Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Mweli aweka bayana mafanikio ya Elimu Bure

Imewekwa tar.: February 8th, 2020

SERIKALI inajenga shule 1,000 mpya za Sekondari ikiwa ni kukabiliana na ongezeko la wanafunzi lililotokana na kuanza kutolewa kwa elimu bila malipo.

 Hayo aliyabainisha jijini hapa na Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (anayeshughulikia elimu), Gerald Mweli alipokuwa akizungumzia mafanikio ya utekelezaji wa elimu bila malipo kwa elimumsingi ulioanzishwa na Rais John Magufuli.

Alisema kupitia programu ya kuboresha elimu ya sekondari, serikali inajenga shule 1,000 mpya ambazo zitasaidia uchukuaji wa wanafunzi wote waliofaulu.

 “ Hili suala la kufanya machaguo ya pili kwa wanafunzi wanaojiunga na elimu ya sekondari linafika mwisho kwasababu serikali inajenga shule mpya 1,000 za sekondari, achilia mbali zile zinazoboreshwa na kukarabatiwa.”

  “ Ikumbukwe pia serikali iliamua kutoa elimu bila malipo kuanzia mwaka 2016 na kulikuwa na idadi kubwa ya wanafunzi waliandikishwa elimu ya msingi ambao kwa sasa wako darasa la tano, hivyo ujenzi wa shule mpya pia ni maandalizi ya kuwapokea wanafunzi hawa.”

 Mweli alisema shule hizo zitakuwa na uwezo wa kuchukua wanafunzi 600 kwa kila shule kwa wakati mmoja.

“ Hivyo kwa kujenga shule hizi mpya, ni kuhakikisha kuwa hakuna mtoto ambaye atafaulu atakosa nafasi ya kuendelea na masomo kutokana na upungufu wa vyumba vya madarasa au kukosa shule.”

Alisema Serikali kuanza kutoa elimu bila malipo hakukuanza kwa bahati mbaya, kuna tafiti zilifanyika mwaka 2014/2015 ambazo zilionesha takribani watoto milioni 3.5 walio na umri wa kwenda shule hawako shuleni na moja ya sababu ilikuwa ni wazazi kukosa fedha lakini pia ni katika kutekeleza malengo ya maendeleo endelevu.


Aidha, Mweli alisema kwa mwaka huu, mikoa na maeneo ambayo wanafunzi waliofaulu hawakupata nafasi katika chaguo la awali wameamua maeneo hayo wanafunzi wasome kwa zamu katika kipindi cha miezi miwili.

" Sio kweli kuwa wanafunzi watalundikana, kuna maeneo wanafunzi wameongeza wawili watatu, lakini kuna maeneo wataingia kwa zamu na utaratibu kama huu sio mpya hata huko nyuma kulikuwa na wanafunzi wanasoma kwa zamu."

Alisema hadi kufikia Februari 29 mwaka huu, madarasa yanayojengwa yatakuwa yamekamilika na wanafunzi kuingia kwenye utaratibu wa sasa.

Kwa upande wa shule za msingi, Mweli alisema katika kipindi cha kuanzia mwaka 2016 mpaka sasa shule mpya za msingi 295 zimejengwa na madarasa 2000 yamejenga.

" Shule ya Msingi ya Majimatitu ya Jijini Dar es Salaam ambayo ilikuwa na idadi kuwa ya wanafunzi walioandikishwa mwaka 2016 ni moja ya shule ambazo zimenufaika na ujenzi wa shule mpya, kuna moja tumejenga eneo hilo lakini shule ya pili tumeijenga aneo ambalo serikal imepewa ekari tatu bure."

Mweli alisema kabla ya kuanza kutolewa elimu bila malipo uandikishaji wa wanafunziwa elimu ya awali walikuwa ni milioni moja nchi nzima na asilimia 55 ya wanafunzi walioandikishwa darasa la kwanza walikuwa wakipitia kwenye elimu ya awali.

 “ Tangu tuanze kutoa elimu bila malipo wanafunzi wanaoandikishwa elimu ya awali wamefikia wanafunzi 1,295,000 kwa mwaka na asilimia 82 ya wanafunzi wanaoandikishwa darasa la kwanza wanakuwa wamepitia kwenye elimu hiyo ambayo inawasaidia katika stadi za kusoma, kuandika na kuhesabu.”



Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert May 12, 2025
  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert May 12, 2025
  • Fursa kwa Wahitimu wa Kidato cha Nne 2024 kubadili Tahasusi na Kozi April 02, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI AJIRA ZA AFYA - TAMISEMI 2025 March 15, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • PJT-MMMAM Yawezesha Uanzishwaji wa Vituo 206 vya Malezi ya Watoto Wadogo

    May 21, 2025
  • SERIKALI KUJENGA DARAJA LINALOUNGANISHA KIJIJI CHA NEGERO – KILINDI

    May 21, 2025
  • MHE. MCHENGERWA ABORESHA TAARIFA ZAKE KWENYE  DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

    May 20, 2025
  • Msovela: Fanyeni Kazi Kama Timu Kuleta Maendeleo

    May 20, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.