Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Halmashauri zatakiwa kusimamia kwa karibu miradi ya ujenzi inayotekelezwa kupitia Force Account

Imewekwa tar.: February 13th, 2019

Na Mathew Kwembe, Morogoro,

Serikali imewataka viongozi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa kuhakikisha kuwa wanasimamia kwa karibu utekelezaji wa ujenzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo ili kuleta matokeo yanayotarajiwa kwa umma.

Wito huo umetolewa leo na Mkurugenzi wa Serikali za Mitaa kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Dkt Charles Mhina wakati akizungumza na Maafisa Manunuzi kutoka halmashauri 118 wanaoshiriki mafunzo kuhusu marekebisho ya sheria ya ununuzi wa umma  na kanuni zake na mfumo wa utoaji taarifa za manunuzi (PMIS) yanayofanyika mkoani Morogoro.

Dkt Mhina aliwaambia Maafisa Manunuzi hao kuwa halmashauri haiwezi kutekeleza miradi ya maendeleo kwa kutumia force account bila ya kuwatumia wataalamu wake kwani wana jukumu kubwa la kusimamia na kutoa ushauri wa kitaalamu katika utekelezaji wa mradi.

Aliongeza kuwa kwa mujibu wa mwongozo uliotolewa na serikali karibu kila kamati inayohusika katika utekelezaji mradi iwe kamati ya ujenzi, manunuzi, au mapokezi ya vifaa ni lazima iwe na mtaalamu wa halmashauri.

Hivyo Dkt Mhina alisisitiza kuwa endapo kamati hizo zitatekeleza majukumu yake ipasavyo, mfumo wa force account utakuwa na tija kwa halmashauri kwani utawezesha miradi mingi ya ujenzi kukamilika mapema na kuonyesha thamani halisi ya fedha zilizotumika kwenye ujenzi wa miradi hiyo.

Aliongeza kuwa mfumo wa force account unahitaji uongozi wote wa halmashauri uwajibike kwa pamoja katika utekelezaji wa miradi ambapo pia watawajibika kuhakikisha kuwa ujenzi husika unazingatia vigezo vya ubora ili viendane na thamani halisi ya fedha zilizotolewa.

"Force account lengo lake ni kupunguza gharama za ujenzi, hivyo liability ya ubora inahamia kwa mmiliki ambapo halmashauri kupitia kwa mhandisi wa ujenzi anabeba jukumu la kutoa ushauri wa kitaalamu na kuhakikisha kazi inakuwa bora kwa vigezo vilivyowekwa badala ya jukumu hilo kumtwisha mkandarasi,"alieleza Dkt Mhina.

Alisema mfumo huu ni mzuri kwani mahali ambapo mkandarasi angedai alipwe shilingi milioni mia nane zaidi ya gharama halisi za ujenzi kupitia force account fedha hizo zinaokolewa kwani jukumu la usimamizi na mwajibikaji wa ujenzi ni Mhandisi wa ujenzi wa Halmashauri.

Dkt Mhina aliongeza kuwa hata Ofisi ya Rais TAMISEMI inajenga jengo la ghorofa makao makuu Dodoma kwa kutumia mfumo wa Force Account ambapo ili kupata matokeo yanayotarajiwa, viongozi wote wa wizara akiwemo Waziri wa Nchi wamejipanga kuhakikisha kuwa wanasimamia kwa ukaribu ujenzi wa jengo hilo ili likamilike kwa wakati na ubora unaotakiwa.

" Wakuu wote wa Idara wa Ofisi ya Rais TAMISEMI tumepangiana zamu za kuwa site (eneo la ujenzi) pale Mtumba na tunahakikisha kuwa tunasimamia kamati zote za ujenzi kuanzia ile ya mapokezi ya vifaa, manunuzi, na ya ujenzi ili tuweze kukamilisha ujenzi kwa wakati," alisisitiza.

Kwa mujibu wa Dkt. Mhina, Viongozi wa Halmashauri wanapaswa kujipanga vizuri kutekeleza miradi ya ujenzi wa vituo vya afya, hospitali za wilaya na miradi mingine ya maendeleo inayotekelezwa katika halmashauri zao kwa kuisimamia kwa ukaribu.

Mafunzo ya siku nne ya marekebisho ya sheria ya ununuzi wa umma na kanuni zake yanaendeshwa na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa kupitia Programu ya Maboresho ya Fedha za Umma Awamu ya V (PFRMP V) kwa kushirikiana na Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA).



Matangazo

  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert (extension) 1 May 28, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert (extension) May 28, 2025
  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • RC CHALAMILA ATAKA MACHINGA KARIAKOO KUFUNGUA NJIA

    May 30, 2025
  • Wamiliki wa vituo vya kulelea watoto wadogo mchana watakiwa kuzingatia miongozo na kanuni zilizopo.

    May 29, 2025
  • Mhe. Katimba awapokea Wabunge wa Zambia waliokuja kujifunza kuhusu Usimamizi na Uendeshaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa Tanzania Bara

    May 28, 2025
  • Mtwale Atoa Mwongozo kwa Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.