logo

TAMISEMI

Students

FR
Fred Kibanofred.kibano@tamisemi.go.tz

Katimba atembelea banda la TAMISEMI kwenye Kongamano la Kimataifa na Maonesho ya Elimu Mtandao Jijini Dar es Salaam

Naibu Waziri anayeshughuhulikia Elimu Ofisi ya Rais - TAMISEMI   Mhe.Zainab Katimba atembelea banda la TAMISEMI kwenye Kongamano la Kimataifa na Maonesho ya Elimu Mtandao Jijini Dar es Salaam.

Mheshimiwa Zainab Katimba ametembelea banda la maonesho la Ofisi ya Rais -TAMISEMI kwenye Kongamano la 18 la kimataifa na Maonesho ya Elimu Mtandao, Mafunzo na Maendeleo ya Kukuza Ujuzi yanayoendelea katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere Jijini Dar es Salaam kuanzia leo Mei 7 hadi 9, 2025.

Mheshimiwa Katimba amejionea jinsi Mfumo wa Taarifa za Shule (SIS) unavyofanya kazi kwa kukusanya taarifa za shule za kila siku kupitia moduli mbalimbali zilizounganishwa na Mfumo huo.

Pia amepata maelezo ya namna ya darasa janja (smart class) linavyofanya kazi za kufundisha na kutoa mafunzo kama sehemu ya Elimu Mtandandao (eLearning).

Maonesho na Kongamano hilo la Elimu Mtandao yanajulikana kama “eLearnging Africa’ yanafanyika kwa mara ya pili Tanzania na mara ya kwanza yalifanyika mwaka 2007, yameandaliwa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ikiwahusisha wadau mbalimbali kutoka Wizara, Taasisi, Mashirika ya Kimataifa na Wadau wengine na Kauli Mbiu yake ni “Kufikiri Upya Elimu na Maendeleo ya Rasilimali Watu kwa ustawi wa Baadae wa Afrika”

Comments

Please sign in to leave a comment.

Matangazo Muhimu

Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.

Habari na Matukio

Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.

Cookie

We use cookies to enhance your browsing experience, provide personalized content, and analyze our traffic. By clicking "Accept All Cookies", you agree to the storing of cookies on your device to improve site navigation, analyze site usage, and assist in our marketing efforts. To learn more about how we use cookies and to manage your preferences, please visit our Cookie Policy.
National Election Commission Logo

Uchaguzi 2025

Kujiandikisha Kuwa Mpiga Kura ni Msingi wa Uchaguzi Bora