
Waziri mchengerwa akutana na kampuni iliyoonesha nia kulifanya jiji la dar kuwa la kisasa
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI Mhe. Mohamed Mchengerwa amekutana na wawakilishi wa Kampuni ya Straling Holding ya Abu Dhabi na kujadili namna bora ya ujenzi wa mji mpya wa kisasa katika Jiji la Dar es Salaam.
Waziri Mchengerwa amekutana na Kampuni ya Straling Holding leo tarehe 14.02.2025 kwenye ukumbi TAMISEMI jijini Dodoma ambao wameonesha nia ya kuwekeza kwenye ujenzi wa miundombinu ya barabara, madaraja, elimu, afya, bandari, umeme wa maji, reli, mifumo ya umwagiliaji, madini na viwanda nchini.
Mhe. Mchengerwa amefanya kikao kazi na wawekezaji hao ili kuwa na uelewa wa pamoja juu ya shughuli wanazozifanya, ili kuona kama kuna haja ya kushirikiana nao katika ujenzi wa mji mpya wa kisasa katika jiji la Dar es Salaam kwa kuzingatia maslahi mapana ya taifa
Comments
Please sign in to leave a comment.
Matangazo Muhimu
Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.
Tangazo la kuitwa kazini ajira za TMCHIP 2025
Mpango Mkakati wa Usimamizi wa Takwimu wa Ofisi ya Rais TAMISEMI - 2024/25 -2028/29
Kanuni za Uchaguzi wa Mwenyekiti wa Kitongoji 2024
Kanuni za Uchaguzi wa mwaka 2024
Tangazo la Uchaguzi

