Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Mweli ahoji kushuka kwa Kiwango cha Ufaulu Shinyanga

Imewekwa tar.: March 11th, 2020

Naibu Katibu Mkuu anayeshughulika Elimu OR-TAMISEMI Gerald Mweli amehoji kushuka kwa kiwango cha ufaulu kwa Mkoa wa Shinyanga Kitaifa kutoka nafasi ya 3 kwa mwaka 2018 hadi nafasi ya 13 kwa mwaka 2019.

Akizungumza katika ziara yake ya kikazi Mkoani humo amesema haiwezekani kwa kipindi cha mwaka mmoja Mkoa huo kuporomoka kitaaluma kwa kiwango hicho jambo lililomfanya aanzie ziara yake Mkoani hapo ili kufahamu kulikoni na  namna walivyojipanga kurudi katika nafasi nzuri zaidi kitaifa.

“Akielezea sababu za kuporomoka huko Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga ambaye pia ni Afisa Elimu Mkoa huo Mohamed Kahundi amesema tatizo kubwa lililopo ni uhaba wa walimu haswa wa masomo ya Sayansi, uchakavu wa miundombinu pamoa na hulka ya Mkoa huu wa kupendelea ufugaji hivyo kuhamasisha watoto kwenda kufuga kuliko kuzingatia masomo.

“Tunajitahidi sana katika kuhakikisha tunatoa elimu bora lakini upungufu wa walimu haswa katika masomo ya Sayansi umechangia kwa kiasi kikubwa kurudisha nyuma jitihada wa kupandisha kiwango cha elimu katika Mkoa huu” alisema Kahundi.

Aidha Kahundi aliongeza kuwa uchakavu wa miundombuni katika baadhi ya shule piani miongoni mwa changamoto zinazoshusha ari ya walimu kufundisha kwa ufanisi lakini pia na wanafunzi kutokufanya vizuri katika masomo yao.

Akizungumzia hulka ya kupenda kuchunga kuliko masomo amesema wazazi wa Mkoa huu haswa ameneo ya pembezoni hupendelea kuwapeleka watoto machungani lakini sio kumshawishi mtoto kutumia muda wake wa mapumziko kujisomea hivi vyote kwa ujumla vimechangia katika kushusha kiwango chetu cha Elimu kwa kipindi husika alisisitiza Kahundi.

Naibu Katibu Mkuu Mweli amesema haoni kama sababu zilizoainishwa zinaweza kuchangia moja kwa moja kushusha kiwango cha Elimu kwa sababu changamoto hizo sio ngeni katika mazingira yao na ilikuwaje katika mwaka 2018 kufanya vizuri na mwaka uliofutia kufanya kushuka je ni kwamba changamoto hizo zimetokea baada ya mwaka huo au zilikuwepo kwa kipindi chote.

“Nimezipoeka lakini hazijanishawishi na inabidi kushughulikia kila moja kwa namna yake kama ni ya miundombinu ishughulikiwe kimiundombinu na kama ni ya Kitaalumu halkadhalika nayo iweze kushughulikiwa kitaaluma” alisema Mweli.

Kwa sasa hivi tunarekebisha miundombinu katika shule nyingi Nchini kupitia mradi wa Lipa kulingana na matokeo(Paying for Result – Ep4r), shule nyingi sana Nchini tumeshazifikia na kupitia ziara hii pia tumekuja kuona uchakavu wa shule za Mkoa huu ila nazo ziweze kufanyiwa marekebisho hivyo hili sasa litakwisha na sitarajii kuliskia tena kama changamoto alisisiza.

Aliongeza kuwa changamoto iliyoibaini kutokana na taarifa hiyo ni usimamizi; Nina mashaka na usimamizi kuanzia kwenye Waratibu wa Elimu Kata, Walimu Wakuu, Walimu wa Taaluma pamoja na walimu katika kufundisha vipindi ipasavyo.

Suala la upungufu wa walimu sioni kama ni changamoto katika Mkoa huu maana walimu wa masomo ya sanaa takwimu zinaonyesha wapo wa kutosha je hawa wanafanya kazi ipasavyo kabla hamjaanza kuomba hao walimu wa Sayansi tunataka kuona hawa waliopo wamefanya kazi kwa kiasi gani na imeleta matokeo chanya kwa kiwango gani alihoji Mweli.

Hivyo tuongeze nguvu katika ksuimamia katika ngazi ili kila mtu atimizie wajibu wake nina uhakika mtarudi kwenye kiwango kile au hata na zaidi kwa sababu tayari mlionyesha mnaweza na nitapenda kuona mafanikio yale ya mwaka 2018 yanafikiwa.


Naibu Katibu Mweli katika ziara yake Mkoani Shinyanga mefanya kikao na wasimamizi wa Elimu sambamba na kutembelea shule ya ufundi Mwadui , shule mpya ya wasichana inayoendelea kujengwa hapo hapo Mwadui zote zipo katika Halmashauri ya Kishapu kuangalia uchakavu wa miundombinu na namna Serikali inavyoweza kuchukua hatua za makusudi za ukarabati ili kuboresha utoaji wa Elimu.

Kupitia ziara hiyo pia Mweli atatembelea Mkoa wa Geita, Mwanza pamoja na Simiyu.

Mwisho.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert May 12, 2025
  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert May 12, 2025
  • Fursa kwa Wahitimu wa Kidato cha Nne 2024 kubadili Tahasusi na Kozi April 02, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI AJIRA ZA AFYA - TAMISEMI 2025 March 15, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI

    May 23, 2025
  • PJT-MMMAM Yawezesha Uanzishwaji wa Vituo 206 vya Malezi ya Watoto Wadogo

    May 21, 2025
  • SERIKALI KUJENGA DARAJA LINALOUNGANISHA KIJIJI CHA NEGERO – KILINDI

    May 21, 2025
  • MHE. MCHENGERWA ABORESHA TAARIFA ZAKE KWENYE  DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

    May 20, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.