Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Kilimanjaro, Lindi tishio soka wasichana UMITASHUMTA

Imewekwa tar.: June 27th, 2019

Na Mathew Kwembe, Mtwara

Timu za mikoa ya Kilimanjaro, Lindi na Manyara zimekuwa tishio kwa timu nyingine zinazoshiriki michuano ya UMITASHUMTA inayoendelea katika viwanja vya chuo cha ualimu Mtwara baada ya jana kutoa vipigo vikali kwa wapinzani wao.

Timu ya soka wasichana ya mkoa wa Kilimanjaro iliibugiza Katavi magoli 7-0, Lindi nayo ikiifunga Ruvuma 5-0 huku Mara nayo ikitoa kipigo kama hicho kwa kuichapa Rukwa 5-0.

Matokeo mengine katika mchezo huo yanaonyesha kuwa Manyara iliifunga Singida 2-1, Simiyu ilipata ushindi wa chee baada ya Arusha kutofika uwanjani, Kagera imeifunga Mbeya 2-0, huku Iringa ikifungwa na Geita 0-3.

Katika mchezo wa soka maalum Kagera iliifunga Katavi magoli 9-0, Shinyanga wakiibugiza Rukwa magoli 6-0, Njombe walifungwa na Kilimanjaro 0-1, Manyara ikitoka sare na Singida ya 0-0, Tanga ikifungwa na Mtwara magoli 1-4, Dodoma ikiichapa Geita 1-0, na Mara ilifungwa na Ruvuma 1-3.

Kwa upande wa soka wavulana matokeo yanaonyesha kuwa Dodoma walifungwa na Dar es salaam 2-3, Kilimanjaro iliifunga Tanga 1-0, Singida iliifunga Mara 2-0, Lindi ilitoka suluhu ya bila kufungana na Simiyu, na Mtwara ilifungwa na Pwani magoli 0-3.

Iringa ilifungwa na Mwanza magoli 1-5, Manyara ilichapwa na Shinyanga magoli 0-5, Ruvuma iifungwa na Geita 0-2, Kigoma iliichapa Njombe 1-0, huku Songwe nayo ikpata kipigo kutoka kwa Kagera kwa magoli 0-2, Tabora ilitoka suluhu Rukwa na Arusha ilifungwa na Morogoro magoli 1-3.

Michezo mingine iliyochezwa leo ni pamoja na mchezo wa mpira wa mikono ambapo matokeo yanaonyesha kuwa Kagera ilifungwa na Songwe magoli 3-11, Tabora wasichana walifungwa na Lindi  magoli 5-9, Rukwa wavulana walifungwa na Dar es salaam magoli 12-31, Mbeya walitoka sare na Mara kwa kufungana magoli 10-10, Tabora waliifunga Iringa 19-14, na kagera walifungwa na Pwani 9-10.

Matokeo mengine Njombe wavulana walifungwa na Tanga magoli 4-27, Dodoma wasichana waliifunga Shinyanga magoli 15-7, Shinyanga wavulana walifungwa na Manyara 6-13, Lindi wasichana waliifunga Kagera 13-1, Kagera wavulana walifungwa na Dodoma 12-23, Manyara wasichana na Tabora walitoka sare 8-8, Pwani wavulana iliifunga Njombe 11-8, na Mbeya wavulana walifungwa na Morogoro 6-15.

Shinyanga wasichana iliifunga katavi 10-9, Mtwara wavulana ilifungwa na Arusha 5-9, Morogoro wasichana waliichapa Mtwara 17-7, Songwe wavulana waliibugiza katavi magoli 20-13, Tanga wavulana waliifunga Kigoma 11-9, Mara wasichana iliipa kipigo Songwe 19-01, Mara wavulana ilifungwa na Morogoro 17-19, Dar es salaam wavulana iliifunga Ruvuma 24-03, na Mwanza wasichana iliichapa Singida 08-03.

Katika mchezo wa riadha kuruka juu wavulana medali ya dhahabu imechukuliwa na Lomnyaki Yakobo wa Manyara ambaye aliruka urefu wa mita 1 na sentimita 62, medali ya fedha ilikwenda kwa mwanariadha Daniel Kileo wa Manyara abaye aliruka urefu wa mita 1 na sentimita 60, huku medali ya shaba ikichukuliwa na mwanariadha Nguruko Mashaka wa Pwani aliyeruka urefu wa mita 1 na sentimita 58.

Matangazo

  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert (extension) 1 May 28, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert (extension) May 28, 2025
  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • MHE MCHENGERWA AWATAKA MA RC, DC KUONGOZA JOGGING KWENYE MAENEO YAO

    June 14, 2025
  • MANYARA NA MWANZA MABINGWA RIADHA MITA 800 

    June 14, 2025
  • HAKIKISHENI MNAKUWA WABUNIFU  KATIKA KUANDAA MIRADI YA MAENDELEO- ADOLF NDUNGURU 

    June 13, 2025
  • WAVU KWAENDELEA KUNOGA UMITASHUMTA

    June 13, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.