• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
  • Kuhusu Sisi
    • Local Government History
    • Kuhusu Wizara
      • Directories
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi na Programu
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Speech
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Machapisho ya Halmashauri
  • Machapisho
    • Taarifa Mbalimbali
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
    • Green and Smart Cities
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Michoro ya Ujenzi
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali

Dar yatolewa na Mtwara robo fainali ya soka UMISSETA

Imewekwa tar.: June 30th, 2021

Na Mathew Kwembe, Mtwara

Kipigo cha magoli 5-4 ilichokipata timu ya soka ya wavulana ya mkoa wa Dar es salaam dhidi ya wenyeji Mtwarakwa njia ya mikwaju ya penati kimeiondoa timu hiyo katika kinyang’anyiro cha kuwania kombe la UMISSETA mwaka huu.

Licha ya kupoteza mchezo huo, hadi kipindi cha kwanza kinamalizika Dar es salaam walikuwa wakiongoza kwa magoli 2-0, lakini hali ya mchezo ilibadilika kipindi cha pili na kupelekea kusawazisha magoli hayo.

Hadi dakika 90 za mchezo kumalizika timu hizo zilifungana magoli 2-2, huku magoli ya Dar yakifungwa na wachezaji Juma Ahmad na Ibrahim Hussein kutoka sekondari ya Makongo huku magoli ya Mtwara yakifungwa na Ikram saidi na Abdul Mussa.

Katika mikwaju ya penati Mtwara walishinda 5-4, huku penati ya tano ikiwekwa wavuni na mchezaji AbdulAziz Said na kuibua nderemo na vifijo kwa wakazi wa Mtwara na viunga vyake.

Mara baada ya mchezo huo kocha timu ya soka ya mkoa wa Dar es salaam Abel Mtweve na viongozi wake iliwabidi kufanya kazi ya ziada kuwabembeleza wachezaji wa Dar waliokuwa wakibubujikwa na machozi kutokana na kutoamini kutolewa kwenye mashindano ya UMISSETA mwaka huu.  

Naye Kocha wa Mtwara Mwalimu Hamis alisema wachezaji wake walishinda mchezo huo kutokana na wachezaji wake kucheza kwa morali na kujiamini hasa baada ya kuwa nyuma kwa magoli 2-0 katika kipindi cha kwanza aliwaambia hawana cha kupoteza wakikaba sana na kupambana kwa nguvu zao zote.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa kamati ya kitaifa ya kusimamia mchezo wa mpira wa miguu wa UMISSETA Israel Nkongo alisema kuwa ushindani na msisimko katika mchezo huo umeongezeka mwaka huu.

Nkongo ambaye ni refarii wa kimataifa alisema kuwa UMISSETA ya mwaka huu imeibua vipaji vingi vya wachezaji wanaofaa kucheza ligi kuu ya Tanzania lakini ameshangazwa kutoona wawakilishi wa vilabu vikubwa kuja kuona vipaji vya usakataji kabumbu.

Mwenyekiti huyo wa kamati ya soka ya UMISSETA amewataka viongozi wa vilabu vikubwa kuyafuatilia mashindano ya UMITASHUMTA na UMISSETA kwani ndiyo chimbuko la wachezaji wote wakubwa waliowahi kuvuma na wanaocheza ligi kuu hivi sasa.

Aliwataka viongozi hao kuondokana na kasumba ya kila mwaka wakati wa usajili kukimbilia nje ya nchi kusaka vipaji vya soka ilhali wachezaji wenye vipaji wapo katika mashindano ya UMITASHUMTA na UMISSETA.

 Katika michezo ya nusu fainali ya soka itawakutanisha wenyeji Mtwara watakaochuana na Dodoma na mabingwa watetezi wa kombe hilo Geita watachuana na timu ya soka ya Pemba leo katika Uwanja wa Chuo cha Ualimu Mtwara

Matangazo

  • MAJINA YA WALIOPATA AJIRA KADA ZA AFYA NA UALIMU June 26, 2022
  • ORODHA YA WAKUU WA KITENGO CHA FEDHA YENYE MABADILIKO 5-5-2022 May 06, 2022
  • Kazi za muda za makarani na wasimamizi wa Sensa 2022 May 05, 2022
  • MUDA WA NYONGEZA MAOMBI YA AJIRA ZA TAMISEMI 2022 May 04, 2022
  • Taarifa ya Kitengo Manunuzi na Ugavi, April 2022 April 04, 2022
  • Safeguard Documents for TACTIC Project March 30, 2022
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • BASHUNGWA AWAAGIZA VIONGOZI WA MIKOA NA MAMLAKA ZA SERIKALI ZA MITAA KUTANGAZA MIRADI YA MAENDELEO.

    July 02, 2022
  • Mameya, Wenyeviti wa Halmashuri watoa kongole kwa Rais Samia kuibadili Dodoma

    June 30, 2022
  • MAMEYA, WENYEVITI WA HALMASHAURI SIMAMIENI UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO- PROF. SHEMDOE

    June 30, 2022
  • WAZIRI MKUU MAJALIWA AWAFUNDA MAMEYA, WENYEVITI WA HALMASHAURI

    June 27, 2022
  • Angalia zote

Video

Taarifa ya Ukusanyaji wa Mapato ya Halmashauri, kipindi cha robo ya pili ya mwaka wa fedha 2021/22
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tume ya Ajira Tanzania
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.