logo

TAMISEMI

Students

FR
Fred Kibanofred.kibano@tamisemi.go.tz

Dkt. Mfaume: TAMISEMI tumejipanga vyema utekelezaji wa sheria ya Bima ya Afya kwa Wote

Mkurugenzi wa Idara ya Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI, Dkt. Rashid Mfaume, amesema kuwa katika kuelekea utekelezaji wa Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote, TAMISEMI imejipanga vyema kuhakikisha kunakuwa na usimamizi bora huduma za afya katika ngazi ya msingi. 

Dkt. Mfaume ametoa kauli hiyo alipokuwa katika ziara yake ya kukagua utoaji wa huduma za afya, lishe, na ustawi wa jamii mkoani Dodoma, ambapo alitembelea Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa.

Amesema TAMISEMI itahakikisha katika ngazi ya afya ya msingi bidhaa zote muhimu za afya zinapatikana.

"Tunawahakikishia Watanzania kuwa katika ngazi ya huduma za afya ya msingi, Ofisi ya Rais TAMISEMI imejipanga kuhakikisha wananchi wote wanaojiunga na Bima ya Afya kwa Wote wanapata huduma zote stahiki kama inavyotakiwa," amesema Dkt. Mfaume.

Aidha, amebainisha kuwa hapo awali kulikuwapo na changamoto ya baadhi ya wanachama wa bima ya afya kukosa dawa katika vituo vya kutolea huduma na kulazimika kununua dawa hizo wenyewe.

Hata hivyo, kwa sasa TAMISEMI imechukua hatua kuhakikisha vituo vya afya vinakuwa na akiba ya kutosha ya dawa na vifaa tiba ili kuboresha huduma kwa wananchi

Comments

Please sign in to leave a comment.

Matangazo Muhimu

Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.

Habari na Matukio

Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.

Cookie

We use cookies to enhance your browsing experience, provide personalized content, and analyze our traffic. By clicking "Accept All Cookies", you agree to the storing of cookies on your device to improve site navigation, analyze site usage, and assist in our marketing efforts. To learn more about how we use cookies and to manage your preferences, please visit our Cookie Policy.
National Election Commission Logo

Uchaguzi 2025

Kujiandikisha Kuwa Mpiga Kura ni Msingi wa Uchaguzi Bora