Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

FANYENI KAZI KWA KUZINGATIA MAADILI YA UTUMISHI WA UMMA

Imewekwa tar.: June 21st, 2022

Asila Twaha, OR TAMISEMI

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Innocent Bashungwa amewataka watumishi wa Ofisi ya Rais, TAMISEMI kufanya kazi kwa kuzingatia  maadili ya utumishi wa umma kwa kuwa  Wizara hiyo imabeba taswira  ya nchi.

Waziri Bashungwa amesema hayo Juni 21, 2022 kwenye Kikao kazi   na Watumishi wa Ofisi ya Rais, TAMISEMI ikiwa ni Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma ambapo kila mwaka huadhimishwa kuanzia tarehe 16-23 Juni.

Amewataka watumishi hao kuhakikisha wanatunza  siri za Serikali na kufuata  sheria, kanuni na taratibu za utumishi wa Umma kwa kuwa   TAMISEMI imebeba maisha ya watanzania.

Waziri Bashungwa ameendelea kwa kuwataka watumishi hao pia kufanyakazi kwa weledi na  kujitoa katika kuwahudumia wananchi na kutojihusisha na rushwa  katika utekelezaji wa majukumu yao.

“TAMISEMI tuna jukumu kubwa la kutoa huduma kwa wananchi niwatake watumishi suala la utoaji wa huduma ni ibada tusimamie katika utendaji wa haki pasina kujihusisha na rushwa Wizara hii ni kubwa ujue ukiwa humu unatakiwa ufuate maadili ya utumishi wa Umma na imani tuwe nayo sababu sisi tunatoa huduma moja kwa moja kwa wananchi wetu” amesema Waziri Bashungwa

Amesema kuwa baadhi ya  vitendo vinatokea ambavyo  ni kinyume na maadili ya utumishi wa Umma ambapo baadhi ya watu wanaharibu taswira na picha ya Ofisi hii kwa kushiriki kwenye vitendo ikiwemo kugushi barua za uhamisho  wa watumishi  hivyo, amemuelekeza  Katibu Mkuu Prof. Riziki Shemdoe  kulishughulikia kwa haraka suala hilo.

“Ninaelekeza wale wote ambao waliopata barua za uhamisho ambazo tumeshafanya uchunguzi na  sio halali warudishwe kwenye vituo vyao vya awali na kama kuna stahiki zozote walipatiwa ambapo ni fedha za Serikali zirudishwa na wachukuliwe hatua” amesisitiza Waziri Bashungwa

Kwa upande wa  Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. David Silinde  amewashukuru watumishi hao kwa kuendelea kutoa ushirikiano kwa viongozi hao  kuweza kutekeleza majukumu yao ikiwa wao ni moja kwa moja wanawajibika na wananchi amewataka  kuendelea kuwahudumia wananchi kwani wana imani na Wizara hiyo.

“Imani ya wananchi ni pamoja na kuwa na imani ya Rais wetu Mhe. Samia Suluhu Hassan na sisi TAMISEMI tunawajibika moja kwa moja kwa wananchi nitoe rai kwa  watumishi  wote kufanyakazi kwa weledi kwa kuwa  tumeaminiwa hivyo tuaminike” amesema Mhe. Silinde

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais  Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Prof. Riziki Shemdoe amemuhakikishia Mhe. Waziri kuwa, maelekezo yote aliyoyatoa anaenda kuyasimamia ili kuendelea kuboresha utoaji wa huduma amesema wao kama watendaji watahakikisha wanaendelea kushirikiana na viongozi wa ngazi zote za Wizara hiyo ili kuendelea kuwahudumia wananchi

Akiongea kwa niaba ya watumishi Bi. Namsifu Maduhu(Afisa Utumishi Mkuu)  ameushukuru uongozi na kuahidi kutekeleza yale yote yaliyoagizwa   kwa lengo la kuhakikisha wanatoa huduma bora kwa wananchi.



Matangazo

  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert (extension) 1 May 28, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert (extension) May 28, 2025
  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • GEITA YAENDELEZA UBABE KIKAPU WASICHANA

    June 12, 2025
  • MWANZA YAIADHIBU PWANI SOKA MAALUMU WASICHANA

    June 12, 2025
  • SANAA ZA MAONESHO ZAANZA RASMI UMITASHUMTA 2025 MKOANI IRINGA

    June 11, 2025
  • KILIMANJARO, RUVUMA NA NJOMBE MABINGWA RIADHA MAALUMU UMITASHUMTA 2025

    June 11, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.