Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

NAIREJESHA TAMISEMI KWA WANANCHI’ MHE. MCHENGERWA

Imewekwa tar.: September 8th, 2023

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe. Mohamed Mchengerwa amesema atairejesha wizara hiyo kwa wananchi kwa kuhakikisha viongozi wote wanasikiliza na kutatua kero zao kwa wakati.


Pia amewaonya watendaji katika Mamlaka za Serikali za Mitaa ambao ni wabadhilifu, wala rushwa na wasiowajibika katika utendaji kazi wao hawatakuwa sehemu ya utendaji kazi wake.


Mchengerwa ameyasema hayo  leo Septemba 4, 2023 Jijini  Dodoma mara baada ya kuwasili  katika Ofisi za TAMISEMI zilizopo Mji wa Serikali, Mtumba.


“Niwaombe watumishi wenzangu kuwa sasa tunairejesha Ofisi ya Rais-TAMISEMI kwa wananchi, maana yake tunataka kufanyakazi hasa ili tuweze kufanikiwa na malengo ya Mheshimiwa Rais yaweze kutimia, hivyo lazima tufanyekazi usiku na mchana hakuna namna. Wizara yetu tunaisogeza kwa wananchi, tutasikiliza kero za wananchi.”amesema


Mchengerwa ametumia fursa hiyo kuwaagiza wakuu wa mikoa na wilaya kuhakikisha wanatoka ofisini na kwenda kusikiliza na kutatua kero za wananchi na kusisitiza kuwa asilimia 45 ya wakuu wa wilaya  hawafanyi majukumu yao.


“Kuanzia sasa wakuu wa mikoa wote, wakuu wa wilaya washuke chini kusikiliza kero za wananchi, asilimia 45 ya wakuu wa wilaya hawafanyikazi kabisa, hawasikilizi kero za wananchi, kwa hiyo tunataka kila mmoja afanyekazi ili tuweze kutimiza malengo ya watanzania, malengo ya Chama cha Mapinduzi, malengo ya Rais wetu.”


Kuhusu utekelezaji wa miradi ya maendeleo, Mchengerwa amewaonya wakurugenzi wa halmashauri ambao wamekalia fedha za miradi na kusisitiza kuwa hataongeza muda wa utekelezaji wa miradi hiyo.


“Mheshimiwa waziri (Kairuki) umesema kuna miradi mingi ambayo tayari imeshaanzwa lakini kuna baadhi ya watu hawajaitimiza, uliwawekea deadline, sitaongeza hata siku moja, na nitaomba unikabidhi hayo makaratasi, kila mmoja kule aliko lazima ajue, Wakurugenzi ambao wamekalia fedha za miradi sitaongeza siku hata moja.”


Aidha, Mchengerwa amesema watendaji ambao  hawatimizi wajibu wao, wabadhilifu wa fedha za umma na wala rushwa hawatakuwa sehemu ya utendaji wake kwenye serikali hii.


Amesema pia hatakubaliana na uonevu wa watumishi na kuwataka maafisa utumishi katika mamlaka za serikali za mitaa kusikiliza kero za watumishi na kuzitatua.


“Kuwaonea watumishi hiyo sitakubali, kila mmoja sasa lazima aanze kujipanga, najua asilimia 76 ya watumishi wa umma wako TAMISEMI hivyo tunakazi kubwa ya kulinda haki za watumishi.”


“Nilipokuwa utumishi walinyooka, hivyo maafisa utumishi huko mliko nataka msikilize kero za watumishi kwenye maeneo yenu.”

Aidha, Mchengerwa ameweka bayana kuwa hayuko tayari kufanya kazi na mtumishi asiyefanyakazi na kusisitiza kuwa atamuweka kando.


“Katibu Mkuu (Adolf Ndunguru) utakuwa na kazi ya kufanya, yule asiyefanyakazi nitamuweka kando, sitakubali kwenda na mtu hataki kufanyakazi, sitakubali kwenda na afisa utumishi hasikilizi kero za watumishi, nilikuwa hakimu kwahiyo nilikuwa najua namna ya kugawa haki.”


“Ukifanya kazi na kutimiza majukumu yako kwa haki, utakiwa karibu na mimi, lakini ujanja ujanja na kufanyakazi kwa mazoea sio sehemu ya utendaji wangu wa kazi, kwa hiyo niwaombe lazima tubadilike.”


 “Hufanyikazi nitakuweka kado nah ii ni kwa yoyote, hakuna gold father hapa kama mtu ameletwa na mtu kwa jina lazima afanyekazi kwa bidii na hii ni kwa kila mtumishi hii si kwa watendaji wa wizara pekee bali mpaka kijijini kama umepata kazi kwa jina la mtu ufanyekazi kwa bidhii sitakubali hata kidogo.”


Mchengerwa amesema Serikali imepeleka fedha nyingi za kutekeleza miradi katika mamlaka za serikali za mitaa na kubainisha kuna baadhi wasiotekeleza wajibu wao na kusisitiza kuwa hatamvumilia mtu yeyote.


“Serikali imepeleka fedha nyingi lakini miradi mingi haijamailika kwa watu kuiba, wanakula rushwa,  ubadhilifu wa fedha miradi…

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert May 12, 2025
  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert May 12, 2025
  • Fursa kwa Wahitimu wa Kidato cha Nne 2024 kubadili Tahasusi na Kozi April 02, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI AJIRA ZA AFYA - TAMISEMI 2025 March 15, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI

    May 23, 2025
  • PJT-MMMAM Yawezesha Uanzishwaji wa Vituo 206 vya Malezi ya Watoto Wadogo

    May 21, 2025
  • SERIKALI KUJENGA DARAJA LINALOUNGANISHA KIJIJI CHA NEGERO – KILINDI

    May 21, 2025
  • MHE. MCHENGERWA ABORESHA TAARIFA ZAKE KWENYE  DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

    May 20, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.