

Akifungua kikao kazi hicho kinachoendelea mkoani Morogoro, Mkurugenzi wa Tawala za Mikoa Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Bi. Beatrice Kimoleta, amewasisitiza watendaji hao kusimamia kikamilifu pesa zote zitakazotolewa kwa lengo la kuwezesha utekelezaji wa mradi akikemea ubadilishwaji wa matumizi ya pesa za miradi. 

“Hapa naomba nisisitize hizi pesa zisitumike kinyume na taratibu zilizoelekezwa katika utekelezaji wa programu hii, Serikali inahitaji kuona matokeo chanya kama yanavyolengwa na programu, isitokee mkabadilisha hata shilingi ya matumizi ya pesa hizi, kufanya hivyo itakuwa ni kama dhuluma kwa walengwa, na sitarajii mtu yeyote kubadilisha matumizi” alisema Bi. Kimoleta.

Awali akitoa taarifa ya Programu hiyo Bw. Salimu Mwinjaka ambaye ni mratibu wa programu ya AFDP ameitaja mikoa itakayonufaika na programu hiyo kuwa ni Morogoro, Manyara, Singida, Dodoma, Tabora, Mwanza, Lindi, Pwani, Shinyanga, Geita na Tanga.

Aidha amesema tamati ya programu ya AFDP Serikali inatamani kuona ikiwa na meli zake za uvuvi katika bahari ya hindi, wananchi upande wa visiwani Zanzibar kunufaika na uwepo wa zao la mwani, upotevu wa mazao ya samaki kupungua, uwepo wa mbegu bora za mahindi, alizeti na mimea mingine jamii ya kunde pamoja na kuanzishwa kwa viwanda vya kutengeneza chakula cha samaki, hatua itakayowezesha uwepo wa vifaranga vya samaki vyenye ubora.

Matangazo

  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert (extension) 1 May 28, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert (extension) May 28, 2025
  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • WAACHENI WATOTO WAENDE SHULE- RAIS SAMIA

    June 16, 2025
  • NIMESAINI NOTISI ZA KUVUNJA MABARAZA YA MADIWANI - MCHENGERWA

    June 15, 2025
  • MANYARA BINGWA RIADHA WASICHANA NA WAVULANA MITA 1,500

    June 15, 2025
  • MHE MCHENGERWA AWATAKA MA RC, DC KUONGOZA JOGGING KWENYE MAENEO YAO

    June 14, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.