• Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Machapisho
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
    • Green and Smart Cities
    • Miongozo ya Kilimo
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Michoro ya Ujenzi
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)

Pawaga Atoa Wosia Mzito kwa Ofisi ya Rais TAMISEMI

Imewekwa tar.: May 18th, 2018


Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR TAMISEMI) aliyemaliza muda wake katika Utumishi wa Umma Mohammed Pawaga amewataka watumishi wote wa umma kufanya kazi kwa kuzingatia utu.

Pawaga ameyasema hayo leo katika hafla fupi ya kumuaga iliyoandaliwa na watumishi wa idara, vitengo na Taasisi mbalimbali wa Ofisi ya Rais TAMISEMI iliyofanyika ndani ya ofisi hiyo.
Mbali na kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kumjaalia kufika hatua hiyo ya kustaafu kwa heshima lakini pia aliwaasa watumishi kutumia vyeo na madaraka yao katika kutatua changamoto za kazi kwa weledi.

“Kila mtu awe na ndoto ya kufika hapa, namshukru Mwenyezi Mungu kwa miaka 35 kuwa kazini kwani katika maisha kuna mambo mawili ambayo hayaepukiki ambayo ni kustaafu pamoja na kifo” Alisema Pawaga na kuongeza,

“Mambo haya yote yanahitaji maandalizi, kustaafu unatakiwa ujiandae mapema, kwamba kile ulichokipata unakitumiaje baadaye, na kifo unatakiwa ujiandae kwa matendo mema, nafurahi kuona nastaafu kwa amani” Alisema.

Alisema kiongozi yeyote anatakiwa kutengeneza viongozi na siyo wafuasi hata pale kunapotokea kutokuelewana inapaswa kutatua changamoto hiyo kwa kuzingatia utu jambo ambalo litakuongezea ujuzi na mafunzo katika utendaji wa kazi.

Aliwataka watumishi hao kutobadilika tabia baada ya kupata madaraka au pesa, kwani alisema vitu hivyo humbadilisha binadamu hivyo kuwashauri wale wenye vyeo kukumbuka walipotoka kabla ya kufanya maamuzi ili waweze kuwasaidia kila mmoja kwa kadiri wanavyoweza.

Akitoa salamu za pongezi za idara ya utawala na rasilimali watu mkurugenzi msaidizi wa utawala Mrisho Mrisho amempongeza Bw Pawaga kwa kuikuza TAMISEMI katika nyanja mbalimbali kama vile kuongeza vitengo, watumishi, upanuzi na ukarabati wa majengo pamoja na kuwepo kwa mazingira bora na rafiki ya kazi.

“Tunajivunia kuwa na wewe kwa miaka kumi uliyokaa hapa kwa sababu umechangia kuikuza TAMISEMI, ilikuwa chini na sasa ipo juu, umeanzisha vitengo vipya pamoja na taasisi mbalimbali sambamba na kuongeza idadi kwa watumishi” Alisema Mrisho

Mrisho amesema awali kulikuwa na watumishi 270 lakini kwa sasa wapo watumishi 658, lakini mbali na wingi huo lakini amesema Mkurugenzi huyo amewafundisha uwajibikaji jambo ambalo limesaidia watumishi kufanya kazi kwa umoja na kwa upendo wa hali ya juu.

Salamu kutoka Kitengo cha mawasiliano serikalini zilizotolewa na Fredy Kibano zilimuelezea Bw Pawaga kuwa ni kiongozi aliyefanikiwa kwa kiwango kikubwa kusimamia ukweli, haki na kutengeneza uwelewano ndani ya idara na vitengo vya TAMISEMI.

Mwenyekiti wa chama cha wafanyakazi Serikali Kuu TUGHE, tawi la TAMISEMI Jumbe Akida amesema kuwa Pawaga alijali stahiki za wafanyakazi bila kujali tofauti ya vyeo huku baadhi ya wawakilishi kutoka idara, vitengo na Taasisi mbalimbali zikimuelezea kama mtu aliyejali watu wote bila kuangalia umri wala madaraka.

Matangazo

  • Orodha ya waliopata vibali vya Uhamisho Septemba - Disemba 2022 (OR - TAMISEMI) January 21, 2023
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kidato cha Kwanza Waliorudia Mtihani January 15, 2023
  • Matumizi ya Lugha ya Kiswahili na Kingereza January 14, 2023
  • Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Kwanza 2023 December 14, 2022
  • Orodha ya Waliopangwa kwenye Vituo vya Kazi Kada za Afya (Awamu ya Pili) Agosti 2022 August 30, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA KWA KADA ZA AFYA (Marudio) July 20, 2022
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • LAAC YAPOKEA TAARIFA KUHUSU UTAWALA NA UENDESHAJI WA MAMLAKA ZA SERIKALI ZA MITAA

    March 14, 2023
  • SERIKALI YAWEKA MIKAKATI KATIKA USIMAMIZI WA MIRADI YA MENDELEO, UKUSANYAJI NA UDHIBITI WA MAPATO KATIKA HALMASHAURI

    March 13, 2023
  • WAUGUZI NA WAKUNGA WATAKIWA KUSIMAMIA MAADILI YA KAZI

    March 13, 2023
  • ACHENI KUTUMIANA NYARAKA ZA SERIKALI KWENYE MITANDAO YA KIJAMII NA BARUA PEPE BINAFSI - DKT. MPANGO

    March 13, 2023
  • Angalia zote

Video

Taarifa ya Ukusanyaji wa Mapato ya Halmashauri, kipindi cha robo ya pili ya mwaka wa fedha 2021/22
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.