logo

TAMISEMI

Students

FR
Fred Kibanofred.kibano@tamisemi.go.tz

LAAC yataka hatua dhidi ya watumishi wazembe Mbeya zichukuliwe

Na OR-TAMISEMI, Mbeya

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), chini ya Mwenyekiti wake Mhe. Halima Mdee, imeielekeza Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya kuchukua hatua dhidi ya watumishi wanaokwamisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Maelekezo hayo yametolewa katika kikao cha majumuisho baada ya ziara ya siku tatu ya ukaguzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa mkoani humo.

"Ofisi ya Mkuu wa Mkoa ichukue hatua za kinidhamu kwa watumishi wote watakaobainika kukwamisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo," amesisitiza

Aidha, Kamati imeitaka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kuongeza kasi ya ufuatiliaji wa miradi yote ya maendeleo, ikiwemo kubaini changamoto zinapojitokeza mapema ili kuepusha athari katika utekelezaji wake.

Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Atupele Mwambene, amesema kuwa Ofisi ya Rais – TAMISEMI imechukua maelekezo hayo na itayafanyia kazi kwa kuhakikisha utekelezaji wake unafuatiliwa ipasavyo.

Kamati hiyo imetembelea na kukagua miradi katika Halmashauri ya Wilaya ya Kyela, Halmashauri ya Wilaya ya Chunya, na Halmashauri ya Wilaya ya Mbalizi, mkoani Mbeya.

Comments

Please sign in to leave a comment.

Matangazo Muhimu

Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.

Habari na Matukio

Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.

Cookie

We use cookies to enhance your browsing experience, provide personalized content, and analyze our traffic. By clicking "Accept All Cookies", you agree to the storing of cookies on your device to improve site navigation, analyze site usage, and assist in our marketing efforts. To learn more about how we use cookies and to manage your preferences, please visit our Cookie Policy.
National Election Commission Logo

Uchaguzi 2025

Kujiandikisha Kuwa Mpiga Kura ni Msingi wa Uchaguzi Bora