logo

TAMISEMI

Students

FR
Fred Kibanofred.kibano@tamisemi.go.tz

UMITASHUMTA & UMISSETA 2025 KUFANYIKA KITAIFA MKOANI IRINGA.

OR-TAMISEMI

Mashindano ya Umoja wa Michezo na Taaluma Shule za Msingi Tanzania UMITASHUMTA na yale ya Shule za Sekondari UMISSETA kwa mwaka 2025 yanatarajiwa kufanyika Mkoani Iringa kuanzia Juni 7,2025.

Mashindano hayo yatajumuisha wanafunzi wa shule za Msingi na Sekondari kutoka Mikoa yote ya Tanzania Bara na Zanzibar, yakihusisha michezo mbalimbali kama soka kwa wavulana na Wasichana,Mpira wa kikapu, Netiboli,Wavu na Riadha.

Michezo mingine ni mpira wa Goli ambao ni maalum kwa ajili ya wanafunzi wenye uono hafifu, pamoja na Sanaa za Michezo na Burudani ambayo inahusisha ngoma za asili, kwaya na Muziki wa Kizazi kipya (Bongo Flavor).

Mashindano hayo pia yatajumuisha michezo mingine kwa wanafunzi wenye ulemavu, ikiwepo soka Wasichana na Wavulana pamoja na Riadha.

UMITASHUMTA & UMISSETA 2025 inaratibiwa na Ofisi ya Rais TAMISEMI ikishirikiana na Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia na Wizara ya Habari Sanaa Utamaduni na Michezo.

Comments

Please sign in to leave a comment.

Matangazo Muhimu

Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.

Habari na Matukio

Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.

Cookie

We use cookies to enhance your browsing experience, provide personalized content, and analyze our traffic. By clicking "Accept All Cookies", you agree to the storing of cookies on your device to improve site navigation, analyze site usage, and assist in our marketing efforts. To learn more about how we use cookies and to manage your preferences, please visit our Cookie Policy.
National Election Commission Logo

Uchaguzi 2025

Kujiandikisha Kuwa Mpiga Kura ni Msingi wa Uchaguzi Bora