logo

TAMISEMI

Students

AN
Angela Msimbilaangela.msimbila@tamisemi.go.tz

Waziri mchengerwa: muswada wa makao makuu dodoma uingie bungeni haraka

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Mohammed Mchengerwa, amemuelekeza Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo kuhakikisha Muswada wa Sheria ya Usimamizi na Uendelezaji wa Makao Makuu Dodoma unawasilishwa bungeni kabla ya kuvunjwa kwa Bunge la 12 mwaka huu.

Mhe. Mchengerwa ametoa agizo hilo leo, Februari 6, 2025 katika hafla ya utiaji saini wa mkataba wa ujenzi wa Soko Kuu la Majengo na vituo vya daladala jijini Dodoma kupitia mradi wa  uboreshaji miundombinu ya Miji (TACTIC) awamu ya pili unaotekelezwa chini ya Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA).

Amesema Dodoma haiwezi kuwa Makao Makuu kwa matamko pekee, bali ni lazima kuwe na sheria rasmi itakayohakikisha hadhi yake inalindwa kwa vizazi vijavyo.

Amesema "Sheria hii iharakishwe kama zinavyoharakishwa sheria nyingine. Hatuwezi kusubiri tena. Tutamuomba Mheshimiwa Rais kwa hati ya dharura ili iwasilishwe bungeni kabla ya kuvunjwa kwa Bunge hili."

Comments

Please sign in to leave a comment.

Matangazo Muhimu

Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.

Habari na Matukio

Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.

Cookie

We use cookies to enhance your browsing experience, provide personalized content, and analyze our traffic. By clicking "Accept All Cookies", you agree to the storing of cookies on your device to improve site navigation, analyze site usage, and assist in our marketing efforts. To learn more about how we use cookies and to manage your preferences, please visit our Cookie Policy.
National Election Commission Logo

Uchaguzi 2025

Kujiandikisha Kuwa Mpiga Kura ni Msingi wa Uchaguzi Bora