Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Nzunda ataka walimu kuacha kuwachapa watoto viboko shuleni

Imewekwa tar.: July 25th, 2019

Na Mathew Kwembe, Mwanza

Serikali imewataka walimu kuacha kutegemea matumizi ya viboko shuleni kama njia ya kufundishia kwani inawajengea hofu na uwoga wanafunzi wa kushindwa kujiamini.

Agizo hilo limetolewa leo na Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa anayeshughulikia Elimu bwana Tixon Nzunda wakati akizungumza na walimu na wanafunzi wa shule ya msingi ya ufundi ya Bukumbi iliyopo katika wilaya ya Misungwi mkoani Mwanza.

Kwa mujibu wa Naibu Katibu Mkuu, mwenye mamlaka ya kuchapa viboko shuleni ni mwalimu mkuu peke yake, walimu wengine hawapaswi kufanya hivyo labda kwa kibali chake.

Amesema anachukizwa sana na tabia iliyojengeka miongoni mwa baadhi ya walimu ya kudhani kuwa ili aweze kumsaidia mtoto katika elimu yake ni lazima viboko vitumike awapo shuleni.

“Kwenye psychology (saikolojia) mmesoma au kuna authority (mamlaka) inayosema unaingia darasani na fimbo? Wanafunzi wanaenda shambani upo mgongoni mwao na fimbo?” amehoji Naibu Katibu Mkuu na kuongeza:

“Kwa kuwa mmenisomea taarifa yenu ya shule na nimeona matokeo yenu ya darasa la nne na la saba ni mazuri niwasihi hebu acheni kuwachapa watoto,” amesema.

Bwana Nzunda ameongeza kuwa kama hilo watashindwa basi angalau darasani mpige marufuku hakuna mwalimu kuingia na kiboko darasani.

 “Let the children be free ( acheni watoto wawe huru), build confidence ( wajengeeni watoto ujasiri) ili waweze kujiamini, kesho waje kuwa good teachers (walimu wazuri) waipende kazi ya ualimu, wengine wanaichukia kazi ya ualimu kwasababu walimu wao waliona toka wanaingia shule walimu wao ni fimbo tu, ” amesema.

Mbali na suala la viboko, Naibu Katibu Mkuu  pia alizungumzia suala la kuwa na mikataba ya utendaji kazi kwa walimu.

Amesema serikali inataka kila mwalimu,kila msimamizi wa kazi ana mkataba wa utendaji kazi, lengo ni kuwapima walimu kutokana na mchango wao kwa nchi yao.

Naibu Katibu Mkuu ametaja vigezo vitatu vitakavyotumika kuwapima walimu hao kuwa ni pamoja na kuhakikisha kila mwalimu awe na mfumo wa kufundishia na kujifunzia, ambapo kila mwalimu atapaswa kuwa na azimio la kazi, mpango kazi lakini pia tunataka kuona mwalimu ana strategic plan (mpango mkakati) wa wapi anataka kuwapeleka watoto wake.

Wakati huo huo bwana Nzunda amesema kuwa serikali imetumia bilioni 29 kwa ajili ya kumalizia maboma yaliyokuwa yamejengwa na wananchi ili yakamilike na kutumika katika shule zetu.

Aidha Serikali sasa inajenga madarasa 2897 kwa shule za msingi kwa wakati mmoja na kuongeza kuwa serikali ya awamu ya tano inalenga kutumia raslimali kidogo kuleta matokeo makubwa.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert May 12, 2025
  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert May 12, 2025
  • Fursa kwa Wahitimu wa Kidato cha Nne 2024 kubadili Tahasusi na Kozi April 02, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI AJIRA ZA AFYA - TAMISEMI 2025 March 15, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI

    May 23, 2025
  • PJT-MMMAM Yawezesha Uanzishwaji wa Vituo 206 vya Malezi ya Watoto Wadogo

    May 21, 2025
  • SERIKALI KUJENGA DARAJA LINALOUNGANISHA KIJIJI CHA NEGERO – KILINDI

    May 21, 2025
  • MHE. MCHENGERWA ABORESHA TAARIFA ZAKE KWENYE  DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

    May 20, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.