Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Jafo “Huwezi Kutaja Mafanikio Ya Elimu Nchini Bila Wakuu Wa Shule”

Imewekwa tar.: December 11th, 2019

Katika miaka minne ya utekelezaji wa mpango wa Elimu Msingi bila malipo huwezi kutaja mafanikio ya Elimu Nchini bila kuwataja wakuu wa shule ambao ndio chachu ya mafaniko ya haya katika Sekta ya Elimu.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo alipokuwa akifungua kongamano la 14 la umoja wa wakuu wa shule za Sekondari Tanzania linalofanyika kwa siku tatu katika ukumbi wa chuo cha mipango Jijini Dodoma.

“Tangu mpango wa Elimu Msingi bila Malipo uanze Januari, 2016 Serikali imetoa jumla ya shilingi 937,548,685,734 kugharamia Elimu ya watoto wetu na katika Bajeti ya mwaka 2019/20 Serikali imetenga bajeti ya shilingi 288,485,000,000 na mpango huu umefanikisha ongezeko la watoto wanaoandikishwa kuanza darasa la kwanza, idari ya watoto wanaohitimu na hata ufaulu umeongeza kupitia mpango hii” alisema Jafo.

Serikali imepeleka fedha nyingi lakini bado jukumu kubwa lilibaki kwa Wakuu wa shule kuhakikisha kuwa fedha hizo zinatumika ipasavyo kwa mujibu wa maelekezo na kuleta mafanikio chanya katika mpango hakika siwezi kuzungumzia mafaniko ya Elimu bila kutaja mchango wenu mmejituma kikamilifu nawapongeza sana na naomba mzidi kuchapa kazi alisisitiza Jafo.

Wakati huo huo Waziri Jafo aliwataka Wakuu hao wa shule kuhakikisha wanasimamia nidhamu kwa walimu na wanafunzi ili kujenga msingi bora wa wa utoaji na upatikanaji wa Elimu Nchini.

“Nataka mkasimamie Nidhamu mashuleni kuna baadhi ya walimu hawana nidhanu wanawatendea wanafunzi vibaya wanathubutu hata kuwapa wanafunzi ujauzito hili nataka mkalikemee, mkalisimimie na liishe katika katika shule zetu nataka kuona na kusikia walimu wote wana maadili mema na wanakuza ujuzi na ufahamu wa wanafunzi wetu katika njia iliyo bora” alisema Jafo.


Aliongeza kuwa eneo linguine ambavyo nahitaji mkaongeze usimamizi ni utoro mashuleni na hii ni kwa walimu na wanafunzi tabia hii chafu inachangia katika kurudisha nyuma jitihada za utoaji wa Elimu bora Nchini; Unakuta mwalimu hahudhurii shuleni ipasavyo, hafundishi vipindi vyake alivyopangiwa ipasavyo anafundisha vichache sababu muda mwingi hakuwepo shuleni na mwanafunzi anakosa uelewa wa kutosha wa somo husika kutokana na utoro wa mwalimu.

Na upande wa mwanafunzi hafiki shule kwa wakati au anaondoka kabla masomo hayajaisha au huenda hafiki shuleni kwa siku zote zinazotakiwa ni wazi kuwa masomo yatampita na hawezi kuwa sawa na wenzake ambao wameshiriki kikamilifu katika vipindi vyote hivi tabia hizi kwa pande zote nataka mkazikomeshe ziishe kabisa kila mwalimu na mwanafunzi watimize wajibu wao ipasavyo alisisitiza Jafo.

Waziri Jafo alimalizia kwa kuahidi panapo majaaliwa atahakikisha kuwa kikao cha mwaka2020 kinahusisha Wakuu wote wa shule za Msingi na Sekondari za Serikali na binafsi na wote watakutana kwa muda wa siku tatu na yeye atakuwa na siku maalumu ya kuzungumza na walimu wote kwa ujumla wao.

Naye Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia Elimu OR-TAMISEMI Gerald Mweli amesema kuwa lengo la kokangamo hili ni kuwakutanisha wakuu wa shule za Sekondari za Serikali na zisizo za Serikali nchini ili waweze kujifunza, kubadilishana uzoefu na kujadili kwa panoja changamoto wanazokutana nazo katika maeneo ya shule na kuzitafutia ufumbuzi wa pamoja.

“Jukwaa hili ni muhimu sana kwetu kama Serikali kwa kuwa tunapata sehemu ya kutoa maelekezo muhimu ya Elimu kwa Wakuu wa shule yaan hapa ujumbe hauchakachuliwi unamfikia moja kwa moja kwa muhisika hivyo unamfikia mlengwa kama tulivyoukusudia” alisema Mweli.

Naye Rais wa umoja wa wakuu wa shule za Sekondari za Serikali na zisizo za Serikali  Vitalis Kulindwa Shija amesema umoja huo una wajumbe takribani 5,000 na ulianza mwaka 2014 na hili ni kongamano la 14 kufanyika tangu kuanzishwa kwa umoja huo.

“Mpaka sasa walimu ambao wameshafika katika kongamano hili ni zaidi ya 3500 na imekua ni sehemu nzuri kwetu kukutana, kujifunza, kuwasilisha changamoto zetu na kukutana na viongozi wetu ambao imekuwa ni vigumu kukutana nao katika maeneo yetu ya kazi” alisema Shija.

Aida Rais huyo wa TAHOSSA ameishukuru Serikali ya awamu ya tano kwa kuwezesha mpango wa Elimumsingi bila malipo , upatikanaji wa vifaa vya kujifunza na kufundishia, upatikanaji wa posho za madaraka kwa Wakuu wa shule na waratibu wa elimu kata na ukarabati wa miundombinu ya shule.


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert May 12, 2025
  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert May 12, 2025
  • Fursa kwa Wahitimu wa Kidato cha Nne 2024 kubadili Tahasusi na Kozi April 02, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI AJIRA ZA AFYA - TAMISEMI 2025 March 15, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI

    May 23, 2025
  • PJT-MMMAM Yawezesha Uanzishwaji wa Vituo 206 vya Malezi ya Watoto Wadogo

    May 21, 2025
  • SERIKALI KUJENGA DARAJA LINALOUNGANISHA KIJIJI CHA NEGERO – KILINDI

    May 21, 2025
  • MHE. MCHENGERWA ABORESHA TAARIFA ZAKE KWENYE  DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

    May 20, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.