
LAAC yataka hatua dhidi ya watumishi wazembe Mbeya zichukuliwe
Na OR-TAMISEMI, Mbeya
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), chini ya Mwenyekiti wake Mhe. Halima Mdee, imeielekeza Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya kuchukua hatua dhidi ya watumishi wanaokwamisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo.
Maelekezo hayo yametolewa katika kikao cha majumuisho baada ya ziara ya siku tatu ya ukaguzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa mkoani humo.
"Ofisi ya Mkuu wa Mkoa ichukue hatua za kinidhamu kwa watumishi wote watakaobainika kukwamisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo," amesisitiza
Aidha, Kamati imeitaka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kuongeza kasi ya ufuatiliaji wa miradi yote ya maendeleo, ikiwemo kubaini changamoto zinapojitokeza mapema ili kuepusha athari katika utekelezaji wake.
Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Atupele Mwambene, amesema kuwa Ofisi ya Rais – TAMISEMI imechukua maelekezo hayo na itayafanyia kazi kwa kuhakikisha utekelezaji wake unafuatiliwa ipasavyo.
Kamati hiyo imetembelea na kukagua miradi katika Halmashauri ya Wilaya ya Kyela, Halmashauri ya Wilaya ya Chunya, na Halmashauri ya Wilaya ya Mbalizi, mkoani Mbeya.
Comments
Please sign in to leave a comment.
Matangazo Muhimu
Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.
ADDITIONAL BEST INDICATORS 2025
TANGAZO LA KUITWA KAZINI NAFASI ZA KUJITOLEA SHULE ZA MSINGI KADA YA ELIMU MRADI WA GPE - TSP
ORODHA YA WALIMU WALIOCHAGULIWA NAFASI ZA KUJITOLEA SHULE ZA MSINGI MRADI WA GPE TSP
BASIC EDUCATION STATISTICS 2025
TANGAZO LA KUITWA KAZINI AJIRA YA MKATABA PROGRAMU YA TIMCHIP
Habari na Matukio
Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.




