logo

TAMISEMI

Students

FR
Fred Kibanofred.kibano@tamisemi.go.tz

Laac yaagiza ujenzi wa hospitali ya mji ifakara ukamilike

Na OR-TAMISEMI, Ifakara

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), imeielekeza Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Ifakara kuhakikisha ujenzi wa hospitali ya mji huo unakamilika kwa wakati ili wananchi wapate huduma bora za afya.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Halima Mdee, ametoa maelekezo hayo baada ya kutembelea na kukagua miradi miwili ya maendeleo ambayo ni ujenzi wa jengo la utawala na ujenzi wa hospitali ya Mji wa Ifakara.

"Afisa Masuuli aondoe dosari zote zilizobainishwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ili mradi huu ukamilike na kutoa huduma kamili kwa wananchi. Aidha, taarifa ya kila robo mwaka ya maendeleo ya ujenzi huu iwasilishwe kwa CAG kwa ajili ya uhakiki," amesisitiza Mhe. Mdee.

Pia, amemtaka Afisa Masuuli kuhakikisha kuwa zaidi ya Sh. milioni 133, ambazo zilichukuliwa kutoka kwenye fedha zilizotolewa na Serikali Kuu kwa ajili ya ujenzi wa hospitali hiyo, zinarudishwa ili kuendeleza mradi huo.

Vilevile, Mhe. Mdee ameelekeza kuwa utekelezaji wa miradi katika halmashauri hiyo uzingatie sheria, kanuni, na miongozo inayotolewa na Ofisi ya Rais – TAMISEMI.

Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Atupele Mwambene, amesema kuwa ofisi yake imepokea maelekezo hayo na itahakikisha yanatekelezwa kikamilifu kwa usimamizi wa Halmashauri ya Mji wa Ifakara.

Comments

Please sign in to leave a comment.

Matangazo Muhimu

Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.

Habari na Matukio

Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.

Cookie

We use cookies to enhance your browsing experience, provide personalized content, and analyze our traffic. By clicking "Accept All Cookies", you agree to the storing of cookies on your device to improve site navigation, analyze site usage, and assist in our marketing efforts. To learn more about how we use cookies and to manage your preferences, please visit our Cookie Policy.
National Election Commission Logo

Uchaguzi 2025

Kura yako haki yako jitokeze kupiga kura