Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

WAZIRI MKUU AAGIZA WAKUU WA WILAYA KUKUTANA NA WAFUGAJI

Imewekwa tar.: December 26th, 2022

*Asisitiza vikao vya pamoja vya maridhiano ya wakulima na wafugaji

MOROGORO

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameagiza Wakuu wa Wilaya kuitisha vikao na wafugaji ili kujadiliana na kuweka namna bora ya kufanya shughuli za ufugaji ikiwa ni pamoja na kutambua mifugo yote iliyoko ndani ya Wilaya husika na kuweka zuio la mifugo mingine kuingizwa katika wilaya zao.

Mheshimiwa Majaliwa pia ameagiza viongozi katika mikoa na wilaya kuweka mpango wa matumizi bora ya ardhi kwenye maeneo yote yenye wafugaji na wakulima ambapo pia kuna vyanzo vya maji.

Amesema kuwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan anataka kuona uharibufu wa vyanzo vyote vya maji vinadhibitiwa kwa kuwekewa mpango mkakati utakaowezesha kuyatunza maeneo hayo dhidi ya uharibifu wa aina yeyote.

Amesema hayo leo Jumamosi (Disemba 24, 2022) wakati akiongoza kikao cha pamoja na Mawaziri wa Kisekta, Makatibu na Naibu Makatibu wakuu kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa na Wilaya za Morogoro wadau na wasimamizi wa masuala ya ardhi na mifugo ili kutatua, changamoto za usimamizi wa masuala ya ardhi ndani ya Mkoa huo.

Kikao hicho kimefuatia maagizo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan aliyoyatoa Desemba 22, 2022 Wakati akifunga njia ya kuchepusha maji na kuanza ujazaji maji kwenye bwawa la kuzalisha umeme la Julius Nyerere (JNHPP).

“Agizo la Mheshimiwa Rais ni lazima litekelezwe kwa sisi wasaidizi kutimiza wajibu wetu na kuweka mikakati ya kutekeleza agizo hilo kwa ufanisi.”

Katika hatua nyingine Mheshimiwa Majaliwa amewataka wakuu wa Wilaya kuunda kamati za maridhiano baina ya wafugaji na wakulima, ili kutengeneza umoja kati ya makundi hayo mawili “Wafugaji washirikishwe kuandaa miundombinu ambayo wanyama wao wataitumia kupata malisho, maji pamoja na majosho”

Aidha, Mheshimiwa Waziri Mkuu amekemea vitendo vya rushwa kuanzia kwenye ngazi ya viongozi wa Serikali za vijiji “unakuta kiongozi wa kijiji anaruhusu wafugaji kutoka maeneo mbalimbali kwasababu tu amepewa rushwa na anasahau athari ambazo wanazipata wanavijiji wao”

“Jambo lingine muhimu tutambue maeneo yote ya vyanzo vya maji, pamoja na kutambua maeneo ambayo ng’ombe wanaingia katika maeneo ya vyanzo vya maji na kuwaondoa wote ili maji yaendelee kutirika kuelekea katika bwawa la umeme”

Waziri Mkuu amekubaliana na maombi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro la kuwaondoa wafugaji walioko katika eneo la mto kilombero ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Mheshimiwa Rais Dkt.Samia.

Awali, akizungumza katika kikao hicho Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Fatma Mwasa amesema hali ya usimamizi wa ardhi na vyanzo vya maji kwa Mkoa wa Morogoro si ya kuridhisha kwani maeneo mengi ya vyanzo vya maji yameathirika hivyo zinahitajika jitihada za haraka kunusuru hali hiyo.

“Maeneo ya madakio ya maji ya mto kilombero hadi sasa yameathirika kwa asilimia 80 na asilimia 20 iliyobaki ndio inayotegemewa kuzalisha maji katika mto huo tusipochukua hatua sasa hali itakuwa mbaya zaidi.


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert May 12, 2025
  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert May 12, 2025
  • Fursa kwa Wahitimu wa Kidato cha Nne 2024 kubadili Tahasusi na Kozi April 02, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI AJIRA ZA AFYA - TAMISEMI 2025 March 15, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI

    May 23, 2025
  • PJT-MMMAM Yawezesha Uanzishwaji wa Vituo 206 vya Malezi ya Watoto Wadogo

    May 21, 2025
  • SERIKALI KUJENGA DARAJA LINALOUNGANISHA KIJIJI CHA NEGERO – KILINDI

    May 21, 2025
  • MHE. MCHENGERWA ABORESHA TAARIFA ZAKE KWENYE  DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

    May 20, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.