
Wagonjwa 6,847 watibiwa hospitali ya wilaya Handeni
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Mohamed Mchengerwa amesema wagonjwa wapatao 6,846 wamepata huduma za Afya Katika Hospitali ya Wilaya ya Handeni tangu ilipokamilika na kuanza kutoa huduma.
Waziri Mchengerwa ameyasema hayo wakati wa uzinduzi wa Hospitali hiyo iliyozinduliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa katika siku ya kwanza ya ziara yake mkoani Tanga.
Amesema ujenzi wa hospitali hiyo umegharimu jumla ya shilingi Bilioni 7.3 ambapo Serikali imetoa kiasi cha shilingi Bilioni 4.3 na wadau wa Islamic Help wametoa kiasi cha shilingi Bilioni 3.
Amesem mpaka sasa jumla ya majengo yaliyokamilika ni 15 amesema Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Mkoani Tanga hadi sasa imeshapokea wajawazito 900 na kati yao 300 walijifungua kwa njia ya upasuaji ndani ya miaka mitatu(3).
Rais Samia amefanya uzinduzi wa hospitali hiyo akiwa katika ziara mkoani Tanga ambayo ameanza leo Februari 23, 2025 hadi Machi 1, 2025 kwa lengo la kukagua na kuzindua miradi mbaliambali iliyotolewa fedha na Serikali.
Comments
Please sign in to leave a comment.
Matangazo Muhimu
Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.
ADDITIONAL BEST INDICATORS 2025
TANGAZO LA KUITWA KAZINI NAFASI ZA KUJITOLEA SHULE ZA MSINGI KADA YA ELIMU MRADI WA GPE - TSP
ORODHA YA WALIMU WALIOCHAGULIWA NAFASI ZA KUJITOLEA SHULE ZA MSINGI MRADI WA GPE TSP
BASIC EDUCATION STATISTICS 2025
TANGAZO LA KUITWA KAZINI AJIRA YA MKATABA PROGRAMU YA TIMCHIP
Habari na Matukio
Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.




