logo

TAMISEMI

Students

FR
Fred Kibanofred.kibano@tamisemi.go.tz

WAGANGA WAKUU WA MIKOA HAKIKISHENI HOSPITALI ZA WILAYA ZINALEA VITUO VYA AFYA – Prof. NAGU  

OR-TAMISEMI

 

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI anayeshughulikia afya Prof. Tumaini Nagu amewaelekeza Waganga Wakuu wa Mikoa (RMO`S) Kuhakikisha hospitali zote za Wilaya nchini zinalea vituo vilivyopo chini yao ili kufanikisha upatikani wa huduma bora za afya kwenye vituo vyote vya ngazi ya afya Msingi.

Prof. Nagu ametoa maelekezo hayo wakati wa ziara ya usimamizi shirikishi katika Hospitali ya Wilaya ya Mkuranga, mkoani Pwani yenye lengo la kuangalia upatikanaji wa huduma za Afya, Lishe na Ustawi wa jamii katika Mkoa huo.

“Waganga Wakuu wa Mikoa wote hakikisheni huduma bora zinazotolewa katika hospitali za Wilaya, vivyo hivyo hospitali hizo zilee vituo vya afya vilivyopo chini yake navyo viweze kutoa huduma bora na vituo vya afya vitalea zahanati za maeneo husika” amesisitiza Prof. Nagu. 

Aidha, Prof. Nagu amewapongeza watumishi wa hospitali ya Wilaya ya Mkuranga kwa uhamasishaji mkubwa kwa wananchi kushiriki katika uchangia mkubwa wa damu na kufanya kuwe na hazina ya kutosha ya damu.

“Tumeona kuna damu nyingi kwenye majokofu yenu ya kuhifadhia damu na kuna utunzaji mzuri, pia katika maabara yenu kumekuwa na mwitikio mkubwa wa wananchi kuchangia damu, hii imetokana na elimu ambayo mmekuwa mkiitoa kwa wananchi” alisema Prof. Nagu.

Pia, ameipongeza Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga kwa kuwa na maabara bora yenye ithibati ambayo inahakikishia ubora wa majibu ya vipimo hivyo kuwezesha matibabu sahihi.

Comments

Please sign in to leave a comment.

Matangazo Muhimu

Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.

Habari na Matukio

Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.

Cookie

We use cookies to enhance your browsing experience, provide personalized content, and analyze our traffic. By clicking "Accept All Cookies", you agree to the storing of cookies on your device to improve site navigation, analyze site usage, and assist in our marketing efforts. To learn more about how we use cookies and to manage your preferences, please visit our Cookie Policy.
National Election Commission Logo

Uchaguzi 2025

Kujiandikisha Kuwa Mpiga Kura ni Msingi wa Uchaguzi Bora