• Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Machapisho
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
    • Green and Smart Cities
    • Miongozo ya Kilimo
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Michoro ya Ujenzi
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)

Msiwaadhibu Walimu kwa Matokeo Mabaya ya Wanafunzi - Nzunda

Imewekwa tar.: November 14th, 2018

Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia Elimu Ofisi ya Rais TAMISEMI Tixon Nzunda amewataka Viongozi katika Mikoa, Mamlaka za Serikali za Mitaa na Mamlaka nyingine zinazohusika na walimu kutowaadhibu walimu kutokana na matokeo mabaya ya mitihani ya mwisho.

Nzunda ametoa kauli hiyo hapo jana wakati wa kikao kazi alichofanya mjini Kigoma na Maafisa Elimu Wilaya Msingi na Sekondari, Maafisa Elimu Taaluma Msingi na Sekondari, Maafisa Vielelezo na Takwimu Msingi na Sekondari, Waratibu Elimu Kata, Wakuu wa shule za Msingi na Sekondari, baadhi ya walimu wa msingi na sekondari na Wathibiti Ubora wa Elimu kwa lengo la kutoa maagizo ya Serikali kwa mkoa huo na mikoa mingine nchini ili kuendelea kuboresha elimu mashuleni.  

“Viongozi katika Sekta ya Elimu wasifanye kazi ya kuwaadhibu Walimu, Waratibu wa Elimu Kata kwa sababu tu ya wanafunzi kufeli mtihani wa mwisho wa kidato cha nne, kidato cha sita au mtihani wa kuhitimu darasa la saba, kwa sababu inawezekana watoto wamefeli si kwa sababu yenu ni kwa sababu ya watoto wenyewe, ila tuwaadhibu walimu kwa sababu ya kushindwa kutoa taaluma, utoro madarasani, utoro shuleni, kutokuzingatia taratibu za ufundishaji na ujifunzaji, suala la maadili, hilo ndilo liwe sababu kama kuna haja ya kufanya hivyo”

Amesema matokeo ya mtihani wa mwisho yawe ni kipimo cha kujitathmini, kujipanga upya na kujisahihisha kwani wakifanya hivyo itakuwa rahisi kuimarisha taaluma nchini katika ngazi zote.

Aidha, amekemea tabia ya wizi na uvujaji wa mitihani na utoaji wa rushwa na kwamba mtumishi wa Umma atakayebainika ataondolewa katika utumishi wa Umma na atafikishwa katika vyombo vya sheria badala ya kuendelea kuwakumbatia na kujenga Taifa la wezi, wasio na uwezo na mzigo Taifa.

Amewaasa wataalam hao kuacha kufundisha masomo kwa kuchanganya lugha ya Kiswahili na kiingereza kwani kwa kufanya hivyo kunapunguza umahiri wa lugha kwa watoto na walimu wenyewe.

Kuhusu suala la utoro amewataka watendaji hao kuchukua hatua kwani suala la utoro linakuwa sugu siku hadi siku na kwa hivi sasa kwa mujibu wa taasisi moja ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam utoro wa walimu wa aina tofauti mashuleni umefikia asilimia 56 jambo ambalo ni hatari kwa ustawi wa taaluma nchini.

Bwana Salum Mohammed ni Mkuu wa shule ya Gungu sekondari amesema kikao hicho kilikuwa na tija na kwamba maagizo yote ya Serikali watayazingatia na kuyatekeleza mara moja, lakini ametoa ombi kwa Serikali kukumbuka kuwapandisha madaraja ili kuwamotisha walimu waweze kufanya kazi zao vizuri na kuleta matokeo chanya kwani ni muda mrefu madaraja hayo yalisimamishwa.

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI (ELIMU) Tixon Nzunda, amemaliza ziara yake ya kikazi mkoani Kigoma na kurejea Jijini Dodoma kuendelea na majukumu mengine ya kitaifa.

                             Anaandika Fred Kibano


Matangazo

  • Orodha ya waliopata vibali vya Uhamisho Septemba - Disemba 2022 (OR - TAMISEMI) January 21, 2023
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kidato cha Kwanza Waliorudia Mtihani January 15, 2023
  • Matumizi ya Lugha ya Kiswahili na Kingereza January 14, 2023
  • Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Kwanza 2023 December 14, 2022
  • Orodha ya Waliopangwa kwenye Vituo vya Kazi Kada za Afya (Awamu ya Pili) Agosti 2022 August 30, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA KWA KADA ZA AFYA (Marudio) July 20, 2022
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • LAAC YAPOKEA TAARIFA KUHUSU UTAWALA NA UENDESHAJI WA MAMLAKA ZA SERIKALI ZA MITAA

    March 14, 2023
  • SERIKALI YAWEKA MIKAKATI KATIKA USIMAMIZI WA MIRADI YA MENDELEO, UKUSANYAJI NA UDHIBITI WA MAPATO KATIKA HALMASHAURI

    March 13, 2023
  • WAUGUZI NA WAKUNGA WATAKIWA KUSIMAMIA MAADILI YA KAZI

    March 13, 2023
  • ACHENI KUTUMIANA NYARAKA ZA SERIKALI KWENYE MITANDAO YA KIJAMII NA BARUA PEPE BINAFSI - DKT. MPANGO

    March 13, 2023
  • Angalia zote

Video

Taarifa ya Ukusanyaji wa Mapato ya Halmashauri, kipindi cha robo ya pili ya mwaka wa fedha 2021/22
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.