
LAAC yataka Utekelezaji wa miradi uzingatie Miongozo na Kanuni
OR-TAMISEMI
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), imeielekeza Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mlimba kuhakikisha inazingatia miongozo na kanuni katika utekelezaji wa miradi.
Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Halima Mdee ametoa maelekezo hayo baada ya ukaguzi wa miradi miwili ambayo ni nyumba ya Mkurugenzi wa Halmashauri na kukagua mradi wa wodi tatu (wanaume, wanawake, na watoto) katika hospitali ya Halmashauri.
“Ofisa Masuhuri ahakikishe miradi yote inayotekelezwa inafuata miongozo, sheria, na kanuni zinazotolewa na Ofisi ya Rais – TAMISEMI,” amesisitiza.
Amesema kamati imeongeza kuwa matumizi sahihi ya miongozo, sheria, na kanuni ni muhimu katika kuhakikisha miradi inatekelezwa kwa kuzingatia thamani ya fedha na kuepusha matumizi mabaya ya rasilimali.
Naye, Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Mhe. Dkt. Festo Dugange, amesema kuwa ofisi yake imepokea maelekezo hayo na tayari imeanza kuyafanyia kazi kwa utekelezaji.
Comments
Please sign in to leave a comment.
Matangazo Muhimu
Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.
ADDITIONAL BEST INDICATORS 2025
TANGAZO LA KUITWA KAZINI NAFASI ZA KUJITOLEA SHULE ZA MSINGI KADA YA ELIMU MRADI WA GPE - TSP
ORODHA YA WALIMU WALIOCHAGULIWA NAFASI ZA KUJITOLEA SHULE ZA MSINGI MRADI WA GPE TSP
BASIC EDUCATION STATISTICS 2025
TANGAZO LA KUITWA KAZINI AJIRA YA MKATABA PROGRAMU YA TIMCHIP
Habari na Matukio
Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.




