logo

TAMISEMI

Students

FR
Fred Kibanofred.kibano@tamisemi.go.tz

Mchengerwa: tuulinde muungano kwa vizazi vyetu

OR-TAMISEMI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa ametoa wito kwa Watanzania kuuenzi Muungano kwa ajili ya kudumisha amani, umoja na udugu huku akipendekeza kuanzishwa kwa wiki maalum ya Muungano kwa shule zote nchini ili kukuza uelewa wa wanafunzi kuhusu historia ya Muungano.

Mhe.Mchengerwa ameyasema hayo katika kijiji cha Sangambi mkoani Mbeya baada ya kukagua na kuweka mawe ya msingi kwenye miradi ya maendeleo yenye thamani ya Sh.bilioni 40 huku wananchi wakimpongeza Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan kwa uwekezaji mkubwa.

Amehamasisha wasanii na waandishi kuendeleza simulizi za mshikamano wa kitaifa ili kudumisha Muungano huku akiwaasa wazazi kuwaelimisha vijana juu ya thamani ya Muungano.

Amesisitiza kuwa Tanzania ni mfano wa amani barani Afrika, tofauti na mataifa mengine yaliyogubikwa na migogoro na kwamba Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ulikuwa wa kweli, wa kiitikadi na kimaadili, na umeleta mafanikio makubwa kwa taifa.

Waziri Mchengerwa ampongeza Rais Samia kama alama ya mafanikio ya Muungano, akisema kuwa Tanzania imekuwa ya kwanza Afrika Mashariki kumpa mwanamke nafasi ya urais, jambo ambalo hata mataifa makubwa hayajafanikisha.

Comments

Please sign in to leave a comment.

Matangazo Muhimu

Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.

Habari na Matukio

Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.

Cookie

We use cookies to enhance your browsing experience, provide personalized content, and analyze our traffic. By clicking "Accept All Cookies", you agree to the storing of cookies on your device to improve site navigation, analyze site usage, and assist in our marketing efforts. To learn more about how we use cookies and to manage your preferences, please visit our Cookie Policy.
National Election Commission Logo

Uchaguzi 2025

Kujiandikisha Kuwa Mpiga Kura ni Msingi wa Uchaguzi Bora