Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Dar yatolewa na Mtwara robo fainali ya soka UMISSETA

Imewekwa tar.: June 30th, 2021

Na Mathew Kwembe, Mtwara

Kipigo cha magoli 5-4 ilichokipata timu ya soka ya wavulana ya mkoa wa Dar es salaam dhidi ya wenyeji Mtwarakwa njia ya mikwaju ya penati kimeiondoa timu hiyo katika kinyang’anyiro cha kuwania kombe la UMISSETA mwaka huu.

Licha ya kupoteza mchezo huo, hadi kipindi cha kwanza kinamalizika Dar es salaam walikuwa wakiongoza kwa magoli 2-0, lakini hali ya mchezo ilibadilika kipindi cha pili na kupelekea kusawazisha magoli hayo.

Hadi dakika 90 za mchezo kumalizika timu hizo zilifungana magoli 2-2, huku magoli ya Dar yakifungwa na wachezaji Juma Ahmad na Ibrahim Hussein kutoka sekondari ya Makongo huku magoli ya Mtwara yakifungwa na Ikram saidi na Abdul Mussa.

Katika mikwaju ya penati Mtwara walishinda 5-4, huku penati ya tano ikiwekwa wavuni na mchezaji AbdulAziz Said na kuibua nderemo na vifijo kwa wakazi wa Mtwara na viunga vyake.

Mara baada ya mchezo huo kocha timu ya soka ya mkoa wa Dar es salaam Abel Mtweve na viongozi wake iliwabidi kufanya kazi ya ziada kuwabembeleza wachezaji wa Dar waliokuwa wakibubujikwa na machozi kutokana na kutoamini kutolewa kwenye mashindano ya UMISSETA mwaka huu.  

Naye Kocha wa Mtwara Mwalimu Hamis alisema wachezaji wake walishinda mchezo huo kutokana na wachezaji wake kucheza kwa morali na kujiamini hasa baada ya kuwa nyuma kwa magoli 2-0 katika kipindi cha kwanza aliwaambia hawana cha kupoteza wakikaba sana na kupambana kwa nguvu zao zote.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa kamati ya kitaifa ya kusimamia mchezo wa mpira wa miguu wa UMISSETA Israel Nkongo alisema kuwa ushindani na msisimko katika mchezo huo umeongezeka mwaka huu.

Nkongo ambaye ni refarii wa kimataifa alisema kuwa UMISSETA ya mwaka huu imeibua vipaji vingi vya wachezaji wanaofaa kucheza ligi kuu ya Tanzania lakini ameshangazwa kutoona wawakilishi wa vilabu vikubwa kuja kuona vipaji vya usakataji kabumbu.

Mwenyekiti huyo wa kamati ya soka ya UMISSETA amewataka viongozi wa vilabu vikubwa kuyafuatilia mashindano ya UMITASHUMTA na UMISSETA kwani ndiyo chimbuko la wachezaji wote wakubwa waliowahi kuvuma na wanaocheza ligi kuu hivi sasa.

Aliwataka viongozi hao kuondokana na kasumba ya kila mwaka wakati wa usajili kukimbilia nje ya nchi kusaka vipaji vya soka ilhali wachezaji wenye vipaji wapo katika mashindano ya UMITASHUMTA na UMISSETA.

 Katika michezo ya nusu fainali ya soka itawakutanisha wenyeji Mtwara watakaochuana na Dodoma na mabingwa watetezi wa kombe hilo Geita watachuana na timu ya soka ya Pemba leo katika Uwanja wa Chuo cha Ualimu Mtwara

Matangazo

  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert (extension) 1 May 28, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert (extension) May 28, 2025
  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • MHE MCHENGERWA AWATAKA MA RC, DC KUONGOZA JOGGING KWENYE MAENEO YAO

    June 14, 2025
  • MANYARA NA MWANZA MABINGWA RIADHA MITA 800 

    June 14, 2025
  • HAKIKISHENI MNAKUWA WABUNIFU  KATIKA KUANDAA MIRADI YA MAENDELEO- ADOLF NDUNGURU 

    June 13, 2025
  • WAVU KWAENDELEA KUNOGA UMITASHUMTA

    June 13, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.