Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Jafo Aonya Halmashauri Ambazo Hazijashiriki Mafunzo ya Kuandaa Maandiko ya Miradi ya Kimkakati

Imewekwa tar.: June 19th, 2019

WAZIRI wa Nchi,Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI), Selemani Jafo ameionya mikoa ya Dodoma,Lindi na Njombe iliyoshindwa kupeleka watendaji wake kuhuduhuria semina ya kuandika miradi ya kimkakati.

Onyo hilo juzi jijini hapa wakati akifungua semina ya siku mbili iliyoshirikisha mamlaka za serikali za mitaa zilizopo Tanzania Bara na sekretarieti za mikoa semina iliyofanyika katika Chuo cha serikali za mitaa Hombolo.

Jafo alisema semina hiyo ni muhimu sana kwao kwa ajili ya kuwajengea uwezo utakaowawezesha kuibua miradi mbalimbali lakini ameshangaa mikoa hiyo kutopeleka watendaji wake.

“Hapa hatuna wawakilishi wa mkoa wa Dodoma,Njombe na Lindi wakati Dodoma mradi mkakati walioupata ni Kondoa peke yake,hakuna Bahi,Chamwino wala Jiji,Njombe nao hakuna mradi mkakati walioupata cha kushangaza kwenye semina hii hawapo,"alisema.

Alieleza Lindi wana mradi mkakati katika halmashauri ya Liwale na Ruangwa lakini bado hawajahudhuria semina hiyo na Mtwara halmashauri wana mradi katika halmashauri moja lakini Nanyumbu,Masasi,Newala,Tandahimba na Nanyamba hakuna mradi wowote walioupata lakini pia hawajahudhuria.

"Hii Nanyamba ni halmashauri ya mwisho katika ukusanyaji wa mapato nawaagiza  wahakikishe awamu ya pili ya semina hiyo wanakuwepo,"alisema.

Jafo alisema mpaka sasa kiasi cha Sh.Bilioni 268.37 zimeshatolewa na serikali kwa ajili ya kugharamia miradi 38 na hapo kuna halmashauri hazijaguswa na miradi hiyo kutokana na maandiko yao kutokuwa na sifa za kuweza kupata fedha na hali yao ya uchumi bado ipo mbaya sana.

“Leo hii unapoona halmashauri zimepewa nafasi hiyo lakini still zimelala kuanzia wilayani hadi mkoani hapo kuna matatizo,”alisema Waziri Jafo.

Alibainisha kuwa ni lazima kubadili mbinu za ukusanyaji wa mapato kwa kuwa serikali lengo lake kubwa ni kuhakikisha inaondoa mzigo kwa watu wanyonge na ili hizo kodi na tozo zenye kero ziweze kuondoka ni lazima halmashauri iweze kupata mapato kwa njia nyingine mbadala.

“Jiji la Dodoma hawapo hapa,sijui kiburi cha  kukusanya mapato mengi ndio maana hawataki kuja hapa na fedha hizo ujue ni fedha za kwetu tumeandikia miradi sisi ya TSP  wala hawajaandika ya kwao,nilitamani waje hapa wajifunze, leo hii Dodoma mpaka mwezi huu wameshakusanya Sh.Bilioni 60 wangekuja hapa wangepata maarifa mengine zaidi,"alisema.

Alizitaka halmashauri kutekeleza miradi inayopelekwa kwao bila ya kusua sua kwa kuingiza maslahi yao hasa katika ajenda ya manunuzi ambapo kila mtu anaenda na makaratasi yake ikiwa na mkadarasi wake hali inayofanya miradi hiyo kutoendelea mbele .

Awali, Mkurugenzi Msaidizi Idara za Serikali za Mitaa, Angelista Kihaga alisema miradi ya kimkakati ni utaratibu mpya wa serikali wa kutoa fedha za maendeleo kwa mamlaka za serikali za mitaa.

Naye, Kaimu Mkuu wa Chuo cha Hombolo Dk. Michael Msendekwa alisema mafunzo hayo yametokana na tafiti zilizofanywa na chuo hicho kuonyesha kuna changamoto katika maandishi ya miradi katika mamlaka za serikali za mitaa.

Alisema mafunzo hayo yanatolewa kwa ushirikiano baina ya TAMISEMI na Wizara ya Fedha lengo likiwa ni kuelekezana na kusaidiana kutatua changamoto hiyo.


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert May 12, 2025
  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert May 12, 2025
  • Fursa kwa Wahitimu wa Kidato cha Nne 2024 kubadili Tahasusi na Kozi April 02, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI AJIRA ZA AFYA - TAMISEMI 2025 March 15, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI

    May 23, 2025
  • PJT-MMMAM Yawezesha Uanzishwaji wa Vituo 206 vya Malezi ya Watoto Wadogo

    May 21, 2025
  • SERIKALI KUJENGA DARAJA LINALOUNGANISHA KIJIJI CHA NEGERO – KILINDI

    May 21, 2025
  • MHE. MCHENGERWA ABORESHA TAARIFA ZAKE KWENYE  DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

    May 20, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.