logo

TAMISEMI

Students

FR
Fred Kibanofred.kibano@tamisemi.go.tz

Mchengerwa: Mhe.Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa kipaumbele kwa Serikali za Mitaa kuchochea maendeleo

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa amesema Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameendelea kuweka mkazo katika kuimarisha serikali za mitaa kama chachu ya maendeleo ya wananchi kwa kuongeza rasilimali, kuboresha mifumo ya utendaji, na kuimarisha uwajibikaji wa viongozi wa halmashauri.

Waziri Mchengerwa amesema hayo Machi 11, 2025 kwenye ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa 39 wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) uliofanyika jijini Dodoma.

“Maendeleo siyo ahadi, bali ni hatua zinazochukuliwa kila siku kwa vitendo. Tunamshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwa mstari wa mbele kuhakikisha serikali za mitaa zinakuwa msingi wa maendeleo ya wananchi. Serikali yake imeonesha kuwa maendeleo yanaanzia chini kwenda juu, na kwa kuimarisha serikali za mitaa, tumewawezesha wananchi kushiriki moja kwa moja katika mchakato wa maendeleo,” amesema Mhe. Mchengerwa.

Ameeleza kuwa uwekezaji mkubwa umefanyika katika sekta ya elimu, afya, na miundombinu, hatua inayowezesha wananchi kushiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi.

Aidha, Waziri Mchengerwa amewahimiza viongozi wa serikali za mitaa kuwa wabunifu, kuzingatia uadilifu katika utendaji wao, na kushirikiana na serikali kuu ili kuhakikisha maendeleo ya taifa yanapiga hatua kwa kasi zaidi.

Comments

Please sign in to leave a comment.

Matangazo Muhimu

Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.

Habari na Matukio

Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.

Cookie

We use cookies to enhance your browsing experience, provide personalized content, and analyze our traffic. By clicking "Accept All Cookies", you agree to the storing of cookies on your device to improve site navigation, analyze site usage, and assist in our marketing efforts. To learn more about how we use cookies and to manage your preferences, please visit our Cookie Policy.
National Election Commission Logo

Uchaguzi 2025

Kujiandikisha Kuwa Mpiga Kura ni Msingi wa Uchaguzi Bora