• Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Machapisho
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
    • Green and Smart Cities
    • Miongozo ya Kilimo
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Michoro ya Ujenzi
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)

Maafisa Manunuzi na Wakaguzi wa ndani kutoka halmashauri 118 wapigwa msasa

Imewekwa tar.: February 11th, 2019

Jumla ya watumishi 280 ambao ni Maafisa Manunuzi na Wakaguzi wa Ndani kutoka Halmashauri 118 za Mikoa 16 nchini wanashiriki mafunzo ya siku nne yanayofanyika mkoani Morogoro kwa lengo la kuwajengea uwezo maafisa hao ili waweze kuutumia vizuri Mfumo wa utoaji wa taarifa za ununuzi pamoja na marekebisho ya Sheria ya Ununuzi wa Umma ya mwaka 2016 pamoja na marekebisho ya kanuni zake.

Mafunzo hayo yanaendeshwa na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa kupitia Programu ya Maboresho ya Fedha za Umma Awamu ya V (PFRMP V) kwa kushirikiana na Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) ambao ndiyo wawezeshaji kwenye mafunzo hayo.

Akifungua mafunzo hayo jana mjini Morogoro, Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro bwana Clifford Tandari alisema kuwa baada ya serikali kuifanyia marekebisho kadhaa sheria ya manunuzi ya umma kulikuwa na umuhimu mkubwa kwa watendaji hao kujengewa uwezo ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.


Aliongeza kuwa Serikali iliona kulikuwa na haja ya kuifanyia marekebisho sheria hiyo ili iweze kuleta matokeo yaliyokusudiwa hasa kufanikisha lengo la upatikanaji wa thamani halisi ya fedha katika manunuzi kama ilivyokuwa imekusudiwa.
Kwa mujibu wa Katibu Tawala huyo, baadhi ya changamoto zilizokuwa zikiikabili sekta ya Ununuzina kupelekea Sheria na Kanuni hizo kurekebishwa ni pamoja na bei ya manunuzi kuwa kubwa kulinganisha na bei ya soko, gharama za mchakato wa manunuzi kuwa juu kutokana na mpangilio mbaya wa ununuzi na pia kutozingatia sheria, kanuni na miongozo inayotolewa na Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA.
Bwana Tandari alizitaja changamoto nyingine kuwa ni pamoja na mchakato wa ununuzi kuchukua muda mrefu jambo ambalo limekuwa likileta athari mbalimbali ikiwemo kupanda kwa bei ya huduma, vifaa au kandarasi kutokana na hali ya soko kubadilika.
Changamto nyingine ni kutotumiwa kwa viwango hasa kwenye huduma na bidhaa kama vile utengenezaji wa magari, ununuzi wa bidhaa mtambuka hasa bidhaa zinazopatikana GPSA na MSD kwani lazima bidhaa hizo zitoke huko.
Bwana Tandari alieleza pia tofauti kati ya taratibu za ununuzi zinazotumiwa na Halmashauri na Taasisi nyingine za Umma hasa kutokana na kukosekana kwa taratibu za kisheria zinazowahakikishia wauzaji kuwa ununuzi unazingatia ushindani thabiti, haki, uwazi na uwajibikani, uadilifu na maslahi ya taifa.

Katibu Tawala wa Mkoa aliongeza kuwa kutokana na marekebisho ya sheria ya ununuzi serikali inatarajia kuongezeka kwa ushindani na uwazi katika ununuzi wa uma, kuongezeka kwa uwajibikaji na kupungua kwa gharama za ununuzi wa magari kwa kupitia Wakala wa Huduma ya Ununuzi Serikalini na kuboresha ukidhi na uzingatiaji wa sheria ya ununuzi ambapo sheria imetoa fursa kwa PPRA kuzikagua taasisi nunuzi na kupima kama zimezingatia ukidhi wa sheria katika ununuzi.
Bwana Tandari alisema kuwa sheria imetoa mwanya pia wa kutumia mfumo wa TEHAMA  ambapo taasisi nunuzi huwasilisha taarifa zake PPRA kwa kutumia mifumo iliyowekwa.
Kwa upande wake Mratibu wa Mafunzo hayo bwana Lucas Mrema alisema kuwa mikoa 16 inayoshiriki mafunzo haya ni  mbali na ile mikoa 10 iliyokuwa ilishiriki kwenye utekelezaji wa programu ya usimamizi wa fedha za Umma awamu ya nne.
" Katika utekelezaji wa programu ya Usimamizi wa Matumizi ya fedha za Umma awamu ya tano tunatarajia kuwa mikoa yote 26 na halmashauri zake 185 zitashirikishwa," alisema.
Kwa upande wake Mhandisi Mary Swai Kaimu Mkurugenzi Msaidizi kutoka Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) aliwataka Maafisa Manunuzi kuhakikisha kuwa wanafuata taratibu zote za manunuzi pindi wanapotekeleza najukumu yao.
Aliongeza kuwa Maafisa Manunuzi wanapaswa kuhakikisha kuwa makini katika utekelezaji wa mikataba mbalimbali ambapo alidai kuwa pindi mkataba unaposainiwa wahakikishe kuwa mkataba huo unatekelezwa vizuri.
Anaandika Mathew Kwembe, Morogoro

Matangazo

  • Orodha ya waliopata vibali vya Uhamisho Septemba - Disemba 2022 (OR - TAMISEMI) January 21, 2023
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kidato cha Kwanza Waliorudia Mtihani January 15, 2023
  • Matumizi ya Lugha ya Kiswahili na Kingereza January 14, 2023
  • Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Kwanza 2023 December 14, 2022
  • Orodha ya Waliopangwa kwenye Vituo vya Kazi Kada za Afya (Awamu ya Pili) Agosti 2022 August 30, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA KWA KADA ZA AFYA (Marudio) July 20, 2022
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • BODI YA MIKOPO YA SERIKALI ZA MITAA KUSUKWA UPYA

    January 23, 2023
  • MAKAMU WA RAIS AWAPONGEZA DODOMA JIJI KWA UWEKEZAJI

    January 20, 2023
  • SERIKALA YASISITIZA KILA MMOJA KUTUNZA MAZINGIRA

    January 20, 2023
  • TANZANIA ITAENDELEA KUSHIRIKANA NA WADAU KATIKA MAPAMBANO DHIDI YA UKIMWI

    January 20, 2023
  • Angalia zote

Video

Taarifa ya Ukusanyaji wa Mapato ya Halmashauri, kipindi cha robo ya pili ya mwaka wa fedha 2021/22
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.