logo

TAMISEMI

Students

FR
Fred Kibanofred.kibano@tamisemi.go.tz

Wakurugenzi wa halmashauri waelekezwa kuwasilisha majina ya watumishi wanaodai malimbikizo

OR-TAMISEMI

Naibu Waziri Ofisi ya Rais – TAMISEMI Mhe. Zainab Katimba amewaelekeza wakurugenzi wa Mamlaka za serikali za mitaa kutengeneza mchanganuo na kubaini watumishi wangapi wanadai malimbikizo ya mishahara na yasiyo yamishahara na kuyawasilisha Utumishi kuhakikiwa na kupekwa hazina kwaajili ya malipo.

Ameyatoa maelekezo hayo bungeni Dodoma wakati akijibu swali la Mhe. Bonnah Kamoli mbunge wa Segerea kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais – TAMISEMI Mhe. Mohamed Mchengerwa, aliyetaka kujua serikali inampango gani wa kulipa malimbikizo ya mishahara na marupurupu ya walimu.

Akijibu hilo Mhe. Katimba amesema “Naomba nitoe msisitizo huo na jana kwenye bajeti ya wizara ya utumishi maelekezo hayo yalitolewa na wizara hiyo na mpaka itakapo fika tarehe 31 Mei wakurugenzi wote wawe wamewasilisha majina hayo ya watumishi hao ambao wanadai malipo yao” Amesema

Aidha, akijibu kuhusu mazingira bora ya walimu Mhe. Katimba amesema serikali inaendelea kujenga nyumba za walimu ili walimu wapate mazingira mazuri ya kuishi na kufanyakazi kwa ufanisi.

Comments

Please sign in to leave a comment.

Matangazo Muhimu

Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.

Habari na Matukio

Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.

Cookie

We use cookies to enhance your browsing experience, provide personalized content, and analyze our traffic. By clicking "Accept All Cookies", you agree to the storing of cookies on your device to improve site navigation, analyze site usage, and assist in our marketing efforts. To learn more about how we use cookies and to manage your preferences, please visit our Cookie Policy.
National Election Commission Logo

Uchaguzi 2025

Kura yako haki yako jitokeze kupiga kura