• Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Machapisho
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
    • Ramani za mradi wa BOOST
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
    • Green and Smart Cities
    • Miongozo ya Kilimo
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Michoro ya Ujenzi
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)

Dkt. Gwajima, Aapa Moto wa Dawa Hakuna kupoa, atuma Salamu mikoani wajipange.

Imewekwa tar.: October 31st, 2019

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Dkt. Dorothy Gwajima, ameapa kwamba moto dhidi ya wabadhilifu wa dawa aliouwasha katika zoezi la ufuatiliaji hautazimika wala kupoa, huku akiwaomba wananchi kutoa ushirikiano wa karibu kwa kuwafichua watu/mtu yeyote atakayebainika kuhujumu jitihada za serikali.

Gwajima ametoa kauli hiyo ikiwa ni mara ya pili kurudia wito huo mbele ya Makatibu Tawala wa Mikoa, wataalamu Wafamasia kutoka mikoa 13 na wadau wa maendeleo Global Supply chain, waliokutana mjini Dodoma kwenye ukumbi wa Mikutano wa OR-TAMISEMI katika kikao kazi cha tathmini ya mbinu mpya ya kuimarisha takwimu za bidhaa za afya.

Akizungumza katika kikao hicho Gwajima amesema, vita hiyo wataweza kuishinda kwa kuunganisha nguvu na wananchi kutoka maeneo yote nchini.

“Niwaombe wanachi kuwa mstari wa mbele kufichua wale wote mtakaowabaini wanahujumu suala la dawa kwani vita hiyo siyo ya mtu mmoja mmoja wala serikali peke yake bali ni ya jamii nzima” alisema Gwajima na kuongeza kuwa, “wapo watu wanaotambua nani ni adui wao katika vita hivi ndiyo maana jana nimeona kwenye Jamiiforum wakinipa pole na kunipongeza, lakini nasema lazima tutembee na wananchi katika hili.” alisisitiza kiongozi huyo.

Gwajima alisema inashangaza unafika kwenye kituo ambacho kina wafamasia wasiopungua sita (6) lakini unakuta kitabu cha kupokelea dawa (ledger) hakijahuishwa kwa zaidi ya miezi 5, hii ni hali ya hatari sana, suala hilo halivumiki na wala hawezi kukubaliana nalo.

“Viongozi wangu Makatibu Tawala, mnaelewa tunatekeleza ilani ya Chama Cha Mapinduzi ya 2015-2020, hivyo fuatilieni hili hadi kwenye stoo za kutunzia dawa lakini pia ombeni taarifa na ingieni kwenye mikutano yao muone kile wanachokijadili maana humo hakuna zuio lolote kwa kuwa taarifa zinazojadiliwa humo sio siri za mgonjwa, sasa wasije wakajifichia kwenye mwamvuli wa taarifa za kitabibu kwa kuwahadaa eti siri za Mgonjwa?” Alihoji na alikemea   

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Global Supply Chain Tukay Mavere aliwataka wachumi, watawala wa fedha pamoja na watumiaji wa mfumo wa eLMIS kukaa pamoja na kuja na mbinu mbadala za kudhibiti hali ya dawa na upatikanaji wake na kutoa mrejesho wa kile ambacho serikali imewekeza.

“Lengo la mfumo huu tunataka tuwe tunachukua jambo, tunalichakata na kisha tunalitolea majibu kwa wakati sio kungoja muda uende, aidha hii inakuwa ni zoezi endelevu katika utendaji wa siku kwa siku kama mfumo ulivyo, hivyo tumeitana ili tuwe na uwelewa wa pamoja juu ya hili tunalokusudia kulifanikisha” alisema Mavere.

Kwa upande wao washiriki wa warsha hiyo wameipongeza serikali na wadau kuja na mfumo huo, kwani ni matumaini yao utakuwa suluhu ya yale wanayofanyia kazi kila siku.

“Kama Naibu Katibu Mkuu alivyosema, mfumo huu utasaidia kuondoa ziada ya dawa inayosababisha upotevu wa pesa kutokana na kuchina kwa Bidhaa zilizoingizwa bila takwimu sahihi, vema sasa kila mmoja wetu akitoka hapa awe mstari wa mbele katika kuutumia mfumo kwenye utendaji wake.” alisema, Msalika Makungu Katibu Tawala wa Mkoa wa Tabora.

Katika kikao hicho cha siku mbili pamoja na mambo mengine yatakayojitokeza, wataalam watajifunza kupata takwimu sahihi kwa ajili ya kufanyia maoteo kwa kuwa mfumo unaanzia chini kwenye huduma kwenda juu, hivyo itakuwa ni fursa ya kuwajengea uwezo timu za uratibu wa afya za Mikoa na Wilaya, kupata taarifa sahihi na kufanya ugawaji wa dawa kulingana na mahitaji na kuondokana na tatizo la dawa kwenye maeneo yenye dawa nyingi.

Mambo mengine ni kufanya bajeti kulingana na rasilimali zilizopo lakini pia kuwezesha kufanya usimamizi kwa njia ya mtandao Online Supervision. 

Katika kikao hicho, Wataalamu hao walikumbushwa juu ya viapo vyao kwa kuongozwa na kiapo mbele ya Naibu Katibu Mkuu huku wakiwa wamenyoosha mikono juu na kuapa kwamba, watakuwa chachu ya mapambano dhidi ya ubadhilifu wa dawa na endapo wakishindwa basi wawe tayari kuachia nyadhifa zao hata kwa kutuma ujumbe wa maandishi kwenye mtandao wa kundi sogozi (WhatsApp) kuhusu  kuachia madaraka waliyonayo.

Na. Atley Kuni- TAMISEMI


Matangazo

  • Orodha ya Majina ya Waliopata Ajira Kada za Afya na Elimu Juni 2023 June 05, 2023
  • TANGAZO LA AJIRA - UALIMU NA AFYA - TAMISEMI APRILI, 2023 April 12, 2023
  • Orodha ya waliopata vibali vya Uhamisho Septemba - Disemba 2022 (OR - TAMISEMI) January 21, 2023
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kidato cha Kwanza Waliorudia Mtihani January 15, 2023
  • Matumizi ya Lugha ya Kiswahili na Kingereza January 14, 2023
  • Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Kwanza 2023 December 14, 2022
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • NDEJEMBI HAJARIDHISHWA USIMAMUZI WA UJENZI WA VYUMBA VYA MADARASA CHEMBA - DODOMA

    May 31, 2023
  • MIKATABA YA UTEKELEZAJI MRADI WA UENDELEZAJI WA JIJI LA DAR ES SALAAM DMDP 2 YASAINIWA

    May 30, 2023
  • DKT. MPANGO AFUNGUA MKUTANO WA ALAT

    May 30, 2023
  • WANANCHI KIJIJI CHA MAJALILA WAISHUKURU SERIKALI KUWAJENGEA SHULE

    May 23, 2023
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.