• Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Machapisho
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
    • Green and Smart Cities
    • Miongozo ya Kilimo
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Michoro ya Ujenzi
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)

Mweli awatolea uvivu kidato cha Nne, Sita, awajenga kinidhamu

Imewekwa tar.: January 11th, 2021

Na Atley  Kuni, Shinyanga

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, (anayeshughulikia elimu), Bw. Gerald Mweli, amesema Wanafunzi wa kidato cha Nne na Sita, muda wao walionao kwa sasa ni miezi Minne kwa kidato cha Sita na Miezi tisa kwa kidato cha Nne kuamua hatma ya maisha yao kielimu na mafanikio yao kimaisha. Bw. Mweli aliyazungumza hayo wakati wa ziara yake ya kikazi leo tarehe 11 Januari, 2021 mkoani Shinyanga

“Muda mlionao ninyi ni mchache sana wa kuamua hatma ya maisha yenu kielimu, kuna wenzenu walifukuzwa shule huko mkoani Arusha juma moja kabla ya kuanza mitihani yao ya kuhitimu baada ya nidhamu yao kwenda kinyume na sheria, taratibu na kanuni za shule kwa kuharibu miundombinu ya shule.” alisema Mweli na kuzidi kusisitiza kuwa Uvutaji bangi, uzinzi, upigaji mawe na kuharibu miundombinu ya shule ni baadhi ya makosa ambayo yataweza kuwafukuzisha shule hata kama wamebakiza siku mbili kuanza mitihani yao, hivyo akawaasa wawe wanafunzi watiifu.

Mweli amewaonya wanafunzi hao kuwa, endapo watashindwa kuzingatia nidhamu wakiwa shuleni hapo, basi ipo siku watafunzwa nidhamu wakiwa chini ya miongozo ya vyombo vya dola vya polisi na Magereza, “Sitaki kuona vijana wangu, wadogo zangu mnafikia huko.

“Kidato cha sita tambueni mna miezi minne tu ya kuamua hatma yenu, na ninyi kidato cha Nne mna miezi Tisa tu, hivyo ni hiyari yenu kuamua nini mnakihitaji katika Maisha yenu siku zijazo, ni wazi kwamba, kusoma sio kibali cha kutajirika, lakini itakusadia na kukujengea heshima mbele ya jamii yako.” Mweli amewasisitiza wanafunzi hao.

Awali akitoa taarifa ya Shule ya Sekondari Shinyanga, mbele ya Naibu Katibu Mkuu, Mkuu wa Shule hiyo Benard Ishengoma, amemwambia Naibu Katibu Mkuu kuwa, Shule ya Sekondari Shinyanga ilipokea kiasi cha Shilingi 897,335,247.05 kwa ajili ya ukarabati wa shule hiyo kongwe yenye zaidi ya miaka 55 toka kuanzishwa kwake mnamo mwaka 1966.

Akiwa shuleni hapo, Naibu Katibu Mkuu, amewakumbusha walimu majukumu yao lakini pia, kuwataka kuwasimamia wanafunzi na kuwahimiza kujiunga na Klabu mbalimbali ikiwepo Skauti, lakini pia kuwakumbusha kuzingatia suala la uzalendo ikiwepo kuwafundisha wanafunzi nyimbo za kizalendo ikiwepo, Wimbo wa Taifa, Wimbo wa Afrika Mashariki sambamba na Wimbo wa Uzalendo wa Tanzania nakupenda kwa moyo wote, kila mara.

Naibu Katibu Mkuu Gerald mweli amefika shuleni hapo ikiwa ni sehemu ya ziara yake, ambapo katika siku ya kwanza mbali ya kutembelea shule ya Sekondari Shinyanga ametembelea na kukagua Shule ya msingi Buhangija, Shule ya Sekondari Mwadui ufundi na Shule ya Sekondari Maganzo na kisha kufanya mkutano wa pamoja na Waratibu Elimu Kata, Wakuu wa Shule na Walimu Wakuu.

MWISHO

Matangazo

  • Orodha ya waliopata vibali vya Uhamisho Septemba - Disemba 2022 (OR - TAMISEMI) January 21, 2023
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kidato cha Kwanza Waliorudia Mtihani January 15, 2023
  • Matumizi ya Lugha ya Kiswahili na Kingereza January 14, 2023
  • Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Kwanza 2023 December 14, 2022
  • Orodha ya Waliopangwa kwenye Vituo vya Kazi Kada za Afya (Awamu ya Pili) Agosti 2022 August 30, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA KWA KADA ZA AFYA (Marudio) July 20, 2022
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • BODI YA MIKOPO YA SERIKALI ZA MITAA KUSUKWA UPYA

    January 23, 2023
  • MAKAMU WA RAIS AWAPONGEZA DODOMA JIJI KWA UWEKEZAJI

    January 20, 2023
  • SERIKALA YASISITIZA KILA MMOJA KUTUNZA MAZINGIRA

    January 20, 2023
  • TANZANIA ITAENDELEA KUSHIRIKANA NA WADAU KATIKA MAPAMBANO DHIDI YA UKIMWI

    January 20, 2023
  • Angalia zote

Video

Taarifa ya Ukusanyaji wa Mapato ya Halmashauri, kipindi cha robo ya pili ya mwaka wa fedha 2021/22
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.