Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

OPRAS Ni njia Muhimu ya Kuleta Ufanisi wa Watumishi

Imewekwa tar.: October 17th, 2018

Imeelezwa kuwa moja ya njia itakayowezesha taifa liweze kupiga hatua katika nyanja mbali mbali za maendeleo ni kwa taifa hilo kujiwekea mazingira ya kupima utendaji wa kazi kwa njia iliyo wazi na inayotoa nafasi kwa mtumishi kujitathmini mwenyewe.

Kauli hiyo imetolewa na Ndg Moses Chitanda (kwa niaba ya Katibu wa Tume ya Utumishi wa Walimu Bibi Winfrida Rutaindurwa) kwenye mafunzo ya siku mbili kwa Maafisa Elimu wa Mamlaka za Serikali za Mitaa juu ya mfumo wa (Open Performance Review Appraisal System-OPRAS) kwa Mkoa wa Manyara yanayofanyika jijini Dodoma.

Ndg Chitanda alisema mataifa mengi yaliyoendelea yaliwekeza katika rasilimali watu ikiwemo katika kupima na kufanya tathmini, na hii imewezesha mataifa hayo kupiga hatua za kimaendeleo.

Chitanda alisema, kujituma, nidhamu sambamba na kupokea maelekezo ndio njia pekee inayomwezesha mtumishi wa umma kupiga hatua katika utendaji wake wa kazi.

Mkurugenzi huyo wa rasilimali watu kutoka Tume ya Utumishi wa Walimu alifafanua, katika hali ya sasa nchi inahitaji watu wabunifu na wachapa kazi ambao watapatikana kwa rasilimali watu kutekeleza mfumo wa OPRAS.

“Mafunzo haya ya OPRAS yatasaidia kuibua ubunifu na utendaji uliotukuka hivyo tutegemee matokeo chanya kwa walimu”.

Chitanda alisema, shabaha kuu ya kuanza na kada ya walimu kwenye kuboresha ujazaji wa malengo ya OPRAS ni kutokana na kundi hilo kuwa na majukumu mengi yanayo fanana lakini pia weledi na wepesi wakusaidia kuisambaza elimu hiyo kwa makundi na kada zingine.

“Ili kuwa na utekelezaji wa uhakika wa utaratibu ulioboreshwa, wadau walikubaliana kuchagua kada moja katika utumishi wa umma ili liwe kundi la kuanzia, kwa kutumia vigezo mbalimbali, alisema Chitanda na kuongeza ilikubaliwa zoezi lianzie kwa walimu ambao kwa mujibu wa kazi zao ni lenye majukumu ya aina moja ambayo yanaweza kupangwa kwa kutumia maelezo ya kazi ya kada ya walimu”.  Lakini pia ni rahisi kueneza elimu hii mpya ya upangaji malengo ya mtumishi”.

Kwa upande wake Mwakilishi kutoka Mradi wa Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta ya Umma, PS3 Geoffrey Lufumbi, alisema mafunzo hayo ni mwanzo wa mafunzo yanayotolewa nchi nzima kwa Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa na kufuatiwa na walimu wote nchini.


Ndg Lufumbi alibainisha kuwa zoezi hili limefanikiwa kwa ushirikiano uliopo baina ya Serikali kupitia Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Tume ya Utumishi wa Walimu na PS3 kama sehemu mojawapo ya uimarishaji wa mifumo ya Rasilimali Watu kupitia Mradi wa PS3.  

“Maamuzi yote ya taasisi ikiwepo upangaji wa kazi na watumishi yatafanikiwa tu endapo OPRAS zitajazwa kwa ufasaha na itasaidia kutambua malengo kama yamefikiwa ama la”.


“Kama PS3 tunafanya kazi katika vipengele mbalimbali ikiwepo Utawala Bora, Mifumo ya TEHAMA, Mifumo ya Fedha, Tafiti tendaji pamoja na Rasiliamali Watu.

Akitoa mada katika kwenye mafunzo hayo ya siku mbili, mmoja ya wawezeshaji wa kitaifa wa OPRAS Ndg Samson Medda, alisema Mipango, malengo, dira na dhima ya taasisi vitafanikiwa kwa taasisi kuwa na OPRAS inayotekelezwa kwa umakini.

Katika Semina hiyo Ndugu Chitanda hakuacha kuwashukuru Watu wa marekani kupitia mradi wa uimarishaji wa mifumo ya sekta za umma PS3 kwa kazi kubwa wanayoifanya nchini yakuwezesha mifumo mbali mbali hususan ni imarishaji wa Mifumo ya Sekta ya Umma.

Mpango wa watumishi kwa njia ya wazi umefafanuliwa kupitia,  Miongozo na Sheria mbali mbali za utumishi wa umma ikiwepo Sheria ya Utumishi wa Umma ya Mwaka 2007 kupitia Kifungu cha (3) cha marekebisho Namba 18 ya 2007 kinafafanua dhima ya Makatibu Wakuu, Makatibu Tawala wa Mikoa, Wakuu wa Taasisi zinazojitegemea pamoja na Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa kutumia fomu za OPRAS katika kupima utendaji wa watumishi waliopo chini yao.

Anaandika Atley Kuni- OR TAMISEMI




Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert May 12, 2025
  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert May 12, 2025
  • Fursa kwa Wahitimu wa Kidato cha Nne 2024 kubadili Tahasusi na Kozi April 02, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI AJIRA ZA AFYA - TAMISEMI 2025 March 15, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • NENDENI MKAITANGAZE SERIKALI.

    May 24, 2025
  • SOKO LA KISASA LA NYAMA CHOMA LAZINDULIWA VINGUNGUTI

    May 24, 2025
  • DKT. Biteko asisitiza wazazi kuthamini nafasi ya familia katika malezi na makuzi ya mtoto.

    May 24, 2025
  • Mhe. Rais Samia amtaka Prof. Nagu kuboresha  huduma ya afya ya msingi.

    May 24, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.