logo

TAMISEMI

Students

FR
Fred Kibanofred.kibano@tamisemi.go.tz

LAAC yaielekeza iringa kukamilisha ujenzi wa uzio wa madarasa ya Awali

Na OR-TAMISEMI, Iringa

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC),  imeielekeza Halmashauri ya Manispaa ya Iringa Mjini kuhakikisha inakamilisha ujenzi wa uzio katika madarasa ya awali ya Shule ya Msingi Uyole.

Maelekezo hayo yametolewa katika kikao cha majumuisho baada ya Kamati hiyo kufanya ziara ya kukagua miradi ya maendeleo katika Halmashauri hiyo na Mjumbe wa Kamati hiyo ambaye Mbunge wa Kilindi, Mhe. Omary Kigua kwa niaba ya Mwenyekiti wa LAAC, Halima Mdee.

Amesema “Afisa Masuhuri hakikisha uzio katika madarasa ya awali uwe umejengwa kabla ya kukamilika kwa mwaka wa fedha 2025/26, na taarifa ya ujenzi huo iwasilishwe kwa CAG kwa ajili ya mapitio.”


Pia, Amesema Kamati imeelekeza Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo kuhakikisha kuwa ujenzi wa jengo la kufulia katika Kituo cha Afya Itamba unakamilika kabla ya mwisho wa mwaka huu wa fedha.


Naye, Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Mhe. Dkt. Festo Dugange, amesema kuwa serikali kupitia TAMISEMI itafanyia kazi mapungufu yote yaliyoainishwa na Kamati ili kuhakikisha miradi inatekelezwa kwa viwango vinavyokubalika kwa manufaa ya wananchi.

Miradi iliyokaguliwa na kamati hiyo ni pamoja na Ujenzi wa machinjio ya kisasa Ngelewala, Ujenzi wa Shule ya Msingi ya Mkondo Mmoja Uyole na Ujenzi wa Kituo cha Afya Itamba ambapo kamati imesisitiza ikamilike kwa wakati ili kuboresha huduma kwa wananchi wa Iringa.

Comments

Please sign in to leave a comment.

Matangazo Muhimu

Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.

Habari na Matukio

Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.

Cookie

We use cookies to enhance your browsing experience, provide personalized content, and analyze our traffic. By clicking "Accept All Cookies", you agree to the storing of cookies on your device to improve site navigation, analyze site usage, and assist in our marketing efforts. To learn more about how we use cookies and to manage your preferences, please visit our Cookie Policy.
National Election Commission Logo

Uchaguzi 2025

Kura yako haki yako jitokeze kupiga kura