Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Rais Magufuli Awataka Maofisa Tarafa kuzitunza Pikipiki alizowakabidhi

Imewekwa tar.: June 11th, 2020

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, amewataka Maofisa Tarafa Nchini kuzitunza pikipiki 448 alizowakabidhi mapema leo hii kwa lengo la kuwahudumia wananchi.

Kauli hiyo ameitoa  leo hii alipokua kwenye hafla ya uzinduzi wa  jengo la TARURA Makao Makuu sambamba na kukabidhi pikipiki 488 za Maofisa Tarafa.

"Niwatake Maofisa Tarafa wote Nchini, mkazitunze pikipiki hizi,na sio kupakizana Mishikaki au kuzitumia kwa matumizi yasiyofaa, hata kama wewe Ofisa ni mwanamke usiiache hiyo pikipiki tafuta msaidizi wako akuendeshe na uweze kufanya kazi za umma kwa ufanisi". amesisitiza Rais Magufuli.

Aidha Rais Magufuli ameelekeza Ofisi ya Rais, TAMISEMI kuweka utaratibu wa kuaandikisha maofisa tarafa hao kipindi watakapokabidhiwa  pikipiki hizo ili kuweza kuwa na ushahidi pale kutakapo tokea uharibifu wowote katika pikipiki hizo au kuipoteza basi muhusika anatakiwa kuwajibika juu ya uharibifu huo ikiwa ni pamoja na kuilipa endapo itakua ameipoteza.

Katika hatua nyingine Rais Magufuli amewapongeza watendaji wa TARURA kwa kukamilisha ujenzi wa jengo lao na kuwataka kutumia fedha zinazoletwa na Serikali kutekeleza miradi ya barabara za mjini na vijiji kwa ufanisi.

Rais Magufuli amesema Tanzania imepata fedha za msamaha kutoka  Shirika la Fedha Duniani (IMF) kwa kuidhinisha Dola 14.3 milioni za msamaha wa madeni kwa Nchi ya Tanzania kwa kuwa Nchi yetu imeweza kupambana vizuri na ugonjwa wa corona.

“Nitamuandikia barua Mkurugenzi Mkuu wa IMF kwa niaba ya Watanzania kumshukuru,fedha za IMF tutazitumia kuendeleza mapambano dhidi ya ugonjwa wa corona, na maendeleo mengine yatakayosaidia corona isirudi tena katika nchi yetu” ameweka wazi Rais Magufuli.

Aidha Rais  Magufuli ameongeza kuwa  tukitengeneza barabara nzuri watu wakapita haraka, hata mdudu wa corona hawezi kumsogelea yule anayekimbia, Corona bado haijaisha lakini imepungua sana hivyo tuendelee kuchukua tahadhari na Mungu wetu anatupenda na tuendelee kumtegemea yeye.

"Tunamshukuru sana Mungu kwa kutuepusha na ugonjwa wa Corona, mambo yanaenda vizuri na tusidharau dawa za kienyeji uchawi tu ndiyo mbaya, Nimetoa maelekezo kwenye Wizara ya Afya, kile kitengo cha madawa ya asili kiendelezwe kwa nguvu zote na bajeti yake iongezwe " ameeleza Rais Magufuli

Awali  Rais Magufuli aliwataka  wananchi wote waliohudhuria hafla hiyo  kutoa heshima ya kuwaombea aliyekuwa Rais wa Burundi Mhe. Piere Nkurunziza aliyetutoka siku chache zilizopita pamoja na Watu Nane waliofariki Dunia baada ya hiace waliyokua wamepanda kugongwa na Lori huko Mkoani Mwanza.

Naye Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI), Mhe. Selemani Jafo amesema  takribani bilioni 89.1 ni fedha iliyotengwa kwa ajiri ya kukamilisha mtandao wa barabara za lami kilomita 51.2 katika mji wa kiserikali.

“Mhe. Rais, nikuhakikishie kuwa barabara hizo ulizoziwekea jiwe la msingi leo zitapambwa na miti ya matunda pembeni na taa zaidi ya 700 za barabarani ili kuleta hadhi katika Jiji la Dodoma kuwa makoa makuu ya nchi yetu,” amesema Mhe. Jafo.

Awali akisoma taarifa ya ujenzi wa jengo hilo Mkurugenzi Mtendaji wa TARURA Mhandisi Victor Seif amesema jengo hilo lina sakafu(Flow) 3 na  limejengwa kwa kutumia mfumo wa Force Account na umegharimu takribani shilingi Bil 1.9.

Awali kabla ya hafla hiyo Rais Magufuli ameweka jiwe la msingi la ujenzi wa Barabara za lami a mzunguko zenye urefu wa kilomita 51.2 katika mji wa Serikali Mtumba zinazojengwa na kusimiwa na TARURA.

MWISHO


Matangazo

  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert (extension) 1 May 28, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert (extension) May 28, 2025
  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • RC CHALAMILA ATAKA MACHINGA KARIAKOO KUFUNGUA NJIA

    May 30, 2025
  • Wamiliki wa vituo vya kulelea watoto wadogo mchana watakiwa kuzingatia miongozo na kanuni zilizopo.

    May 29, 2025
  • Mhe. Katimba awapokea Wabunge wa Zambia waliokuja kujifunza kuhusu Usimamizi na Uendeshaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa Tanzania Bara

    May 28, 2025
  • Mtwale Atoa Mwongozo kwa Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.