logo

TAMISEMI

Students

AN
Angela Msimbilaangela.msimbila@tamisemi.go.tz

Halmashauri zatakiwa kupima maeneo ya huduma za afya na kupata hati miliki

Mkurugenzi wa Idara ya Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI, Dkt. Rashid Mfaume, amezitaka Mamlaka za Serikali za Mitaa kuhakikisha zinapima ardhi za Zahanati, Vituo vya Afya, na Hospitali zote nchini ili kupata hati miliki za maeneo hayo.

Dkt. Mfaume ametoa ushauri huo alipokuwa katika ziara ya ukaguzi wa huduma za afya, lishe, na ustawi wa jamii katika Mkoa wa Dodoma, ambapo alitembelea Kituo cha Afya Kibakwe kilichopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa.

“Ni lazima tupime maeneo yetu, tuweke mipaka rasmi na kuhakikisha yanakuwa na hati miliki ili kuzuia uvamizi na kuimarisha utoaji wa huduma za afya,” amesema Dkt. Mfaume.

Ameongeza kuwa kasi ya ukuaji wa miji inasababisha watu kuhamia karibu na vituo vya huduma, hivyo upimaji wa maeneo hayo utasaidia kulinda miundombinu ya afya dhidi ya uingiliaji usio rasmi.

Comments

Please sign in to leave a comment.

Matangazo Muhimu

Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.

Habari na Matukio

Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.

Cookie

We use cookies to enhance your browsing experience, provide personalized content, and analyze our traffic. By clicking "Accept All Cookies", you agree to the storing of cookies on your device to improve site navigation, analyze site usage, and assist in our marketing efforts. To learn more about how we use cookies and to manage your preferences, please visit our Cookie Policy.
National Election Commission Logo

Uchaguzi 2025

Kura yako haki yako jitokeze kupiga kura